Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Leo asubuhi kulitokea mabishano home

Ukitoa toa bila kukumbuka wala kufuatilia... mambo yake muachie mwenyewe...
 
Habari waungwana.

Habari ipo hivi. Nyumbani tuna House gal ambaye Kama kawaida husaidia kazi za Nyumbani pamoja na kulea watoto .Sasa wkt anakuja nikagundua Hana nguo za kutokea kwa maana mfano kutokea tukienda mahali au akiumwa au akienda tembelea ndugu ZAKE weekend.

Nilichofanya nikampa nguo yangu moja NZURI ambayo hata Mimi ni zile za kanisani au kwenda sehemu special na pia nikamuongezea na za kushindia kwa maana za Nyumbani Kama anafanyafanya shughuli ndogo ndogo ,lakini wkt Nampa nilimfafanulia na Tena siku iyo nakumbuka alifurahi Sana na ni siku alikuwa anaenda kusalimia ndugu zake ilibidi avue Ile aliyokuwa ameivaa na kuvaa ile niliyompa akisema anashukuru Sana na ameipenda Sana .

Na alipovaa ni Kama alipimwa ilimpendeza Sana. Baada ya Kama wiki nikagundua Ile nguo ameigeuza ya kushindia na NDO anafanyia usafi.Nikamwita nikamwelekeza kwa Nini asivae zile zingine kwa maana Ile uwe Kama nilivyomuelezea.Akaelewa akaivua na kuifua.

Sasa Leo asubuhi naamka nikamkuta ameivaa anaifagilia nje na hata Jana yake aliivaa anamenyea nduzi(nikiongelea hivyo nduzi Zina utonvu na ni nyeupe) Nikamuuliza mbona umerudia kuifubaisha nguo NZURI na nilikuelezea? Nikamwambia vua ntampa hata ndugu yangu atakayeithamini.

Sasa Baba watoto akasema Kwanza Iyo nguo kumpangia masharti aivae vipi umekosea kwa kuwa wakati unampa hakukuomba ulimpa mwenyewe na kanuni ya kumpa mtu kitu chochote ukishampa umempa matumizi ni juu yake hata angeamua kudekia kufanyaje ni yeye maana imekuwa yake.

Kweli Kama mama nimeshangaa Sana kwa hizo kauli. Je Mimi makosa yangu ni yapi au ni kweli mtoto ndani ya nyumba hupaswi kumshauri(Huyo msichana Ana miaka 18 kwenda 19) Na ikumbukwe ni mista huyo huyo aliyenilalamikia kwamba huyo msichana tangia aje anavaa vinguo vyepesi na khanga tu akijua na yeye yupo kwa maana Kama Ana majaribu na akimfananisha na dada mwingine ambaye aliondoka ambavyo hakuwa na majaribu Kama ya huyu wa Sasa kwa maana kujipitisha Mara kajilaza ovyo Yaani Mambo Kama hayo.

(Kwa hayo malalamiko yake nikaongea na Dada nikamshauri jinsi ya kuvaa na hasa azingatie nguo za heshima.Walau akabadirika.
Sasa Leo NDO hayo.

Naombeni maoni na mista atawasoma Mana kajaa tele humu
Ukiona anaivaa kilasiku ujue anaipenda Sana kuliko nguo zote kwaiyo hutakiwi kumzui
 
Mi nilinunua jeans kali 25000 enzi hizo ikanibana kiuno ikiwa mpya kabisa nikampa ndugu yangu mtoto wa ba mdogo kesho yake akaikata pensi,
Nyeye alikuwa anapenda pensi kwaiyo hakufanya kosa kila mtu ana penda nguo za tofauti na wengine
 
MKE WANGU HAYA MAMBO TUMEJADILI NYUMBANI KAMA FAMILIA, NI KWANINI UMEAMUA KUYALETA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII HUKU?
 
Zinazoitwa changamoto za ndoa mnazishughulikia vipi ikiwa jambo dogo kama hili limeleta mpasuko ndani ya nyumba?
Ni kweli nguo uliompa ndio ameipenda na zingine kaziona tambara kama wewe ulivyoona ni nguo za kuburuta kwa shughuli za nyumbani.
Hao ndugu zako hukuweza kuwapa hiyo nguo kabla ya kuona kuwa house girl anaiharibu?
Pengine Mr kamwambia avae hiyo badala ya vipande vya matambara ya kanga au nguo za ajabu alizokuwa anavaa ili kuepusha balaa ndani ya nyumba.
 
Heloo, nadhani unasahau kuwa huyo HG anatoka katika familia gani. Hapo alipo ni kama yupo 5 star hotel na anaona ni vyema akawa smart kila wakati.
Usisahau, ukimtuma HG dukani, lazima aingie bafuni kuoga na ajikwatue. Huo ni umri unasumbua na mazingira aliyomo yanamzuzua. Kwa mantiki hiyo ndo maana kila siku anapenda kuivaa hiyo nguo hata akiwa anamenya ndizi zenye utomvu.

Kwa wengine wote, usitoe zawadi kwa mtu yeyote awe mtoto, mpenzi etc zawadi yenye thamani kubwa! Kwa kawaida zawadi huwa ni ile ambayo hata mkiachana au mkakasirikiana hutaitumia kama fimbo. Hata kama ni rafiki, urafiki ukikoma unamwachia na haitakuuma. Ndiyo maana humu tunaambiwa Mchumba hasomeshi. Ukimpa mtu zawadi usiifuatilie! Mfano ukimjengea mwanamke nyumba, hata mkiachana unaondoka bila kinyongo na hata ukikuta njemba imetanua miguu, usiumie. Kama unadhani utaumia acha usimjengee nyumba maana hiyo si zawadi bali CHAMBO.
 
Haaaa haaaa wanaume wanachelewa Basi muda tu inakuwa bado au mtu awe na hofu ya Mungu
Hapa ndipo unapopaswa kuwa mvumilivu kwa hayo ya dada wa kazi kwa maslahi mapana ya wanao (familia).
 
Point taken.
Ila Mimi Nina moyo flan flagile Kuepuka hayo sitampa Tena nguo yangu ya thamani Basi.Mana ntaonekana namnyanyasa
Sawa mpendwa, huo pia n uamuz wa busara 😊
 
Habari waungwana.

Habari ipo hivi. Nyumbani tuna House gal ambaye Kama kawaida husaidia kazi za Nyumbani pamoja na kulea watoto .Sasa wkt anakuja nikagundua Hana nguo za kutokea kwa maana mfano kutokea tukienda mahali au akiumwa au akienda tembelea ndugu ZAKE weekend.

Nilichofanya nikampa nguo yangu moja NZURI ambayo hata Mimi ni zile za kanisani au kwenda sehemu special na pia nikamuongezea na za kushindia kwa maana za Nyumbani Kama anafanyafanya shughuli ndogo ndogo ,lakini wkt Nampa nilimfafanulia na Tena siku iyo nakumbuka alifurahi Sana na ni siku alikuwa anaenda kusalimia ndugu zake ilibidi avue Ile aliyokuwa ameivaa na kuvaa ile niliyompa akisema anashukuru Sana na ameipenda Sana .

Na alipovaa ni Kama alipimwa ilimpendeza Sana. Baada ya Kama wiki nikagundua Ile nguo ameigeuza ya kushindia na NDO anafanyia usafi.Nikamwita nikamwelekeza kwa Nini asivae zile zingine kwa maana Ile uwe Kama nilivyomuelezea.Akaelewa akaivua na kuifua.

Sasa Leo asubuhi naamka nikamkuta ameivaa anaifagilia nje na hata Jana yake aliivaa anamenyea nduzi(nikiongelea hivyo nduzi Zina utonvu na ni nyeupe) Nikamuuliza mbona umerudia kuifubaisha nguo NZURI na nilikuelezea? Nikamwambia vua ntampa hata ndugu yangu atakayeithamini.

Sasa Baba watoto akasema Kwanza Iyo nguo kumpangia masharti aivae vipi umekosea kwa kuwa wakati unampa hakukuomba ulimpa mwenyewe na kanuni ya kumpa mtu kitu chochote ukishampa umempa matumizi ni juu yake hata angeamua kudekia kufanyaje ni yeye maana imekuwa yake.

Kweli Kama mama nimeshangaa Sana kwa hizo kauli. Je Mimi makosa yangu ni yapi au ni kweli mtoto ndani ya nyumba hupaswi kumshauri(Huyo msichana Ana miaka 18 kwenda 19) Na ikumbukwe ni mista huyo huyo aliyenilalamikia kwamba huyo msichana tangia aje anavaa vinguo vyepesi na khanga tu akijua na yeye yupo kwa maana Kama Ana majaribu na akimfananisha na dada mwingine ambaye aliondoka ambavyo hakuwa na majaribu Kama ya huyu wa Sasa kwa maana kujipitisha Mara kajilaza ovyo Yaani Mambo Kama hayo.

(Kwa hayo malalamiko yake nikaongea na Dada nikamshauri jinsi ya kuvaa na hasa azingatie nguo za heshima.Walau akabadirika.
Sasa Leo NDO hayo.

Naombeni maoni na mista atawasoma Mana kajaa tele humu
una gubu sana,ndoa itakushinda
msikilize mista
 
Punguza wivu ...!
Nawewe vaa vizuri tupia picha humu tukusifie..!
 
Umejuaje watu 8 bana .

Hahah basi tu nimejaribu kusoma mwandiko....

Hata hivyo hakuna haja ya kumpoka huyo binti hiyo nguo, umetenda wema kumsaidia, wewe enenda zako...

Somo ulilojifunza ni kwamba, vitu unavyovijali wewe si wote huvijali kwa kiwango kilekile...
 
Noted.
Sio mdogo wangu tu hata mtoto wa kumzaa wananguo zao special but point yako hii imenikumbusha kitu Mimi Nina watoto 2 mmoja mkubwa kidogo miaka 10 mwingine huyu mwaka 1.
Huyu huyu Dada nikitoka kazini nakuta kachukua zile nguo kwenye begi lake la nguo za kutokea yeye NDO anashinda nazo Napo nikamwelekeza usiwe unamshindishia hizo kwanza rahisi kufubaa na why wkt za kawaida na NZURI za Nyumbani zipo.Somo langu la Leo naona gumu kwa wengine na wengine wameelewa .Sasa hata wewe mpenzi hunaga tunguo flani tea safari au mtoko?labda hapo NDO kwenye utata
Nakuelewa sana, ulikuwa na maana nzuri, lakini pia huyo ni mtu mzima ameamua kuishi kwa kuvuruga muache.
Eelewa kwamba wanaume hatupendi kelele na msichana wa kazi.
Yani ukitaka kulumbana nae hakikisha mumeo hasikii.
 
Na huenda Hawa wanaowatetea hawajawahi hata ajiri hao wadada wakajua tunachoongelea nimesoma comment Moja hapa inasema'huwa naamua tu kuwauzia wa mitumba kwa bei ndogo au kuziacha kabatini.Ni kweli kabisa Mimi sio mjinga nifungue Uzi tu eti nguo how??nimeongelea mtu kutothamini kitu unachopewa Cha thamani.Na Ukakichukulia kawaida tu.Ninyi mnaobisha hata thamani za kuwalipq na kuwarunza mahausigelo mnazisikia tu Radioni
Wangejua kero ya kuishi na mdada mchafu asiyejipenda anavyoaibisha wakija wageni!kwa Nini ashindie nguo ya kutokea?shenzy zake
 
Wanawake wa siku hizi ni pasua kichwa ndio maana wanaoshia kuachwa..hawasikilizi waume
Ndio kama hivyo tayari anataka kumpamda kichwa mume....ah hawa viumbe bila kiwa nao double double unakufa kwa presha
 
Back
Top Bottom