Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Nasikia serikali ilivunja mkataba na Dowans, nao Dowans hawakukubali wakaenda mahakamani ambako Tanzania iliamriwa kulipa mapesa kibao kwa Dowans na hakuna mtu anyehoji hilo hapo, tuna akili au tumerogwa?
Dowans alipolipwa akamuuzia Symbion mitambo hiyo ambayo, hadi kesho inadunda bila wasiwasi.

Hii inanikumbusha kesi ya minofu ya samaki na meli ya wachina. Tanzania ilipona na hapo au iliamriwa kuwalipa fidia wachina! Nani alikuwa front kwenye sakata hilo?? Mijitu haihoji vitu vya msingi inakalia ushabiki wa kisiasa tu.

Nasikia kiu ngoja niende Kebby's Hotel nipate moja baridi.
Ukisha kunywa uropoke huko,uone kama hujanyea ndo
 
Usisiasishe hoja bwana, hao wanaochafuana kwenye siasa labda ndiyo mchezo wao unavyochezwa. Sisi hapa tunataka sheria ifuate mkondo wake. Lowassa ashitakiwe, Full stop!!
Kama hamchezi siasa mnataka ashitakiwe na nani wakati waliomchafua mnawaona? Waliokuwa kila siku wakija na hoja bungeni za kuunda kamati za Bunge ndo waliomchafua; washaurini walete hoja nyingine za kuunda kamati za bunge za kumsafisha!
 
KWELI IJULIKANE MBIVU NA MBICHI

USHAHIDI KWA SERIKALI NI WATANZANIA AKIWEMO
Mambo ya ushahidi ni wakati Kesi itakapoanza. Nataka kujua wewe unataka Lowassa afikishwe kwenye mahakama ya Mafisadi?
 
Kiashiria cha udhaifu kwa binadamu wakati mwingine ni pale anaposhindwa kulifikisha mwisho jambo la muhimu analotakiwa kulikamilisha. Sisi kama taifa tumekuwa tunatangatanga na Jambo lililosababishwa na mtu mmoja tu na sisi kama taifa tumeshindwa kufikia mwisho wake.

Tarehe 7/2/2008 aliyekuwa Waziri wa Mkuu wa Tanganyika wakati ule, Edward Ngoyai Lowassa alijiuzulu wadhifa wake baada ya kutuhumiwa kuingilia mchakato wa Zabuni ya Ufuaji Umeme iliyosababisha kuletwa kwa Kampuni ya Ufuaji Umeme ya Richmond nchini. Tangu kujiuzulu kwa Lowassa mpaka sasa imeshapita miaka zaidi ya 8 na miezi kadhaa, lakini bado suala la sakata la Richmond halijaisha

Mitambo iliyoletwa na Kampuni ya Richmond ambayo bado ipo Pale Pale ilipofungwa na Kampuni ya Richmond, imeshabadilishwa umiliki wake mara mbili. Imetoka kwa Richmond ikanunuliwa na Dowans na sasa inamilikiwa na Kampuni ya Symbion ya Marekani. Lakini sisi kama taifa tumeachwa pale pale tulipokuwa Mwaka 2008.

Kwa kuwa kuna Mahakama ya Mafisadi inaundwa na sisi kama taifa tunayumbishwa na suala la mtu mmoja tu, ambaye si kiongozi wa serikali kwa sasa, nashauri Kesi ya Kwanza kwenye Mahakama ya Mafisadi iwe ni hii ya "Ufisadi" wa Edward Ngoyai Lowassa kuhusu Ufisadi wa zabuni ya ufuaji umeme iliyosababisha Sakata la richmond.

Ni lazima Lowassa ashitakiwe ili kama yeye anao ushahidi tofauti na ule ambao wapinzani wake wanao aje nao mahakamani ili upimwe kwenye mizani ya kisheria tujue nani mkweli kati yake yeye na wapinzani wake.

Haiwezekani mitambo ile iliyoletwa na Kampuni (Feki?) ya Richmond bado ipo nchini mwetu, inafua umeme, Tannesco wanalipa Capacity charges tanesco wanauziwa umeme kutokana na mitambo ile ile iliyokuwa ya Richmond, mkataba ule ule wa kati ya Richmond na Tannesco ndiyo umekuwa ukihuhishwa na Dowans na sasa Symbion, lakini sisi kama taifa bado tunakumbushana mambo ya mwaka 2008.

Kuukata Mzizi wa fitina ni lazima Lowassa na kama wapo na wengine waliohusika na sakata la Richmond wafikishwe kwenye Mahakama ya mafisadi mara tu Mahakama hiyo itakapoanza kazi. Tunataka Kesi ya kwanza kwenye mahakama hiyo iwe dhidi ya Lowassa na wenzake waliohusika na suala la Richmond.

KESI YA LOWASSA ISIPOKUWA YA KWANZA KWENYE MAHAKAMA YA MAFISADI NITASHANGAA KWELI KWELI!!
Sasa wewe si mtanzania?una haki ya kufungua mashitaka hivyo kusanya ushahidi nenda mahakamani,unataka Nani akusaidie wakati hawaoni ufisadi wake
 
nimekuelewa mtoa hoja. Lazima afikishwe mahakamani haraka........vinginevyo wimbo wa ufisadi tuufute. Chadema baada ya kufanya uchunguzi wa kina waligundua kuwa ni uzushi tu, wakafuta cd yao ya ufisadi dhidi ya EL.
Kuna taarifa kuwa Dk. Slaa alikula dili na waliokuwa wanamwinda EL, wakampa makablasha ya kimagumashi na yeye akawamezesha wenzake, wakaunda bendi na kuanza kufanya shoo za wimbo wa Lowassa ni fisadi kwenye mafiesta kote nchini
 
nimekuelewa mtoa hoja. Lazima afikishwe mahakamani haraka........vinginevyo wimbo wa ufisadi tuufute. Chadema baada ya kufanya uchunguzi wa kina waligundua kuwa ni uzushi tu, wakafuta cd yao ya ufisadi dhidi ya EL.
Kuna taarifa kuwa Dk. Slaa alikula dili na waliokuwa wanamwinda EL, wakampa makablasha ya kimagumashi na yeye akawamezesha wenzake, wakaunda bendi na kuanza kufanya shoo za wimbo wa Lowassa ni fisadi kwenye mafiesta kote nchini

Hahaha mnajidanganya
 
Mheshimiwa Spika. Nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya bunge mpaka ofisini kwangu hata wangeniita ningeenda kwa mguu kama hamna gari. Na nilikuwa tayari kufanya hivyo.Hawa ni watu makini sana, siwezi kuamini kwamba wanaweza kufanya Oversight kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga, walisema Waziri Mkuu ilikuwa hivi, kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza, Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano Mheshimiwa Spika, kufuata utaratibu wa Westminster kuthibitisha hapo unaposema, wenye Richmond ni fulani uka- table Record na ushahidi kwamba ni fulani?
Hapa ndipo kwenye kila kitu!!?

Kwa nini hawakuwataja mpaka leo!!?
 
Kiashiria cha udhaifu kwa binadamu wakati mwingine ni pale anaposhindwa kulifikisha mwisho jambo la muhimu analotakiwa kulikamilisha. Sisi kama taifa tumekuwa tunatangatanga na Jambo lililosababishwa na mtu mmoja tu na sisi kama taifa tumeshindwa kufikia mwisho wake.

Tarehe 7/2/2008 aliyekuwa Waziri wa Mkuu wa Tanganyika wakati ule, Edward Ngoyai Lowassa alijiuzulu wadhifa wake baada ya kutuhumiwa kuingilia mchakato wa Zabuni ya Ufuaji Umeme iliyosababisha kuletwa kwa Kampuni ya Ufuaji Umeme ya Richmond nchini. Tangu kujiuzulu kwa Lowassa mpaka sasa imeshapita miaka zaidi ya 8 na miezi kadhaa, lakini bado suala la sakata la Richmond halijaisha

Mitambo iliyoletwa na Kampuni ya Richmond ambayo bado ipo Pale Pale ilipofungwa na Kampuni ya Richmond, imeshabadilishwa umiliki wake mara mbili. Imetoka kwa Richmond ikanunuliwa na Dowans na sasa inamilikiwa na Kampuni ya Symbion ya Marekani. Lakini sisi kama taifa tumeachwa pale pale tulipokuwa Mwaka 2008.

Kwa kuwa kuna Mahakama ya Mafisadi inaundwa na sisi kama taifa tunayumbishwa na suala la mtu mmoja tu, ambaye si kiongozi wa serikali kwa sasa, nashauri Kesi ya Kwanza kwenye Mahakama ya Mafisadi iwe ni hii ya "Ufisadi" wa Edward Ngoyai Lowassa kuhusu Ufisadi wa zabuni ya ufuaji umeme iliyosababisha Sakata la richmond.

Ni lazima Lowassa ashitakiwe ili kama yeye anao ushahidi tofauti na ule ambao wapinzani wake wanao aje nao mahakamani ili upimwe kwenye mizani ya kisheria tujue nani mkweli kati yake yeye na wapinzani wake.

Haiwezekani mitambo ile iliyoletwa na Kampuni (Feki?) ya Richmond bado ipo nchini mwetu, inafua umeme, Tannesco wanalipa Capacity charges tanesco wanauziwa umeme kutokana na mitambo ile ile iliyokuwa ya Richmond, mkataba ule ule wa kati ya Richmond na Tannesco ndiyo umekuwa ukihuhishwa na Dowans na sasa Symbion, lakini sisi kama taifa bado tunakumbushana mambo ya mwaka 2008.

Kuukata Mzizi wa fitina ni lazima Lowassa na kama wapo na wengine waliohusika na sakata la Richmond wafikishwe kwenye Mahakama ya mafisadi mara tu Mahakama hiyo itakapoanza kazi. Tunataka Kesi ya kwanza kwenye mahakama hiyo iwe dhidi ya Lowassa na wenzake waliohusika na suala la Richmond.

KESI YA LOWASSA ISIPOKUWA YA KWANZA KWENYE MAHAKAMA YA MAFISADI NITASHANGAA KWELI KWELI!!
Eti "nitashangaa kweli kweli",,,,,who care ukishangaa au usiposhangaa??

Kama hii issue inamhusu Lowassa and he is no longer in power, ni kwanni Kikwete na hata huyu Magufuli hawakuivunja huo mkataba?

Kwanini Kikwete na serikali yake hawakumpeleka Lowassa mahakamani mpka leo?

Wewe ni nani unaekuja kulialia hapa wakati wahusika (Kikwete) ambao walikua na obligations ya kumshitaki hawakufanya mpka wanatoka madarakani?

Lazma mkubali mlishashindwa mapema mno maana hiki kinachoitwa Mahakama ya mafisadi ni kisingizio tu maana hata Mahakama hizi zilizopo zingetosha kumfikisha Lowassa huko... these are the delay tactics as you have no substantive reasons and evidence on this matter...

Simtetei Lowassa, lakni ninyi ni waoga mno na hakika mnaujua ukweli wa Richmond na kama mnajiamini sana nendeni mahakamani leo msisubiri kesho...
 
Keanu hayo majengo hayajakamilika? Si mwende mkafungue? Mmegwaya logme in; visandarusi; vijisent; vya mboga;escrow;green finance;meremeta and so on. Mnakuwa kama nyani asiyeweza kujiona makalio yake lakini anawacheka wenzake. Mnakoipeleka nchi hii siko alikopenda Mungu. Am sure atawachanganya lugha tu muwe kama Mara wa babeli
 
mleta uzi kwa kuwa wewe ni Raia na unadai Lowasas alihusika na ufisadi huo kwa uthibitisho wa bunge na taarifa nyingine,nakupa ushauri wa bure kwa kuwa unalipa kodi na unauchungu na kodi unayotoa ambayo pia ilitumika na inatumika katika kuilipa hiyo kampuni pamoja na kwamba imebadilishwa majina mara mbili,hiyo mahakam ikianza kufanya kazi MARA MOJA WAHI UKAMFUNGULIE KESI LOWASSA,nitakufadhili wanasheria ili wakuaidie
 
Hotuba ya Mheshimiwa Edward Lowassa aliyotoa Bungeni wakati anajiuzulu Uwaziri Mkuu.

Nakushukuru mheshimiwa Spika kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii. Lakini la pili nimpongeze Dr. Harrison Mwakyembe Mwenyekiti wa Kamati teule,kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri sana.Kwa kazi nzuri kwa maoni yao na wameiwasilisha vizuri.Lakini Mheshimiwa Spika, nimesimama kuweka kwenye Kumbukumbu kutokuridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa.

Mhesimiwa Dr. Harrison Mwakyembe ni mwanasheria tena daktari alikuwa anafundisha wanafunzi Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni Natural justice. Wewe pia Mheshimiwa Spika ni Mwanasheria, unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba katika Kamati Teule, imesikiliza watu wengine wote, pamoja na waliowaita minong’ono ya mitaani. Wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja katika watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja!

Mheshimiwa Spika. Nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya bunge mpaka ofisini kwangu hata wangeniita ningeenda kwa mguu kama hamna gari. Na nilikuwa tayari kufanya hivyo.Hawa ni watu makini sana, siwezi kuamini kwamba wanaweza kufanya Oversight kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga, walisema Waziri Mkuu ilikuwa hivi, kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza, Waziri Mkuu wanasema ulitoa dokezo hili ni sawa sawa ni kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano Mheshimiwa Spika, kufuata utaratibu wa Westminster kuthibitisha hapo unaposema, wenye Richmond ni fulani uka- table Record na ushahidi kwamba ni fulani?

Mheshimiwa Spika Taifa letu ni taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa Demokrasia pa kubwa katika nchi yetu pote, hapa ndipo penyewe. Kama katika chombo hiki haki haitaonekana kutendendeka, Mheshimiwa Spika nchi haitakwenda vizuri.

Hapa ndipo tunategemewa kuonyesha umakini, umahiri wetu katika mambo ya Demokrasia. Kwa hiyo nilichofanyiwa Mheshimiwa Spika napenda kuweka kumbukumbu sahihi…sawa. Kwamba naona si sahihi, na nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana na nimeonewa sana katika hili. Maana zimechukuliwa tuhuma zikaja kuelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo, mimi sijaulizwa. Kulikuwa na shida gani kuniuliza. Kwa nini muamini minong’ono ya mitaani kuliko maelezo yangu?

Sisi wote hapa ni wanasiasa, tukianza kuamini minong’ono ya mitaani, niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi… Tume wamepewa muda wa kutosha kabisa, lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Lakini mheshimiwa Spika, hata pale uliponinong’oneza ukaniambia “una ushahidi wowote”? Nilikupa ushahidi huo wa maandishi. Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka Ofisi ya Waziri Mkuu, hata mmoja! Lakini kitabu cha Majedwali kimejaa majedwali meengi pamoja na Magazeti mpaka ya Udaku, lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika. Mimi naamini ingekuwa ni heshima wangeliweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii na hii na hii. Mimi nadhani ingejengwa hoja. Lakini kujenga hoja na kuja hapa bungeni, tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki, amefanya hiki bila kumsikiliza, nachelea kuuliza, hivi watu wa chini itakuwaje?

Lakini Mheshimiwa Spika nimetafakari kwa makini sana jambo hili, nikajiuliza, hivi hasa kulikoni. Mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu, wenye heshima zao. Mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo, kulikoni?

Mimi nadhani, they have a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndiye amefanya haya, ionekane Waziri Mkuu amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe. Mheshimiwa Spika. Nimetafakari sana, kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya serikali yangu, nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.

Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa, kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini na kutokukubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya bunge wa kunisingizia.

Mheshimiwa Spika nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais kwa heshima aliyonipa ya kutumikia nchi hii kwa Uwaziri Mkuu kwa miaka miwili, namshukuru sana mheshimiwa Rais. Nakushukuru wewe, nawashukuru Mawaziri na Manaibu Mawaziri, nawashukuru waheshimiwa Wabunge, na wanachama wa CCM tuliosimamia Ilani ya Uchaguzi ya Chama chama Mapinduzi. Baada kusema hayo nakushukuru Mheshimwa.
Asante Allen kwa kuiweka hii hotuba hapa.

Nilimsikiliza Lowasa siku ile akizungumza bungeni sikumuelewa na mie pia nilijazwa ushabiki na kumnanga kwa makofi, vifijo na hoe hae nyingi pale alipotamka kujiuzuru.

Pia nimeendelea kuisikia hotuba hii mara kadhaa na kuipuuza lakini siku aliposema mwenye ushahidi aende mahakamani na hakuna aliyejitokeza hapo nikaingiwa na kigugumizi.

Leo nimeisoma tena na tena, kuna kitu kikubwa sana nimejifunza khs Lowasa na hasa baada ya hekaheka za mwaka wa jana.

Mungu ambariki Lowasa, hotuba hii inaishi na kuna siku mambo yatatoka hadharani ni suala la muda tu.

 
Hata akishitakiwa mawakili wa serikali wenyewe hawapo serious a.k.a v***** lowassa atachomoa tuuu....
 
Hata akishitakiwa mawakili wa serikali wenyewe hawapo serious a.k.a v***** lowassa atachomoa tuuu....
Hilo la kuchomoa kwa Lowassa sisi wengine wala halitusumbui. Lakini tunachotaka ashitakiwe!!
 
Back
Top Bottom