Habari za wakati huu wana bodi wenzangu,
Ama kwa hakika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi muhimu cha kujitakasa na kukaa mbali na dhambi na kutomkaribia shetani.
Kwa mantiki hiyo nimefikiria kwa kina kwamba kuendelea kuwa mwanachama wa chadema chama kinachoongozwa na watu wasio na maadili mema kwa jamii ni kumkufuru Mwenyezi Mungu.
Pili, binafsi nimechoswa na siasa zisizo na mwelekeo kwa sababu chama mpaka sasa hakijielewi dira yake kamili ni ipi tunasikia tu mara Ukawa mara matamko ya wajumbe mara operesheni pamoja daima mara Zitto yaani ni mambo ya hovyo hovyo.
Sasa naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi na viumbe vyote hapa duniani inshaallah ikifika saa12 muda wa adhana nachoma kadi ya chadema. Sina haja ya kuirudisha kwa sababu itakuwa ni sawa na kuwa Katibu Mwenezi wa shetani.
Ramadhan Kareem[/QUOTE
Samahani ndugu, usiichannganye dini yetu na upuuzi wako wa siasa za kipumbavu. Mpuuzi kama wewe unaweza kutamka mambo ya futari sijui nini kumbe uko guest saa hz, halafu ujue kwa waisilamu huu ni mwezi wa toba na chuki tunaweka pembeni wewe kafiri unajificha kwenye uisilamu na siasa zako za majitaka.
kweli kabisa huyu jamaa anataka kutuletea dharau hajui kuwa huu ni mwezi mtukufu.