Lengai Ole Sabaya, asante kwa utumishi wako

Buyaka

JF-Expert Member
Jul 29, 2010
1,643
1,786
Utawala mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan leo umeangusha moja ya nguzo za katikati za urithi, legacy, ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutumbuliwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Kama ulipenda alichokisimamia John Magufuli pengine leo ni siku ya huzuni.

Nilimwona kwenye clip mapema mwaka huu saa sita za usiku akivamia kibanda cha mchaga kwa mbele, kwa nyuma ni ghala lenye shehena ya mzigo wa bia na mapipa ya dizeli na petroli zinazouzwa bila kulipiwa kodi, bila kutolewa risiti, bila taratibu za kuhifadhi shehena ya petroli ndani ya jengo wala bila ya usajili wa biashara zaidi ya leseni za kuuza vocha na mafuta ya taa.

Alikuwa amebeba tochi, amejikunyata kwenye kikoti cha baridi, ameambatana na afisa wa TRA, mwanahabari na askari polisi.

Sikuwahi kumwona au kusikia kiongozi wa nchi hii katika historia yake ya miaka 60 akifanya kazi nje ya ofisi kwenye giza tororo saba usiku, awe Afisa Mtendaji, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Waziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Nitamkumbuka kwa taswira ile.
 
Unafahamu vipi kuwa huyu halipi kodi, na mkwepa kodi anaadhibiwa vipi ikithibitika, anathibitishwa na nani kuwa ana hatia, hukumu inatolewa na nani na kwa utaratibu upi?
Ukifuata taratibu tulizojiwekea utapendwa na raia wema maana hutamwonea mtu.
 
Hahaha .. vichekesho kama hivi unavipata wapi?
Yaani mwanahabari pia alikuwepo kwenye ambush?Na bado unaona huyo ni mchapakazi?

Watu huwa mnarogwa vibaya sana
Kwa nini mwanahabari asiwepo kwenye ambush?

Mfanyabiashara akisema DC Ole Sabaya kanikamata kwa vipe alikuja kuomba rushwa nikamkatalia, atajitetea vipi bila ushahidi wa camera ??

Na akishambuliwa akiuliwa kwenye ambush ya serikali saa sita usiku kwenye go down la mtu, kwa nini kusiwe na recording cameras ????
 
Utawala mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan leo umeangusha moja ya nguzo za katikati za urithi, legacy, ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutumbuliwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Kama ulipenda alichokisimamia John Magufuli pengine leo ni siku ya huzuni.

Nilimwona kwenye clip mapema mwaka huu saa sita za usiku akivamia kibanda cha mchaga kwa mbele, kwa nyuma ni ghala lenye shehena za mzigo wa bia na mapipa ya petroli na dizeli zinazouzwa bila kulipiwa kodi wala usajili wa biashara, wala kutolewa risiti.

Alikuwa amebeba tochi, amejikunyata kwenye kikoti cha baridi, ameambatana na afisa wa TRA, mwanahabari na askari polisi.

Sikuwahi kumwona au kusikia kiongozi wa nchi hii katika historia yake ya miaka 60 akifanya kazi nje ya ofisi kwenye giza tororo, awe Afisa Mtendaji, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Waziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Nitamkumbuka kwa taswira ile.
Ujambazi tu ,kwani Kama tahalifa zipo why mvamie usiku, wakati maghala ya bia na mapipa ya petroli unayodai hayawezi hamishika kirahisi ,acheni utoto wa kuleta hoja mfu hapa, tuhuma zinazomkabili ni nyingi mno za ukiukwaji wa haki za binadam na kuuwa, tusubili uchunguzi,
Taifa linatengeneza vibaka waliojificha kwenye kivuli Cha uongozi alafu unakuja na hoja za ajabu,
 
Sawa hilo unaliona ni jema lakini Lengai Ole Sabaya ni kama Jambazi tu..
Huyo ameua..ametesa watu sana..
Kuna watu hapo Hai wana vilema vya huyu mbwa..
Utawala mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan leo umeangusha moja ya nguzo za katikati za urithi, legacy, ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutumbuliwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Kama ulipenda alichokisimamia John Magufuli pengine leo ni siku ya huzuni.

Nilimwona kwenye clip mapema mwaka huu saa sita za usiku akivamia kibanda cha mchaga kwa mbele, kwa nyuma ni ghala lenye shehena ya mzigo wa bia na mapipa ya dizeli na petroli zinazouzwa bila kulipiwa kodi, bila kutolewa risiti, bila taratibu za kuhifadhi shehena ya petroli ndani ya jengo wala bila ya usajili wa biashara zaidi ya leseni za kuuza vocha na mafuta ya taa.

Alikuwa amebeba tochi, amejikunyata kwenye kikoti cha baridi, ameambatana na afisa wa TRA, mwanahabari na askari polisi.

Sikuwahi kumwona au kusikia kiongozi wa nchi hii katika historia yake ya miaka 60 akifanya kazi nje ya ofisi kwenye giza tororo, awe Afisa Mtendaji, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Waziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Nitamkumbuka kwa taswira ile.

Ndio maana Meko alivyokufa alilia sana maana alijua ufedhuli wake hauna muda..
Mama asante kwa ZAWADI IDD.
 
Sifa ya kijinga kabisa hii, kwani angeenda mchana asingeona? Tatizo likishajulikana Luna haja gani ya kwenda usiku? Kuna haja gani ya kwenda na ma camera?
 
Kwa nini mwanahabari asiwepo kwenye ambush?

Mfanyabiashara akisema DC Ole Sabaya alikuja kuomba rushwa nikamkatalia, atajitetea vipi bila ushahidi wa camera ??

Na akishambuliwa akiuliwa kwenye ambush ya serikali saa sita usiku kwenye go down la mtu kwa nini kusiwe na recording cameras ????
Nchi ina taratibu zake, kama una habari za magendo kwanza kaombe search warrant halafu nenda muda wa kawaida tu. Haina haja ya kwenda usiku wakati mapipa ya mafuta si madawa ya kulevya kuwa unaweza kuuficha
 
Sawa hilo unaliona ni jema lakini Lengai Ole...
Ahsante

Angalau umeona hilo lilikuwa jema

Nikajiuliza, hivi kumbe hao wafanyabiashara wenyewe wanaosemwa wanaonewa ndio hawa wanaoficha shehena za mapipa ya dizeli ndani ya go down??

Yakilipuka majirani watapona?

Tunawatetea hawa watu ?
 
Utawala mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan leo umeangusha moja ya nguzo za katikati za urithi, legacy, ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutumbuliwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Kama ulipenda alichokisimamia John Magufuli pengine leo ni siku ya huzuni.

Nilimwona kwenye clip mapema mwaka huu saa sita za usiku akivamia kibanda cha mchaga kwa mbele, kwa nyuma ni ghala lenye shehena ya mzigo wa bia na mapipa ya dizeli na petroli zinazouzwa bila kulipiwa kodi, bila kutolewa risiti, bila taratibu za kuhifadhi shehena ya petroli ndani ya jengo wala bila ya usajili wa biashara zaidi ya leseni za kuuza vocha na mafuta ya taa.

Alikuwa amebeba tochi, amejikunyata kwenye kikoti cha baridi, ameambatana na afisa wa TRA, mwanahabari na askari polisi.

Sikuwahi kumwona au kusikia kiongozi wa nchi hii katika historia yake ya miaka 60 akifanya kazi nje ya ofisi kwenye giza tororo, awe Afisa Mtendaji, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Waziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Nitamkumbuka kwa taswira ile.
Nyoko wewe nadhani ni mkewe,
Hatuwezi kua na viongozi sampuli ya Ole, kichaa, mwendawazimu,mla rushwa, muuaji na mnyanyasaji.
Ulivyoviona ni kudai kodi tu, la kutaka rushwa hukuliona.
Mkuki kwa nguruwe... .....
 
Ole Sabaya alivamia usiku kwa sababu duka lilikuwa lina operate usiku.

Kama biashara ziko wazi usiku kwa nini serikali ilale usiku ?
hiyo biashara ilikua inaoparate usiku,so hata miliki wake alikua hajulikani , kwamba hakuna taratibu zingine za kumkamata mchana chini ya jeshi la polis na kwenda fanya ukaguzi kwake KWA kushirikiana na vyombo vingine ikiwemo TRA n.k achana kufanya Mambo Kama vile tz haijawai kuwa na taratibu au mifumo mnatia aibu
 
Hahaha .. vichekesho kama hivi unavipata wapi?
Yaani mwanahabari pia alikuwepo kwenye ambush?Na bado unaona huyo ni mchapakazi?

Watu huwa mnarogwa vibaya sana
Huyu hazimtoshi akaungane na mwendazake tu hakuna jinsi.
Ajinyonge au anywe sumu
 
Utawala mpya wa Rais Samia Suluhu Hassan leo umeangusha moja ya nguzo za katikati za urithi, legacy, ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kwa kutumbuliwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Kama ulipenda alichokisimamia John Magufuli pengine leo ni siku ya huzuni.

Nilimwona kwenye clip mapema mwaka huu saa sita za usiku akivamia kibanda cha mchaga kwa mbele, kwa nyuma ni ghala lenye shehena ya mzigo wa bia na mapipa ya dizeli na petroli zinazouzwa bila kulipiwa kodi, bila kutolewa risiti, bila taratibu za kuhifadhi shehena ya petroli ndani ya jengo wala bila ya usajili wa biashara zaidi ya leseni za kuuza vocha na mafuta ya taa.

Alikuwa amebeba tochi, amejikunyata kwenye kikoti cha baridi, ameambatana na afisa wa TRA, mwanahabari na askari polisi.

Sikuwahi kumwona au kusikia kiongozi wa nchi hii katika historia yake ya miaka 60 akifanya kazi nje ya ofisi kwenye giza tororo, awe Afisa Mtendaji, Diwani, Mbunge, Mkuu wa Wilaya, Mkuu wa Mkoa, Waziri, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au Rais.

Nitamkumbuka kwa taswira ile.
Mkuu,that was staged.
 
Back
Top Bottom