Lema amvaa Mkapa, yeye (Mkapa) ajitetea...

Kusema wabakaji, wezi nk. Watoke gerezan,!!!? unatarajia nini kwa hawa waliotendwa. Ndo mwanzo wa kuuana coz huwezijua jamii itampokeaje na yeye atakuja na mtazamo gani.

Tusiwe bendera tufate upepo, eti kisa hoja imetolewa na mtu wa chama unachokipenda.
 
lema akili hana,tuwe wastarabu,alijenga daraja lililoshindikana toka uhuru(daraja la mkapa),kawajengea barabara,kawajengea daraja la tanzania na msumbiji,kwa hyo lema alitaka mkapa awajengee nyumba za kuishi?huku kuropoka kutawaponza
 
We ndiyo akili huna,,,,, EPA jibu hoja ya msingi iliyoibuliwa usilete unazi wa wako wa ccm ,,, yawezekana unalipwa na hela zetu za rada .... nyie ankaut zenu ziko uswis ...... hamtazikwa nazo oneni hurma shule za kata ,huduma mbovu za afya .....
 
Kazi kweli kweli angeendeleza mkoa kwa kasi wangesema anapendelea kwao yaani Mkapa mbinafsi. Maana tumeshaanza JK kasema bagamoyo kujengwe bandari na kiwanja cha ndege tayari tunasema hili mara lile. Jamani, ukiwa rais wa TZ unatakiwa kuangalia masuala ya nchi. Nakumbuka wazee wa mkoa walimuita Mkapa wakamuuliza mzee mbona unatutupa huku umaskini umekithiri sana.... Mkapa aliwajibu kuwa yeye sio rais wa kusini bali wa Tanzania. Akasema, serikali inawajengea barabara ambayo miaka yote imekuwa tatizo na zinajengwa barabara na miundombinu kuunganisha mkoa na mikoa mingine kama ruvuma, pia kusini na msumbiji kuna daraja litajengwa pamoja na utafutaji wa rasilimali gas kwa ajili ya umeme hivyo hivi vitakuwa chachu ya maendeleo kwa kanda hii. Zaidi ya hapo nifanyaje? Hata bodi ya korosho kipindi kile iliimarishwa. Akasema shirikianeni na wabunge wenu pamoja na mawaziri wangu wanaotoka huku kulisukuma gurudumu la maendeleo na wananchi waamke na kujituma kikubwa waende shule. Lema kwa hiyo kauli sikusapoti na usirudie tena maana ni ubaguzi kwa watazania wengine, ina maana rais akitoka AR akazane huko umaskini uishe? akifanya hivyo atabalance vipi na mikoa mingine?.

Nteko Vano,

..lakini Mkapa alikuwa mbunge huko kusini kwa miaka mingi sana. nini ilikuwa rekodi yake kama mbunge??

..pia lets look at the big picture: hivi kweli ni halali kwa mikoa ya kusini kusubiri miaka 40++ toka uhuru kujengewa hiyo barabara na daraja??

..tatizo siyo kwamba CCM hawafanyi kitu, wanafanya lakini ni kwa kasi ya konokono. hawana ubunifu and they think they have all the time in the world.

..mikoa ya kusini hali inasikitisha. anazaliwa mtu kwenye nyumba ya makuti, mpaka anapata vitukuu navyo vinaishi kwenye nyumba ya makuti, and yet tunasema tuna serikali ya wananchi na wasomi kutoka eneo hilo.

..Mkapa kuwa Raisi wa Tanzania nzima haimaanishi na wala haihalalishi mikoa ya kusini kukosa barabara na huduma nyingine muhimu, au zao la korosho kutelekezwa na wananchi kugubikwa na umasikini.
 
Hivi ni mafanikio yapi ambayo Watanzania waliyoyaona wakati wa awamu ya Mkapa?

Ikumbukwe aliingia madarakani kwa mbwembe za kujiita Mr Clean kisha akaunda Tume ya Warioba kuchunguza tatizo la rushwa nchini na kuja na mapendekezo ya jinsi ya kupambana nayo. Baada ya kukabidhiwa ripoti ile haikufanyia kazi na kuaicha ipigwe na vumbi pale Ikulu huku yeye na Serikali yake wakiendeleza ufisadi.

  • Aliwaingiza makaburu wa Net Group Solutions wauza stationeries toka RSA kwa mtutu wa bunduki pale TANESCO ambao hawakujua chochote kuhusiana na umeme na kuwapa management positions na kuwalipa mabilioni ya pesa za walalahoi.
  • Aliuza mashirika yetu mbali mbali ikiwemo NBC kwa bei ya kutupa kwa kile kilichoitwa ubinafsishaji na hadi leo hii hakuna matunda yoyote ya tunayoyaona ya sera ile ya Mkapa
  • Kashfa za EPA, Kagoda na Meremeta zote zilitokea wakati Mkapa akiwa madarakani
  • Alihusika katika ununuzi wa rada ambayo baadaya ilikuja kufahamika kwamba ilikuwa imenunuliwa kwa ufisadi wa hali juu....kumbukeni kauli ya Mramba, "hata majani tutakula lakini rada ni lazima inunuliwe."
  • Alihusika katika kumpa zabuni shemeji yake katika uuzwaji wa mali mbali za posta na simu zikiwemo nyumba
  • Alihusika katika ukwapuaji wa nyumba za Serikali ambao umeingiza Serikali katika hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 300 and counting
  • Alihusika katika kununua ndege bomu ya Rais huku akiwa amebakisha miezi mitatu kumaliza awamu yake.
  • Ununuzi wa helicopters na magari ya jeshi ambao ulijaa ufisadi wa hali ya juu ulifanyika katika awamu yake.
  • Hakukuwepo na ongezeko la ajira kwa Watanzania na hii ilisababisha Watanzania waiite awamu yake awamu ya Ukapa
  • Hakukuwa na ahueni yoyote katika upatikanai wa maji, umeme, matibabu au elimu. Upatikanaji wa maji ulikuwa bado ni wa shida katika mikoa minngi nchini na hali kadhalika umeme. Hospitali zetu nyingi zilikuwa hazina dawa, vifaa muhimu na vitanda vya kulalia wagonjwa vilikuwa adimu na hivyo wagonjwa wengi kulala chini au wagonjwa hadi saba kulalia kitanda kimoja au godoro moja.
  • Mishahara ya Wafanyakazi wengi nchini bado ilikuwa ni duni sana na haikuendana na gharama halisi za maisha
  • Wanafunzi wengi bado walikuwa wanahudhuria shule ambazo hazikuwa na hadhi ya kuitwa shule na wengi walikaa chini na hawakuwa na walimu wa kutosha
  • Pia Mkapa alihusika katika ukwapuaki wa Kiwira Coal Mining na pia kufanya biashara akiwa Ikulu.

Tunaona Mkapa anavyojarbu kutaka kujipandisha chart kwamba awamu yake ilikuwa na mafanikio. Je, kama kulikuwa na mafanikio katika awamu ya Mkapa ni mafanikio yepi yaliyopatikana wakati wa awamu ya Mkapa ambayo Watanzania hawakuyaona hadi kutamka, "Mkapa kaleta ukapa?"

Watanzania mjifunze kuwa na shukurani. Hivi ukisema mkapa hakufanya kitu na Kikwete utasemaje? Personal interest huwa hazioni mazuri ni mabaya tu.
 
Ni kweli kila mtanzania anayo haki ya kuishi popote pale nchini, lakini hii ya Mkaahapa kuikacha Mtwara na kwenda kuishi Tanga ni ajabu inayoandamana na aibu!

Yeye kama kioo cha Taifa hakutakiwa kufanya maduguri hayo, kwanini asimwige Nyerere?
...hii inaonyesha dharau aliyo nayo juu ya mahala anakotoka.

Lema ana substance kubwa sana kwenye vidonge anavyompa Mkapa!

Si wanasema yuko juu ya mawe ya DHAHABU... inasemekana kile kilima na eneo lake lote chini kuna madini ya Dhahabu sasa sijui anakuwa anachimba kimya kimya Usiku....

Watu wa Tanga mtoeni baru huko..
 
Amekimbia kula chamaki nchanga "panya" ntwara na supu ya ngozi ya ng'ombe.....kawaachia chinga bendera za ccm!

yeye anaenjoy upepo mwanana wa milima ya usambaa..ikulu ya lushoto......! duh! BM kichwa..!

Btw, kwakweli LEMA anahitaji BIG UP kwa Saaaaaaanaaaaaaa.!
 
Kusema wabakaji, wezi nk. Watoke gerezan,!!!? unatarajia nini kwa hawa waliotendwa. Ndo mwanzo wa kuuana coz huwezijua jamii itampokeaje na yeye atakuja na mtazamo gani.

Tusiwe bendera tufate upepo, eti kisa hoja imetolewa na mtu wa chama unachokipenda.
kuwa na akili kwani hao mawaziri waliotuibia mabilioni na kuachwa unategemea nini kwa sisi wananchi tulioibiwa. jamaa anapinga double standards tusiwe na akili finyu unapinga kisa kasema mtu wa chama fulani.
 
Watanzania mjifunze kuwa na shukurani. Hivi ukisema mkapa hakufanya kitu na Kikwete utasemaje? Personal interest huwa hazioni mazuri ni mabaya tu.
Basi tufanye alifanya mengi sana, vipi kuhusu kumrithisha mtu kama Jakaya uenyekiti wa Chama na Urais, hauoni kama ni ushahidi kwamba Mkapa hakuwahi kuwa na vision ya uongozi na kama alikuwa nayo ilikuwa very short sighted, sababu kama kuna kitu chochote alifanya na sasa ghafla wananchi hawakioni basi inawezekana kimeharibiwa katika awamu hii, awamu hii haijaisha, kwa hiyo kama imefanikiwa kuharibu kitu chochote kizuri kilichopandikizwa wakati wa mkapa ina maana kwamba kitu hicho hakikuwa imara na hakikidhi sifa ya kuitwa msingi.

Hata wewe ukiwarithisha watoto wako kitu ambacho watakiharibu ndani ya muda mfupi sana ni sawa sawa na kwamba haukuwarithisha bali ulikufa unprepared, you dead wanting to continue enjoying it.
 
Kazi kweli kweli angeendeleza mkoa kwa kasi wangesema anapendelea kwao yaani Mkapa mbinafsi. Maana tumeshaanza JK kasema bagamoyo kujengwe bandari na kiwanja cha ndege tayari tunasema hili mara lile. Jamani, ukiwa rais wa TZ unatakiwa kuangalia masuala ya nchi. Nakumbuka wazee wa mkoa walimuita Mkapa wakamuuliza mzee mbona unatutupa huku umaskini umekithiri sana.... Mkapa aliwajibu kuwa yeye sio rais wa kusini bali wa Tanzania. Akasema, serikali inawajengea barabara ambayo miaka yote imekuwa tatizo na zinajengwa barabara na miundombinu kuunganisha mkoa na mikoa mingine kama ruvuma, pia kusini na msumbiji kuna daraja litajengwa pamoja na utafutaji wa rasilimali gas kwa ajili ya umeme hivyo hivi vitakuwa chachu ya maendeleo kwa kanda hii. Zaidi ya hapo nifanyaje? Hata bodi ya korosho kipindi kile iliimarishwa. Akasema shirikianeni na wabunge wenu pamoja na mawaziri wangu wanaotoka huku kulisukuma gurudumu la maendeleo na wananchi waamke na kujituma kikubwa waende shule. Lema kwa hiyo kauli sikusapoti na usirudie tena maana ni ubaguzi kwa watazania wengine, ina maana rais akitoka AR akazane huko umaskini uishe? akifanya hivyo atabalance vipi na mikoa mingine?.

Hauko sahihi hata kidogo, unachokifanya ni kujificha kwenye dhana ya Utaifa, Kama Rais wa nchi Mkapa alitakiwa angalau aache amejenga uwezo wa watu wa kwao kujiinua kiuchumi, kama aliweza kwenda nje ya nchi kuhamasisha globalization issues na kuwaelekeza wageni kuja kuwekeza nchini ni nini kilimfanya ashindwe kwenda kuwaelekeza watu wa kwao kuacha uzembe kama alivyokuwa akitukebehi kila mwisho wa mwezi kwenye TV, Kwa nini kashindwa kuwa role model wao na wao tuwaone wakishiriki kwenye active politics angalau?
 
Nteko Vano,

..lakini Mkapa alikuwa mbunge huko kusini kwa miaka mingi sana. nini ilikuwa rekodi yake kama mbunge??

..pia lets look at the big picture: hivi kweli ni halali kwa mikoa ya kusini kusubiri miaka 40++ toka uhuru kujengewa hiyo barabara na daraja??

..tatizo siyo kwamba CCM hawafanyi kitu, wanafanya lakini ni kwa kasi ya konokono. hawana ubunifu and they think they have all the time in the world.

..mikoa ya kusini hali inasikitisha. anazaliwa mtu kwenye nyumba ya makuti, mpaka anapata vitukuu navyo vinaishi kwenye nyumba ya makuti, and yet tunasema tuna serikali ya wananchi na wasomi kutoka eneo hilo.

..Mkapa kuwa Raisi wa Tanzania nzima haimaanishi na wala haihalalishi mikoa ya kusini kukosa barabara na huduma nyingine muhimu, au zao la korosho kutelekezwa na wananchi kugubikwa na umasikini.

Jokakuu, "UBUNIFU" Mkuu 90% ya waajiriwa hasa wa Serekalini + Mawaziri na Makatibu wakuu wao hilo neno hawalijui wala hawajalisikia. Jamaa wanafanya kazi zao wakiwa ndani ya BOX hawaoni nje wala wajui kinachoendelea Duniani. Aliekalia kiti na meza anaona juu ya meza yake tu, hana tahadhari ya Nyuma, hageuki Kushoto wala Kulia na Mbele haoni! kwa lugha nyingine ni Mazezeta. Inasikitisha mno!
 
lema akili hana,tuwe wastarabu,alijenga daraja lililoshindikana toka uhuru(daraja la mkapa),kawajengea barabara,kawajengea daraja la tanzania na msumbiji,kwa hyo lema alitaka mkapa awajengee nyumba za kuishi?huku kuropoka kutawaponza
hembu kaulize limeanza lini hilo daraja?Alikuja malizia tuu longolongo za CCM kuhusu hilo daraka kwa miaka kibao.ALitaka angalau kuwakopa korosho kuishe, +++
 
Mkapa mapungufu anayo na mazuri pia yapo, lakini tusimtetee ila utawala wa sasa urekebishe mapungufu hayo japo tunachoshudia ni yanaongezeka na ndiyo maana watanzania tunalalamika na mwisho wa siku tutawahukumu.
 
Watanzania mjifunze kuwa na shukurani. Hivi ukisema mkapa hakufanya kitu na Kikwete utasemaje? Personal interest huwa hazioni mazuri ni mabaya tu.

Dada Caroline Danzi kama kuna shukrani ambayo Mkapa anastahili toka kwa Watanzania kwa yale ambayo aliyoyatenda akiwa madarakani basi si vibaya ukayaweka mambo aliyoyatenda akiwa madarakani yaliyostahili kutolewa shukrani. Mimi nadhani na Watanzania wengi watakubaliana nami kwamba hastahili shukrani yoyote kwa kuwa alitumia awamu yake katika kutumia wadhifa wake kujitajirisha yeye, familia yake na marafiki zake wa karibu. Nimeyaweka hapo juu baadhi ya mabaya ambayo Mkapa aliyafanya akiwa madarakani, kama unayakumbuka mazuri basi yamwage hapa tuyajadili ni kiasi gani yaliinufaisha/yaliwanufaisha Tanzania na Watanzania.

Aliweza kuongeza makusanyo ya kodi kwa kiwango kikubwa sana lakini pesa yote badala ya kuitumia kuboresha maisha ya Watanzania aliitumia katika kulipa madeni yetu ya nje na hata kusifiwa sana na nchi za wafadhili pamoja IMF na WB lakini Watanzania waliendelea kuona UKAPA ukizidi kuongezeka zaidi.

Mwaka 2003 kama sikosei baada ya kelele nyingi za Watanzania kuhusu kutoridhishwa na mikataba ya uchimbaji wa dhahabu nchini ambayo ilisemekana haina maslahi kwa Watanzani, Wabunge ikiwemo wale wa CCM walichachamaa na kutaka mikataba ile ipelekwe bungeni wakaione na hatiamye kuijadili. Mkapa kuona Wabunge wamechachamaa akasafiri kwenda Dodoma na kukutana na Wabunge wote wa CCM katika kikao cha siri. Hadi hii leo haijulikani aliwaambia nini lakini baada ya kikao kile Wabunge wote wa CCM wakapoa kabisa na hawakuendelea tena na madai yao ya kutaka kuiona na hatimaye kuijadili mikataba ya uchimbaji wa dhahabu. Mkapa tena akawa amefanikiwa kuendelea kuyaficha madudu yake na hadi hii leo bado anaficha dhambi zake chungu nzima alizozifanya akiwa madarakani.


 
Last edited by a moderator:
Kusema wabakaji, wezi nk. Watoke gerezan,!!!? unatarajia nini kwa hawa waliotendwa. Ndo mwanzo wa kuuana coz huwezijua jamii itampokeaje na yeye atakuja na mtazamo gani.

Tusiwe bendera tufate upepo, eti kisa hoja imetolewa na mtu wa chama unachokipenda.

Inabidi uwe very smart kichwani kuelewa falsafa ya G. Lema, kwa vilaza na wavivu wa kufikiri ni ngumu sana kumuelewa.
 
Inabidi uwe very smart kichwani kuelewa falsafa ya G. Lema, kwa vilaza na wavivu wa kufikiri ni ngumu sana kumuelewa.


tabu watu wengine wakurupukaji, hivi kama jambazi kaiba milioni kumi na waziri kaiba bilioni 1 nani anaetakiwa kwenda magereza? Kwa hio inamaana ukiwa kiongozi unaruhusiwa kuiba bilioni 50 halafu unarudisha bilioni 10 ili kuzima kashfa yako, kwa aliyeiba kuku ukichunguza ni sababu ya hali ngumu ya maisha je waziri ambaye anapokea mshahara mkubwa,bado analipiwa mafuta,chakula,matibabu,posho za vikao atajitetea ana maisha magumu?

Think indeep
 
natamani kweli hawa jamaa (mkapa na kichwa cha nazi a.k.a Janga la Kitaifa) siku moja wapandishwe pale kwa Ocampo the hague, wapigwe mvua 50 kama za Charles Teila, i hate them.. jamaa wako after their own interests, yani wako tayari kutoa uhai wa mtu kwa manufaa yao, huyo mkopa mwenyewe anahusika na mauaji ya wachimbaji wadogo wadogo kule bulyanhulu miaka ya 2000 -01, huyu jk mwenyewe mauaji ya kinyama kwenye kampeni zake, kwa hiyo bana, hawa jamaa sioni sababu ya kutokuwapeleka THE HAGUE Kwa mzee Ocampo
 
Back
Top Bottom