Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Lowassa is out of date.....tuangalie waasiasa vijana wenye maono mapya
Hoja hapa si kujua kama Lowassa anafaa ama umepita muda wake. Tunataka kujua hatima ya "ufisadi" aliofanya kwenye Richmond!!
 
kwa hii serikali dhaifu ya ccm usitegemee kitu kama hicho. afu sasa cha ajabu utaendelea kuishabikia hiyo serikali wakati haiwezi kuchulia hatua za kisheria watuhumiwa, sasa sijui utakuwa mtu wa aina gani?!
Mkuu bado hujamsoma huyo mleta mada
 
Kuna siku Prof.Beregu alisema jambo la msingi sana kwamba sasa Lowasa yupo peupe njooni mumshike
 
Hakuna waziri mkuu wa Tanganyika ,tuna waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania full stop

Siku njema
Mambo ya ndani ni mambo ya Muungano na Ripoti yake hupelekwa kwa Rais wala si Waziri Mkuu. Kumwita kwamba ni Waziri Mkuu wa Tanzania ni kiini macho tu, hana madaraka Zanzibar. Kwa mfano undhani ana madaraka gani Zanzibar?
 
Hoja hapa si kujua kama Lowassa anafaa ama umepita muda wake. Tunataka kujua hatima ya "ufisadi" aliofanya kwenye Richmond!!
Bunge kama muhimili unaojitegemea lilishatoa maamuzi. Adhabu aliyopata Lowassa ya kufukuzwa uwaziri kwa kibunge inatosha.
 
Ni kweli lazima ashitakiwe kama mshtakiwa wa Kwanza. Hata Mimi pamoja na UKADA wangu naona dhahiri Richmond ilikuwa galasa la kisiasa kwa EL. Mwakyembe alifanya siasa na kamati yake ili kuweza kumwepusha MTU mwingine na kikombe kile. Basi apelekwe Mahakama ya Mafisadi akahukumiwe baada ya kuhukumiwa na Mwakyembe the lawyer..
Hiyo mahakama haiwezi kufanya kazi hadi pale katiba mpya itakapo patikana
 
Mimi pia ningependa lowassa na sumaye wspandishwe kizimbani, mmoja ajibu tuhuma za ufisadi,mwingine matumizi mabaya ya madaraka na mauwaji ya watanzania huko visiwani.
Na kwa kuuza mashirika ya umma na nyumba za serikali
 
Mambo ya ndani ni mambo ya Muungano na Ripoti yake hupelekwa kwa Rais wala si Waziri Mkuu. Kumwita kwamba ni Waziri Mkuu wa Tanzania ni kiini macho tu, hana madaraka Zanzibar. Kwa mfano undhani ana madaraka gani Zanzibar?
Hivi waziri mkuu ni nani ?? Ni kiongozi wa shughuli zote za serikali sio ? Na raisi ni nani ?? Ni mtu mmoja sawa lakini ile ni taasisi ,maana ya taasisi ni kwamba hata kama report inakwenda moja kwa moja kwa rais ila kuna watu wake ambao wanahusika naye na huwezi kuniambia waziri mkuu hawezi kuwa mmoja wa hao watu ,mpaka hapo nimeshakupa mfano mmoja wa jinsi waziri mkuu anavyowajibika na Zanzibar kwa mfano wa Ripoti ya Kitwanga


Nilikuuliza hapo juu huku nijibu ,Waziri mkuu anapokula kiapo cha kutokutoa siri ,wewe unafikiri ni siri zipi ??
 
Kazi kubwa huwa kufungua kesi!
Kama wanashindwa kufungua Kesi mbona wana wepesi sana kufungua midomo yao na kubwabwaja mambo wasiyoyaweza? Kama Lowassa ni fisadi basi kesi yake iwe ya kwanza kufikishwa kwenye Mahakama ya mafisadi!!
 
Ukiangalia kwa harakaharaka, utadhani mtoa mada ana hoja kumbe kioja.

"Lissu mmoja au Kibatala mmoja ni zaidi ya mawakili wote wa Jamhuri (including AG Masaju na DPP)" By Malisa GJ,
 
Back
Top Bottom