Hapana mkuu zinashuka
Tumerejea Latino katika safari yake *********** inaendelea
Kama nilivyosema inapofika usiku muda huo nakosa amani kabisa kutokana na vutu vya ajabu ambavyo nilikua naviona pale kisiwani kwaiyo sikupenda kabisa usiku uingie.
Basi nikaendelea kuwepo katika kisiwa kile na maisha ni Yale yale na hata chakula msos ndio ulikua ule wa kaa gogo ila kuna siku nilimpata samaki chewa akiwa ameharibika kafa tayari.
Nikamtengeneza vizuri akawa msosi safi kwangu lakini pia katika kile kisiwa palikua na panya wakubwa wanaendana na ndezi pia walikua wanauma wana meno makali sasa yale mabaki ambayo Mimi nilikua nayaacha wao ndio walikua wanafata kula ivyo nao niliwafanya msosi wanapokuja nilikua nawachoma na ule mti nilio uchonga wakushikia kaa kisha nawachoma natafuna msosi.
Basi katika kuendelea kuwepo pale kama nilivyosema palikua na kelele za ajabu ambazo zilikua zinatoka kwenye msitu apo kisiwani sasa siku iyo mida kama ya saa kumi zile sauti nikazisikia tena sio usiku kama nilivyozoea safari hii ni mchana na jua lake ndio zinapiga,
Sasa nikaona sio kweli nikavaa ujasiri nikaona ngoja nizifatilie zile sauti zinakotoka nijue ni za nini zilitoka ndani kabisa ya msitu.
Basi nika elekea uko nijue kuna nini nikaenda msitu umefunga kwaiyo nilikua nafanya kutanua miti ivi kisha napita taratibu taratibu nikifata zile sauti zinakosikika nilikwenda mpaka nilipokaribia zinakotoka zile sauti nikatulia kwa umakini nikapata nafasi nzuri kisha nikachungulia laivu kabisa nikaona sehemu ya tukio.
Palikua na viumbe na hao viumbe ni nyani wakubwa sio sokwe ni kama walikua wanafanya sherehe kabisa mana walizunguka ki mduara na katkati palikua na wengne kama ndio wahusika na palikua na ngoma izi za miti sio ngozi zile za mfano wa marimba ambazo unapiga na miti waliweka miti ndio wakawa awa nyani wanapiga na wengne wakiwa na shangwe kabisa bila shaka historia aikukosea kusema binadamu tulianzia uko pale palikua na shughuli ambayo wao walikua wanaifanya kama sherehe
Nakazia walikua nyani sababu pale unaweza hisi ni majini lakini kama ni majini Basi ata pale nisinge wafikia na nyani tuna shahabiana na binadamu ata kiakili mengne wanafanya kama binadamu ndio walikua wakifanya shughuli ile pale msituni lakini pia ni ngumu mno kuona yani bahati sana binadamu wa kawaida kuweza kuwaona.
Basi nikiwa natazama kile kinacho endelea pale lakini pia kuna kua na shida endapo ikitokea wale wakajua
nami ndio ikanikuta sababu kumbe pale pana ulinzi yupo ambae anakaa sawaia kuhakikisha akuna kiumbe cha tofauti kinakuja pale kama akiona anaenda haraka kutoa taarifa kabla ujawafikia ina maana mpaka mimi nakwenda pale yule mlinzi wao akuniona bado.
Sasa nikiwa natazama ghafla kuna nyani mmoja alitokea maeneo yale nilipo Mimi uyu sasa ndio alikua mlinzi alikua spidi akaelekaea kule kwa wenzake kutoa taarifa alafu alikua anatoa mlio flani ivi lakini nae alivofika akapigwa makofi na wenzake inavyo ashiria alichelewa alafu baadae akaonesha uku nilipo Mimi hapa sasa nikajiona nipo kwenye hatari ili ni janga akuna kingine zaidi ya kuondoka eneo lile.
Wazo la haraka kupanda kwenye mti uongo kwaiyo nika amua nikimbie na wale nyani wakaunga pale pale kuja kwangu nao spidi aya yalikua madume maana yalikua makubwa sana.
Nilitoka mbio mpaka pale kwenye kibanda nilichofanya sikukaa pale nilikimbilia kwenye maji pale kibandan nilichukua lile dumu kama itatokea wakaingia kwenye maji niende mbali japo sikua na hakika kama wanaweza ingia majini nikaenda nalo dumu mpaka kwenye maji kule nao hao mi nikaingia kwenye maji wao wakaishia ukingoni pale mwa maji ufukweni.
Nilikaa ndani ya maji mule karibu saa nzima wao wapo pale nje wana nisubiri mi nawatizama tu pale baadae wakati Giza linaingia wale nikawaona wanaondoka wakapotea nami nikarudi pale kibandani japo nilikua na hofu lakini mara nyinngi nyani inapofika usiku huwa ana ujanja wa kiasi hicho kwaiyo nilirudi pale bandani.
Siku ya pili asubuhi baada ya kuamka tu ile nikaanza kusaka msosi kuwinda wale wadudu mule pembezoni mwa fuke aisee nikakutana na mshikaji mmoja kati ya wale ambao tuligongwa na meli ambao tulifika kuweka makazi pale kisiwani nilimkuta akiwa katika hali mbaya.
Kachoka na alafu ana vidonda vya kung'atwa na wale panya ambao nilikua nawatafuna nikiwapata pale kibandani wanapokuja kusaka masalio, jamaa kumbe nae pale katika kusambaratishwa aliogelea na kipanda cha ubao cha boti na pale alifika Ila sasa alivunjika mguu mfupa ulikua nje unaonekana
Sasa pale alivyofika mwanzo alikua anatafuta chakula kwa kujivuta kutokana na kuhumia mguu Ila mbeleni alishindwa ndio mana akazoofika nami nilimkuta kwenye hali iyo.
Akaniambia pale yeye angeshakufa isipokua kuna usiku mmoja wakati kama amelala kuna wadada wawili walimtokea yani ndotoni akiwa kwenye usingizi walifika wakiwa na marash yani wananukia kisha wakampa mpole na wakamuuliza hapa mmekuja kufata nini?
Kisha wakatoa kinywaji flani kama maziwa wakampatia anywe akanywa baadae alishtuka na aliweza kukaa kama takriban siku tatu au nne pasipo kusikia njaa.
Jamaa alikua kwenye kauli ya mwisho na ile kuonana na Mimi ndio Mara ya mwisho kwani akuchukua mda alifariki pale pale mbele yangu mwana alikufa nikimuona kumbuka mtu wa pili namshuhudia akifariki.
Nikachimba shimo kumsitiri mshkaji na nikamuhifazi nikampigia dua njema aendako ki ukweli sikua na raha siku iyo maana sasa hisia mbaya zikawa zinanijia kwamba hapa nami nitakufa tu japo nilikua Nina nguvu zangu bila shida yoyote mana sikuumia popote.
Pia pale kisiwani niliiishiwa maji nikawa natumia yale maji yanayopatikana kwenye miti flani unaikata kisha inamwaga maji ya kutosha ndio nikawa sasa natumia ayo.
Siku zilikatika, siku moja sasa nikiwa pale ufukweni kwa mbali nikaona kimeli kidogo ivi kipo na jahazi nyuma wamelifunga wanavuta na walikua wanakuja upande niliopo Mimi pale ufukweni apo nilijificha kwanza nikiwatazama walifika mpaka pale wakashuka walikua ni wasomali walishuka na mirungi na bunduki alafu wale kumbe walikua ni mahalamia wa kuteka meli baharini.
Baadae Mi nikajitokeza, fasta sana wakanipigisha magoti na kuniweka chini ya ulinzi mitutu yote kwangu wakaniuliza jina langu pia dini yangu kiswahili wanakielewa nikawatajia mi ni muislamu wale jamaa nao pia ni ivyo ivyo nivyotaja jina wakasema kuna nabii mwenye jina lako alipata matatizo na akaja kuokolewa na wapita njia una mfahamu?
Nikamtaja basi wakasema nawe pia umeokolewa na sisi pia wakaniambia nisome sura flani ivi ya kufungua ibada waislamu wana elewa ili ufanye ibada unaanza na sura iyo inaitwa surat infaata nikawasomea vilivyo mpaka mwisho uzuri nilikua nafahamu wakaelewa kwa kuitikia msahalaah na kunikaribisha .
Katika wale kwenye lile kundi pia kulikua na mtoto wa kike na pia alikua na kaka yake uyu wa kike aliitwa Sofia na kaka mtu aliitwa Masud yule sofia nilimuona na silaha
sub machine gun (SMG) double magazine zilizo jaa risasi na wale wengne walikua na bunduki za AK47 fourty seven sasa nilijiunga na wale jamaa kwenye ile kambi tukawa pamoja yule Sofia alikua akikaa sana na Mimi akiniulizia sana story jinsi nilivyoweza Ku survive
pale nilipo
basi alikua anapenda sana zile story wale wasomali kufika kwao pale chombo chao kilikua na matatizo ..................................
Tupumzike tutarejea Latino is on....
Jamaa alianguka akateguka.......mara mkaanza kuparamia mbususu za maporini 😏Tuendelee
Baada ya kutolewa pale tukafikishwa eneo husika kwa mkuu wao tukajumuishwa pale usiku umeingia zikawa zinapigwa ngoma za asili wanacheza alafu wengne wanakunywa vinywaji vya asili pamoja na nyama tofuti tofauti zilkia nyama za nyani pale maana palikua na vichwa tuliviona na sisi tukapewa apo akuna kuchagua tukala msosi.
Sasa kukaa kwetu pale mmoja wetu akanogewa bana kwann sababu pale watoto wa kike mabinti walikua wanaacha baazi y sehemu za miili yao wazi hasa kifua na wale mabinti
matiti wndio anaacha wazi kabisa yamesimama si mabinti bado wasichana chipukizi alafu sasa apakua na uchoyo yani unajipakulia tu unatafuna hii ndio ilifanya jamaa anogewe sisi kwetu ilikua laisi kwa sababu bado tunang'aa tumetoka mjini tupo soft.
Jamaa yetu alijimiliksha wasichana wawili kujifanya kama mfalme ivi kwa upande wangu nilichagua msichana flani ivi ambe ni mixa mzaz mmoja mweus mwngne mzungu Africast ki ujumla watoto walikua wazuri tuishie hapo.
Pale tulizoeleka safi tu ila kuna muda tulihitaji kuondoka tuka wataarifu wakasema tusubiri kwanza kuna usafir utakuja tunaweza pata ivyo ikabidi Tuendelee kukaa na pale burudani namna iyo tukaendelea kuwepo.
Palikua na jenereta pale na TV ya chogo wale wazungu ndio walikua wameleta ivi tunaangalia muv ila za zamani kule wanshangaa sie tayari tunazijua sasa kama tukio unafahamu ndio una hadithia pale
Mwisho wa siku walikuja pale wazungu na misaada yao pamoja na kufata madini sie walitupa pesa kidogo za msumbiji zinaitwa (mitcash) kwa ambao wamepita msumbiji kam mhandika uzi. tunazijua hizi kuna mpaka elf 25 ya noti moja mpaka ef amsini noti moja peke yake.
Tulipata lift ila sehemu tuliokua tunakwenda kwa muda huo panaitwa beila ili tupite uko kwenda msumbiji ndani.
walitubeba walifika mahali wakatuacha s maana awawezi kwenda na sisi ,, walipo tuacha ilibidi iyo sehemu turuke fensi tuliruka vizuri tu fresh tukasonga mbele kulekea beila pale mmoja kati yetu akabaki mie na mangushi tuliachana mbele mi nikaelekea Richard bay kuitafuta south uko lakini lazima ufike Maputo .Na uyo mangushi ye alienda kwenye huo mji wa mangushi.
Niliingia gari ice apo sasa ni mjini nilikwenda mpka kwenye beach flani ivi usiku nilifika nikajichanganya pale palikua na washkaji pale nilijitambulisha kama nilishawai Fanya uvuvi pale kule kisiwani na palikua karibu na kule ivyo nikajiunga pale nikaanza kufanya vijikazi kujichanga kidogo ili nivute nguvu ya kwenda uko ,
lakini maeneo Yale lazima uwe makaini sio wote watakupenda ilo ulitambue.
Sasa nilikaa pale nikifanya vijikazi na washikaji kula ilikua donei kujichanga ila kuna jamaa aliitwa joakim yeye alikua sometimes achangi alafu ana fosi kula siku iyo ulipita mchango tukaenda nunua nyama jamaa akuchanga kama kawaida yake sasa basi pika msosi na nyama tumetenga tule jamaa uyu anasogea atuja muita akanawa kutaka kula mshikaji mmoja akamshika mkono na kumzuia vipi we si umegoma kuchanga na sio Mara moja Joakim alichoamua aka kanyaga kile chakula kwamba tukose wote ...........
Tutaendelea
Wazee wa mali za mjerumani nadhani wamekusikia sasa washindwe wenyeweTupo hewani tuendelee kusonga tukamalize mkasa
Kutokana na yale magumashi ikabidi tuachane na yule bibi tukaangalia ishu zingne sasa Mimi nilikwenda kwa mama yangu mzazi ambae alitengana na baba alikua kaolewa sehemu nyingne yule baba ambae alikua kamuoa mama sio baba angu mzazi aliniambia kuna msitu una ivo vitu vya kale ambapo hapo kuna makaburi yapo lakini uendi hivi hivi kuna mauza uza wao waliwai kwenda hapo kufagilia makaburi ilikua saa nne tu asubuhi wakapotea makaburi awakuyaona na eneo ni ilo ilo walirudi siku iyo awakufanya kazi.
tukajipanga ikabidi tufike eno husika kufatilia ivyo vitu tumefika eneo lenyewe sasa ilikua ni kwenye kisima ndio kuna izo Mali ila kisimani akuna maji yalisha kauka muda mrefu wakati tunafika pale kwanza tukakuta fuvu la mtu lipo kwenye miti ivi imefungana alafu pembeni kuna nguo zimechakaa zimeliwaliwa na mchwa sisi tukasonga hapo kwenye kisima kuchungulia kuna Giza kuu kisima kirefu alafu ndani kuna kitu kina ng'aa sana kumuuliza mzee akasema hapo pana nyoka mkubwa na ndio mlinzi wa hizo Mali sasa kinachotakiwa apatikane mtaalamu ili tutoe izo Mali bila ivyo aiwezekani .
mtaalamu tuli mpata alikua ni shehe kaja pale yuko full gado na vitabu vyake kwajili ya kusomea na anajiamini sana kana kwamba tayari alishawahi toa ivo vitu akaanza kusoma wakati yupo pale kisimani
sisi kutokana na uoga tukapanda kwenye miti ye tukamuacha chini akapiga kisomo sana muda mrefu bwana ilitoka mizizi chini kule ikaja juu pale kwa shehe na kumvika alafu inamvutia chini kisimani jamaa yetu mmoja sijui alikua na ujasiri gani akaenda msaidia kumvuta ile miziz ikaachia ikarudi chini na yule shehe kukimbia naona zilikua salamu tu kwamba hana uwezo huo wa kumtoa yule nyoka pale zoez likashindikana tukaondoka patupu izi Mali za wajerumani inasemekana kuna uchawi mkubwa sana upo humo kwaiyo kufanikisha ni kazi ngumu na kuna mitego ipo humo kufa ni swala la dakika tu unapoingia uko. unajitoa mwanga na kuna kodi zao maalumu ambazo wenyewe wanajua.
Jamaa flani ivi vijana wakapata taarifa kuhusu lile eneo ni wa huko kijijini wakaona sisi tumekurukupuka na vile tumetoka mjini awajui kitu ngoja twende sisi wakajikoki vizuri ili wakafnye ilo zoezi na wakatafuta mganga awakutak shehe sababu ana soma dua wao waliamini dua ni mpaka mungu aipokee ivyo kwa haraka ni mganga itakua sahihi kwao basi
Yule mganga aka waambia walete kuku wao walikua wa tatu na mganga wa nne wakaenda eneo husika wamefika mganga akaanza manyanga yake piga tambiko mwisho aka waambia uyu kuku tuna muacha hapa tunakaa siku tatu tunakuja kuangalia asipo kuepo ina maana sadaka imekubaliwa na kinachobaki ni Mali kuchukua basi na tukimkuta kuku bado yupo sadaka aijakubaliwa yule kuku akaachwa pale wao wakaondoka kusubiri zile siku ,
Zile siku tatu zikatimia wakarudi pale yule kuku yupo ina maana sadaka aijakubaliwa mganga aka waambia wasubiri tena siku tatu wakasubiri kurudi yupo ambae alitoa yule kuku nyumbani kwake akaamua jambo moja amchukue kuku wake wenzake walimkataza walimwabia uyu kuku keshafanyiwa dawa muache jamaa aligoma na akasema mganga muongo akamtoa pale wakati wana ondoka yule nyoka kule chini alitoka na kuanza kuwafukuza ila walifanikiwa kurudi nyumbani japo msitu upo mbali sana na kijiji ila kuku jamaa alimpoteza msituni wawili walikua wa kijiji kimoja mwingne kjiji kingne wale wawili kwao walipoulizwa akuna walicho kisema baadae mmoja akaumwa akafariki akafata mwingne nae akafariki yule mwenye kuku alie mtoa alibaki mzima mpka sasa ivi yupo lakini ni chizi ilibidi mganga afwatwe kuulizia imekuaje ndio katika kuagua akaona tukio ambalo liliwakuta na waljchofanya hapo ndio taarifa zikasambaa.
uyo aliebaki hua anarudi kule kwenye Mali lile joka linapo jigeuza kuna baazi ya Mali zinatoka sasa jamaa anapkwenda anzikuta anachukua na kuna sehemu anaenda kuuza alafu anaingia kwenye pombe akuna kingne anachofanya zaidi ya kunywea zile hela mpaka zinaisha na kule anako uza huwa wana mkadiria tu akija nazo ndio watu wanamuona yupo na mzigo wa ela anaishia kunywa tu.
Na icho kjiji ni njia ya kuelekea mzaramoni unapita ufulu unaeleka malumbo alafu kuna kijiji kinaitwa paraka alafu unaingia kidugalo cha kanga ni njia ya kuelekea Mzenga hapa katikati kuna vijiji ambako mzee wangu uyo ambae alimuoa mama baada ya kuachana na baba yangu mzazi ndio asili yake hapo na saizi kuna mji kule unaitwa parisi kwa upande wangu Mimi nipo dar hapa nafanya shughuli zangu nyingine za kujipatia kipato nashukuruni nyote.
MWISHO.
Ndugu zanguni Latino mkasa kaumaliza hapa Mimi pia nashukuru kwa kumuwakilisha hapa kwa kuweka mkasa wake na ndugu zangu wa humu ambao amkupata kusikia basi muusome japo palikua na changamoto nyingi za baazi ya member ambao walikosa ustarabu nashukuru kwa kumaliza mkasa
asanteni.
View attachment 1791112
Latino ni uyo mkono wa kulia iyo ni moja ya interview akismulia mkasa wake na mr davista .
Kuna sentesi inasema kufa ni dakika tu au kua kichaaWazee wa mali za mjerumani nadhani wamekusikia sasa washindwe wenyewe
Ki fupi jamaa ana connection ya ishu nyingi .Asante sana mkuu, msalimie sana Latino mwamba... Stori ni nzuri sana.
Mtu kama Latino akipata mchongo kushughulikia wauza unga... Hawachomoki.
Ina maana Latino hakutoboa?