Leo Jumatatu 29 Juni, Mbagala hakuna umeme

Leo Jumatatu 29 Juni, Mbagala hakuna umeme

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
23,893
Reaction score
29,214
Umeme ulianza kukatika na kuwaka mara kadhaa usiku wa manane, ilipofika alfajiri umeme ukapiga baibai my sani, ndiyo kwaheri hiyo haujarudi. Je, huko kwingine umeme upo? Kwa hali hii hayo maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yaliyoanza jana Jumapili hayataathirika?
 
Tukisema kuwa nchi imekufa mnatuona vichaa
 
Umeme ulianza kukatika na kuwaka mara kadhaa usiku wa manane, ilipofika alfajiri umeme ukapiga baibai my sani, ndiyo kwaheri hiyo haujarudi. Je, huko kwingine umeme upo? Kwa hali hii hayo maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yaliyoanza jana Jumapili hayataathirika?
Umeme wa MAMA
 
Kwa hali hii hayo maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yaliyoanza jana Jumapili hayataathirika?
7.7 bado haijafika labda mitambo imejizima wanafanya mazoezi ya kuzima umeme nchi nzima na kuzima internet nchi nzima ili tucheze gizani unataka kuuliza nini?
 
Tukisema kuwa nchi imekufa mnatuona vichaa

Umeme kukatika Mbagala tu👈

wilaya ya Temeke eneo kubwa Umeme upo✅️ kwenu nchi inaweza kufa kwa kukatika Umeme tu🫎🫎🫎

Akili kama izi lazima kuna mtu anafaidika !!!
kwa tone tone au kwa Sadaka ❗️
 
Umeme kukatika Mbagala tu👈

wilaya ya Temeke eneo kubwa Umeme upo✅️ kwenu nchi inaweza kufa kwa kukatika Umeme tu🫎🫎🫎

Akili kama izi lazima kuna mtu anafaidika !!!
kwa tone tone au kwa Sadaka ❗️
Fanya hivi mtandao wa simu na wewe wakala siku mbili mbagara ufanyi kazi.Kinyeo wewe
 
Umeme ulianza kukatika na kuwaka mara kadhaa usiku wa manane, ilipofika alfajiri umeme ukapiga baibai my sani, ndiyo kwaheri hiyo haujarudi. Je, huko kwingine umeme upo? Kwa hali hii hayo maonesho ya kimataifa ya Sabasaba yaliyoanza jana Jumapili hayataathirika?
Habari, Ndugu Mteja.

Asante kwa kuwasiliana na TANESCO Huduma kwa Wateja.

Pole sana kwa changamoto uliyoipata. Aidha, tunaomba radhi kwa kuchelewa kukujibu kutokana na changamoto ya muda (temporary) iliyojitokeza kwenye akaunti yetu, iliyosababisha ujumbe wako kutufikia kwa kuchelewa.

Tafadhali fahamu kuwa pale tunapolazimika kusitisha huduma ya umeme kwa ajili ya matengenezo yaliyopangwa au kutokana na hitilafu za dharura, huwa tunatoa taarifa mapema kadiri inavyowezekana, zikieleza sababu za usitishaji wa huduma, maeneo yatakayoathirika na, pamoja na muda unaotarajiwa wa kurejea kwa huduma.

Taarifa hizi hutolewa kupitia njia mbalimbali rasmi za mawasiliano, ikiwemo ujumbe mfupi wa simu (SMS) na makundi yetu rasmi ya WhatsApp yaliyopangwa kulingana na mikoa, wilaya na maeneo mbalimbali.
Iwapo hukupokea taarifa hizo, tunaomba radhi kwa usumbufu uliotokea.

Ikiwa ungependa kuzipokea kwa wakati, tafadhali tutumie namba yako ya WhatsApp kupitia inbox, pamoja na jina la wilaya na mkoa unaoishi, ili tukuunganishe kwenye kundi husika na pia kukujumuisha kwenye mfumo wetu wa ujumbe mfupi wa simu (Bulk SMS).Asante kwa uvumilivu na ushirikiano wako. ^CM
 
Back
Top Bottom