Lema: Tutapokea kigogo wa CCM

Lema: Tutapokea kigogo wa CCM

"Chadema kama kanisa, hatubagui mtu unaingia unatubu, unasamehewa tunaendelea kupigania wokovu wa nchi yetu" Hon. Msigwa. M4C for ever
kuna mtu kaandika humu kwamba mateka anaweza kutumika kushinda vita .
 
CCM kwaheri!Hautakuwa nasi kimwili na kiroho.
 
Lowasa ndani ya Ukawa...Nchi itatikisika ...Simba wa Yuda ataunguruma muda si mrefu

Simba wa yuda unamjua wewe au unajiropokea tu? Kama Lowasa atakuwa simba wa yuda Yesu Kristo atakuwa nani? msipoangalia mtaanguka na kumsudia muda si mwingi huyu Lowasa
 
Simba wa yuda unamjua wewe au unajiropokea tu? Kama Lowasa atakuwa simba wa yuda Yesu Kristo atakuwa nani? msipoangalia mtaanguka na kumsudia muda si mwingi huyu Lowasa

Mkuu naona unacheza ngoma husiyo ijua
 
Mbunge wa Arusha Mjini,Godblees Lema, amesema watapokea "kigogo mkubwa" kutoka CCM pamoja na wenyeviti wa mikoa na wilaya katika mkutano utakaofanyika Dar-es-salaam.

Chanzo:Mtanzania

CCM mwaka huu lazima mtafute mchawi wakati mchawi/wachawi mlicheza nao mziki pale ukumbini.

"Ni heshima kubwa kwa Mungu kumzomea fisadi mkubwa kama Lowasa" -Godbles Lema.
 
Ujio wa Lowassa upinzani utabadili kabisa upepo wa siasa za Tanzania, naweza kusema he is a "Game changer" na itachukua muda mrefu sana kusahau tukio hili.
 
Hakuna jipya hapo. Wajanja tulishajua kitambo. Anapita mule mule

Ukitaka uwaziri CCM uwe ni mtu asiye na adabu, mtovu wa nidhamu, mtusi n.k. Nchi itaendelezwa na miwaziri ya aina hii? Ni ukweli usiopingingika kuwa miwaziri na mikuu ya wilaya mitoto toto kadhaa imelazimishiwa uwaziri baada ya kuvurumisha mitusi bungeni kuanzia ile ya mikoa ya Dodoma, Singida n.k. wewe ndio unaona ni dili.
 
Nina uhakika hata kinachoongelwa hujui
Na ndio maana nikawapeni hongera kupata hayo makapi na chuya za kisiasa na kama bado huelewi basi ni pole tu.

Naendelea kusisitiza kuwa hayo ni maneno yako ni ya MKOSAJI
 
nimemueleza kuwa siri mzito anazo aache ushabiki siri za kiapo zipo na zisizo za kiapo zipo siri nyingi wewe unadhani mipango ya ufisadi wanakula kiapo cha kutunza siri vipo vingi ni vya siri kwa chama havihusishi serikali kila chama kinamikakati yake ya ushindi ya siri ni ya chama na siyo ya serikali unadhani aijui kiapo cha serikali ni kulinda vya serikali na ndio maana wana kuwa na ulinzi wanao ufahamu na wasio ufahamu kwa vyeo vyake ana siri nyingi za chama cha mapinduzi

Subiri siri. . . .
 
kuna hatari ya lowasa kutoa siri nzito ambazo wanachama wa ccm hawataamini.hii itasababisha anguko kuu ambalo alijapata kutokea tangia kuumbwa misingi ya ccm. pengine anajua mmiliki wa Richmond ni mkuu wa kaya yani patamu hapo! CCM IMETUDHULUMU VYA KUTOSHA na sasa dhuluma iwarudie tu maana kuna akina mama walipoteza maisha kwa kukosa dawa kwa sababu ya Richmond ,watoto pia.Hakika CCM HAMTABAKI SALAMA KAMWE.
 
Ccm bye bye

Siasa za chadema ni za kitapeli na ulaghai! Leo hii fisadi papa kawahonga viongozi wa chadema bil 10 na ghafla fisadi mmembadili jina na kumuita Simba wa Yuda!!! lahaulaa! ama kweli fedha fedheha. Slaa atabaki kumrembulia macho tu Lowasa na kuanzia sasa siwaamini chadema kwa ishu yoyote matapeli wakubwa. Watu walijeruhiwa maandamanoni, wengine wamepoteza viungo kuijenga chadema eti wakiamini ndio mkombozi wao katika kupambana na ufisadi kumbe ilikuwa ni gia ya kusaka ulaji mnono toka kwa hao hao mafisadi! mmewakatisha tamaa watanzania wenye uchungu na nchi yao. Natangaza rasmi kuwa CHADEMA ni chama cha mafisadi.
 
Wapinzani hawana goli la mkono kama CCM,goli la mkono la wapinzani litakuwa ni Lowassa awe ndani ya CCM humohumo au nje ya CCM kinachotakiwa ni ushindi.
 
Back
Top Bottom