Mkuu nakuunga mkono kabisa sample yangu kuna mjuu wake binti mdogo tu anaitwa Sitti Mwinyi naweza kukapa nidhamu A.
Heshima kwa wakubwa iko vizuri sana hakuna nyodo kabisa, heshima to the family kwa kweli.
Mubashara lina maana ya papo kwa papo...kwa kiingereza wanaita "live".Hivi hili neno "mubashara" lina maana gani?
Ahsante sana mkuu
pale alipoita timu ya taifa kichwa cha mwenda wazimu,, mpka sasa timu yetu imeshindwa kufurukuta.. nimuombe tu atengue hyo kauli tupate kufanya vizuri kama zamani
IMF ndio waliozuia watanzania wasiende ulaya kuatafuta bidhaa ? WB ndio waliowalazimisha watu wasiwe na tv awe nayo mtu mmoka nchi nzima ? Hata sabuni zakuogea zilikiwa shida watu walifulia majani ya mpapai hili nalo nililkuwa ni katazo la IMF watanzania wafulie mipapai ?Alkua anaambiwa na WB na IMF Nate anatimiza so hapakuwa na ujuzi wala ubunifu kupigia mfano!! Ruhusu demokrasia- sawa! ruhusu soko huria-sawa! nk. nk. Kuhusu legacy may be that but for me there was nothing best in particular!
Nakumbuka Mchungaji Mtikila alilia kuuzwa kwa Tausi wa ikulu na kuuzwa kwa Loliondo kwa mwana wa mfalme...Si bora ukae kwenye foleni, baadae upate hiyo ration yako/yenu. Unaweza kaa, foleni ndio imetoa wanne, mnaambiwa "unga wa ngano umeisha". Dah, chapati ilikuwa anasa!
...Acha sukari au mchele. Unakumbuka sabuni nayo ilikuwa shida?
Mungu ndiyo anajua siku zetu za kuishi, kwanini hujasema mniambie mazuri ya Mwingi kabla sijafa?
Hiyo Punguani ulivyoiandika ni dhahiri shahiri umekurupuka Mkuu. Andika tena wanajamvi tukuelewe.Ndo umeandika nini hapa we pungua.ni?
Hii namba nne umekurupuka , hili sakati lilitokea mwaka 1998, je mwinyi alikuwapo? aliyeamrisha alikuwa sumaye je mwinyi alikuwapo, acha chuki zisizo na mpango,1. ALIFUATA TORATI YA MUSA NA KUWANYONGA WOTE WALIOHUKUMIWA KIFO NA MAHAKAMA KWA MUJIBU WA SHERIA ZA TANZANIA BILA MZAHA WALA UPENDELEO AKIWEMO KANALI MMOJA TOKA TABORA NAMPENDA SANA KWA HILO
2. ALIWABEBA SANA WAFANYABIASHARA KIASI KWAMBA AJIRA IKAONEKANA NI UPUUZI NA WENGI WALIACHA KAZI SERIKALINI KWAKUWA MISHAHARA ILIKUWA HAIPATIKANI MPAKA WAFANYABIASHARA WAPELEKE FEDHA BANK NDIPO MFANYAKAZI APATE MSHAHARA NI KATIKA KIPINDI CHAKE ALINISABABISHIA NIACHA KUSOMA BAADA YA KUONA KUAJIRIWA HAKULIPI KAMA KUFANYA BIASHARA
3. ALIMDEKEZA SANA WAZIRI WA FEDHA MAREHEMU PROF. KIGHOMA ALI MALIMA AKAJENGA MSIKITI WIZARA YA FEDHA.
4. NI KATIKA KIPINDI WAISLAM WALITAKA TANZANIA IONGOZWE KIDINI NA MKAKATI HUO ULIONGOZWA NA MAREHEMU SHEIKH YAHYA HUSSEIN KWA KUANZISHA BALKUTA NA KUANZA KUVUNJA MABUCHA YA NGURUWE NA NI KIPINDI HICHO NYAMA YA NGURUWE ILIITWA KWA UTANI "YAHYA" AU MBUZI KATOLIKI
5. NI KATIKA UTAWALA WA MWINYI SERIKALI ILIKUWA HAIKUSANYI KODI NA WAFANYABIASHARA WALIKUWA NA NGUVU YA KUFANYA LOLOTE NA IKULU PALIKUWA PANAINGILIKA KIRAHISI SANA HATA UKIWA NA SHIDA YA ADA YA SHULE ULIRUHUSIWA KUMUONA RAIS NA UKIHITAJI KUCHEZA BAO NA PRESIDAA UNAOMBA NA UNAINGIA KAMA ALIVYOFANYA MWENYEKITI WA YANGA NA MBUNGE WA KILOMBERO MAREHEMU ABBAS GULAMALI. NAISHIA HAPO.
Alkua anaambiwa na WB na IMF Nate anatimiza so hapakuwa na ujuzi wala ubunifu kupigia mfano!! Ruhusu demokrasia- sawa! ruhusu soko huria-sawa! nk. nk. Kuhusu legacy may be that but for me there was nothing best in particular!
Hatuongelei legacy ya Nyerere, weka uzi wa Nyerere uone kama hawatamchana!Uzi huu wale wasiompenda mwinyi kwa ajili ya dini yake wana mengi ya kusema huku wakifumbia macho maovu ya nyerere na kumimina sifa nyingi na utakatifu juu, wakati ukweli upo wazi, Nyerere alitufanya tutembelee viatu vya matairi ya gari, tule dona la njano tena upatikanaji wake mbinde, watu walikuwa wakivaa kaniki kama waganga wakienyeji vile.
Hakuna aliyethubutu kusema lolote alikuwa dikteta anayepewa sifa ya utakatifu.
Mkuu unadai mzee mwinyi kaporomosha uchumi kutoka wapi???
Unajua mzee mwinyi kakuta nchi ina hali gani mwaka 1985???
Usikariri mkuu.
Hata hiyo unayosema yye kwenda arabuni unajua nchi hii mwallim nyerere aliiachaje???
Rejea hotuba ya mzee mwinyi na wazee wa dar dimond jubilee akielezea nchi ameikutaje.hakukuwa na mafuta hata ya kuendesha uchumi kwa week mbili.so kazi yake ya kwanza ni kuzunguka duniani ikiwemo irani kwenda kuomba mafuta.
Hali ilikuwa mbaya sana kila mahali.
Mkuu nakushauri usome historia hasa hali ilivyokuwa wakat mzee mwinyi anapewa nchi na neema ya ruksa ilivowafaa watu.
Wengine wataongezea
Kila unachokiandika huwa nashawishika kukisomaNnazitafuta sana hizo hotuba za Mwinyi na wazee wa Dar, hususan zile mbili za mwanzo.
Ukizipata nijulishe.