Leeds Utd pamoja na Burnley zapanda Ligi Kuu ya Uingereza (EPL)

Leeds Utd pamoja na Burnley zapanda Ligi Kuu ya Uingereza (EPL)

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
11,451
Reaction score
9,974
Klabu za Leeds Utd na Burnley zimerejea Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kwa msimu ujao wa 2025/26.

Leeds Utd na Burnley zote zina alama 94 baada ya michezo 44 huku wakibakiza mechi mbili mbili kabla ya ligi ya Championship kufikia ukingoni. Kwa alama hizo hazitoweza kufikiwa na vilabu vya chini yao.

Timu ya tatu kupanda itapatikana kwa play offs ambapo inahusisha timu ya 3 mpaka ya 6 katika msimamo kucheza kwa mtoano ili kupata timu itakayoungana na Leeds na Burnley.

Wakati huo huo, Southampton, Leicester City na Ipswich Town wameshuka daraja katika EPL.
IMG_6480.jpeg
IMG_6481.jpeg
 
Back
Top Bottom