Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Hii ni barua ya Mh. Mwinyi wakati anajiuzulu uwaziri mwaka 1977
Viongozi wetu wanajifunza nini kupitia mzee Mwinyi?
Screenshot_20190723-095449.jpeg
 
Kisiasa, Uongozi wa Mwinyi ulifanikiwa katika mambo makuu mawili; kufunguliwa kwa milango ya demokrasia na Uhuru wa Vyombo vya Habari. Dhana ya demokrasia, japo haikutumika katika chaguzi za kipindi chake, lakini angalau miaka miwili kabla ya kuondoka madarakani nchi ilifungua mlango wa demokrasia ambapo siasa za vyama vingi zilianza wakati yeye akiwa madarakani.Kwa pamoja na Uhuru wa Vyombo vya habari, nchi ikajenga mazingira mapya kutoka yale ya utawala usiokosolewa kuja utawala uliokosolewa hadharani. Kwa mara ya kwanza ikashuhudiwa demokrasia ya Rais kuchorwa na kusemwa vibaya.

Vijana wa Chuo Kukuu cha Dar es Salaam wao walifikia hatua mbaya zaidi pale walipoifuja demokrasia hiyo kwa kuchora picha za matusi dhidi ya Rais Ali Hassan. Kama tutakavyoona katika kipengele cha elimu, Mwinyi alileta nafuu kubwa ya maisha ya Wanataaluma Chuoni hapo.

Japo wanataaluma walianza kuonesha mfano mbaya wa matumizi ya uhuru wa kujieleza ambao haukuwepo enzi za Nyerere lakini bado Mwinyi hakufunga mlango wa demokrasia.

Kwa mara kwanza tangu miaka ya 1960, Watanzania wakaanza kushuhudia majukwaa ya upinzani dhidi ya Chama tawala na serikali. Ukizungumzia mwanzo wa mageuzi ya kisiasa basi lazima utayakuta ndani ya kipindi cha Mwinyi.

Kama kuna eneo lililoung’arisha mapema utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi basi lilikuwa ni lile la Uchumi. Mwinyi aliaswa na wataalamu wa uchumi kuwa aachane kabisa na fikra zilizoshindwa na Mwalimu Nyerere kama alitaka kufanikiwa katika eneo hili.
Good!
 
Mwinyi na Magufuli wote wamekua marais kwa bahati.

Mwinyi walikubaliana na nyerere kwamba mwinyi kwemye kikao akatae ili nyerere aendelee.. kumbe mwingi baada ya kumwambie mkewe.. akaambiwa kama atakataa asirudi nyumbani..

Mwimyi baada ya kuulizwa akajibu nipo tayari na nashukuru kwa fursa na ndio mwanzo wa nyerere kusema mtu unashauriwa mkeo kitandani .

Wote hawakuwa na mpango nini watalifanyia taifa hili.
 
Foleni zilikuwa za kusukumana kwani watu walikuwa wengi kuliko bidhaa. Ndiyo kusema, wengine walirudi nyumbani mikono mitupu baada ya jitihada za kusukumana ili kulifikia dirisha la duka kushindikana. Wengine walizirai kwenye foleni! Ugumu hasa ulikuwa katika kupata sukari au mchele uliokuja kwa nadra.

Teh teh teh

Hiyo Crisis ilisababishwa na Vita ya Kagera 1978/79 (katika kuweka kumbukumbu sawa though nilikuwa mdogo lakini nakumbuka unga wa Dona ulivyokuwa "dili":oops::oops::oops:)
 
Mimi kama mfanyakazi nitakuwa wa mwisho kumpongeza Rais Mwinyi maana katika utawala wake ndo kipindi wafanyakazi walidharauliwa hata na wauza machungwa barabarani, kilikuwa kipindi kigumu sana kwa kundi la wafanyakazi wa umma. Bila Rais Mkapa kubadilisha mambo sijui nchi hii kama ingekuwepo hadi leo. Maana ni kipimdi ambacho serikali ilikuwa dhaifu sana haikuweza kabisa kukusanya kodi nakumbuka hadi Nyerere alisema serikali dhaifu huwa zinaacha kukusanya kodi kwa wafanya biashara na kufukuzana na machinga barabarani. Sasa Kiongozi aliyeomgoza serikali dhaifu kiasi kile labda akumbukwe kwa hiyo sifa ya kuwa na serikali dhaifu sana.
 
Kuna dhahabu ilikamatwa airport ikimuhusu huyu mzee!! Mrema anakumbuka vizuri!
Legacy ya wizi ndiyo aliiacha pamoja na matangazo ya kondomu. (kelbu)
 
View attachment 448507
Rais mtaafu Mzee ALI HASSAN MWINYI ambaye nadhani ki historia ni mmoja ya watu wachache sana duniani ambao waliwahi kuwa rais wa nchi mbili tofauti. Al Hajj Mwinyi aliwahi kuwa Rais wa Zanzibar na Tanzania pia leo ametimiza miaka 91 toka azaliwe.

Je GREAT THINKERS wa JAMIIFORUMS mnaweza kutupatia dondoo za legacy yake na cha kujiuliza je mnadhani hawa watawala tulionao wangejifunza nini toka kwa Mzee Ali Hassan Mwinyi?
Legacy yake ni vile vibao alicharazwa msikitini! Yule jamaa angempiga ngumi kabisa!
 
Mungu akupe maisha marefu na afya tele mzee wetu mzee ruksa iliikuta nchi iliyokuwa hohe hae inchi imejichokea na sera za ujamaa kila kitu foleni na hata ukiunga foleni huna hakika ya kupata bidhaa lakini ukaja ukaufungua mlango wa ruksa hakika ruksa ikaifaa sana nchi yetu.
Kipindi kile nchi ilihitaji kiongozi mwenye haiba yako ukaamua kwenda kinyume na asili ya ujamaa ili inchi ipone hakika baadhi ya mazuri ambayo tunayashuhudia hadi leo yalitokana na jasho lako.
Uliyafanya haya kwa ujasiri japo haiba yako yaonekana ya upole ila ulifanikiwa kuivusha nchi katika kipindi kigumu kweli kweli.

Nakumbuka ukituaga kwenye hutuba yako ukatuambia "MABAYA YANGU NIACHIENI LAKINI MAZURI YANGU TUGAWANE". Hakika ni kweli leo mazuri yako tunagawan.

Hongera sana mzee ruksa mola aendelee kukupa afya njema na miaka mingi zaidi.
Shairi zuri zana hili ukioimbaa
 
1563876148243.png
uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi mwaka 83 kama sijakosea nafasi yake aliteuliwa mzee mmoja kutoka zanzibar anaitwa mzee natepe kushika uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi.

Natepe alipoingia tu officen alimtaka waziri aliemtangulia kutoka katika nyumba ya waziri ili yeye aweze kukaa hapo kama waziri.

Ilikuwa shida kidogo maana waziri alieondoka bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka kutoka na Natepe.

Ikampasa mzee mwinyi kutoka kwa haraka na siku anatoka pale nyumbani alikuwa amenunua mabati 150 na mifuko ya saruji 100 ya kwake wala sio mali ya serekali.

Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya serekali kweli mzee mwinyi akaviacha akaondoka.

Baada ya miezi kadhaa tu mzee mwinyi akateuliwa kuwa Rais zanzibar Natepe wakati ana jifikiria jinsi ya kwenda kumpongeza na kumuomba radhi kwa aliyomfanyia kabla ya kufikiria njia mzee mwinyi akaletwa bara mwaka 1985 kama Rais wa JMT.

Hapa sasa Natepe akajua kazi hana na atatimuliwa haraka iwezekanavyo tena na kutengwa na nyadhifa za JMT kwakuwa kuna mabaya ya wazi na ya sirini aliyomtendea mzee mwinyi.

Mzee mwinyi baada tu ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT wakati anateua baraza la mawaziri akamteua tena Natepe kuwa waziri pale pale mambo ya ndani.

Siku ya kumuapisha akamwambia Natepe sio kwamba nakupenda sana hapana ila napenda kazi yako unavyofanya endelea kufanya kazi.

Siku moja mzee mwinyi yupo ikulu kapumzika akaona malori yanaingia na akaambiwa mzigo wako huu mh Rais akashtuka mbona sijaagiza kitu mie??

Ndipo akaambiwa umetoka kwa natepe mzee mwinyi akacheka sana akawaambia wasaidizi wake shusheni mabati 150 na saruji 100 hizo ndio haki yangu zingine mrudishieni tu.

Hapa kuna masomo makubwa ma tatu vema viongozi wetu wa sasa wakajipambanua kwayo ili tuende kwa weledi na umakini sana.
 
Hongera kwa jua yaliyomo vyumban kwa watu
Mwinyi na Magufuli wote wamekua marais kwa bahati.

Mwinyi walikubaliana na nyerere kwamba mwinyi kwemye kikao akatae ili nyerere aendelee.. kumbe mwingi baada ya kumwambie mkewe.. akaambiwa kama atakataa asirudi nyumbani..

Mwimyi baada ya kuulizwa akajibu nipo tayari na nashukuru kwa fursa na ndio mwanzo wa nyerere kusema mtu unashauriwa mkeo kitandani .

Wote hawakuwa na mpango nini watalifanyia taifa hili.
 
Surely u weren't on 80's pale mafundi cherehani walipata kipato kwa kuria viraka nguo kwenye viraka.
Mtu ynatumia 4hrs kupanga foleni ili upate pakti moja ya maziwa mche mmoja wa sabuni a kilo of sukari maybe sembe!
Hakika hukukuta hata makuli walitajirika kwa kushirikiana na maofisa ugawaji kufanya ulanguzi!
Utawala julius miaka hiyo wanadunzi sio muhimu kuvaa sare aje tu shule kwa chochote alichojaaliwa kuvaa!
Mwinyi alileta mengi ya manufaa kwa nchi yetu
Kweli mkuu, mi nakumbuka nikiwa mdogo miaka hiyo(nilikulia Kariakoo,Tandamti na Jangwani,au tuseme, Tandamti na Msimbazi),nikimwona mtoto kavaa kandambili pea moja(yaani zinazofanana), nashtuka! nahisi kwao matajiri! maana kwetu ya kushoto azam,kulia yanga,au kushoto simba, kulia ..... yaani ni kawaida kuvaa kimasikini-masikini.

Nakumbuka kisa kingine nilienda kwa kucheza kwa jirani zetu, mida ya mchana ilipofika, ukaletwa ugali una rangi nzuri ya manjano kama jezi ya timu yetu ya Taifa...kwa nilikatazwa kula kwa majirani,niliporudi nyumbani nililalamika sana kuwa wale mbona ugali wao mzuri una rangi,na sisi wa kwetu mweupe!

Nakumbuka kuna mjomba wangu alifika kutoka kijijini, baada ya kupiga naye stori,jioni ilipofika tulimsindikiza kwa mjumbe wa nyumba kumi kumtambulisha (Mareh. Mzee Chaurembo- ILWIR).
Pia nimewahi kutumwa kupanga foleni kwenye "duka la kaya" kwa mahitaji kama sukari na unga.

Kwa kweli nami ni mmoja wa aliyeufurahia utawala mpya wa Rais Mwinyi.
 
Back
Top Bottom