Laini kama supu ya mapupu

Laini kama supu ya mapupu

Mimi nina wasiwasi na njia wanazotumia.
Watu wanaweza kuitwa polisi kwa mahojiano yakafanyika na mwisho wa siku mnaambiwa watu hao hawakukutwa na hatia.Itakua ni upotevu wa rasilimali.
Sidhani kama Tanzania tuna ujasiri wa kutaja wauza unga og kwa sababu wanajulikana ila maigizo yanafanyika mengi na yote ni ili kupata sifa za kisiasa.
Nchi za wenzetu wanafanikiwa kiasi kwa kuwa na sheria kali na hawakuangalii usoni we ni nani au mtoto wa nani.
 
Hivi serikali yetu inaendesha rehabilitation centers/sober house ngapi hapa nchini?.kwa mwenye kujua atujuze na sisi.
Pili viongozi wetu eidha kwa kutokujua ama kwa makusu wanafungia macho na kushindwa kuwajuza wanachi kuwa Tanzania ni njia hub ya kusafirisha na kusambaza unga duniani,unga unaouzwa Tanzania ni kiasi kidogo sana tena mara nyingi wa ubora mdogo(makipi,crack etc) na ni sehemu ndogo ya picha kubwa.kuna hawa wenye connections na huko unga unapotokea.kuanzia poppy fields za afghanistan,maharamia wapikistan mpaka cartel za brazil zenye connection na wauzaji wa peru.huko kote kuna mikono na netwek ya wabongo.Hawa ndo big fish,hawa ndo tunaotakiwa kudeal nao,wale wanaoingiza ma bumu ya mifuko ya heroin yenye thamani ya mabilioni,sio wale wanaoweka ndugu na marafiki bondi pakistan kwa ma supplier ilo wapewe kilo kadhaa kuja kuuza na kulipa hela hao ni vidagaa.
Mizigo inakamtwa ulaya huko marekani na china.yote imetokea bongo sasa hamjiulizi huo mzigo kwanini utokee Tanzania upelekwe china,europe na kwengineko,kwani tunauzalisha hapa,kama hapana then unakuja kugundua kuwa Tanzania ni kituo cha clearing and forwarding ya ngada.
Hivi shkuba kesi yake bado iko kwenye due process?
 
Kwa hapa kwetu tutaishinda hii vita manake bado ma Don hawaja invest sana kwenye majeshi yao.
TUTASHINDA
Taarifa zenyewe za list tumeishia kuiona kwa Makonda.

Madawa yenyewe yanayoingizwa nchini usikute yanayokamatwa ni 10% ya yote yanayoingizwa.

So hakuna mwenye uhakika wa kama hao maDon wameinvest vya kutosha hapa nchini kwenye hayo majeshi Yao.
 
Hii vita ya mkuu wa mkoa sidhani km itakuwa endelevu ingawa amefanya jambo jema


Nadhani angeunda kitengo maalum kushughulikia hili suala kwa muda mrefu
Kakurupuka sana asidhani hii ni sawa na ile ya kero za wanadarisalama
 
Alafu sisi watanzania tuna mambo ya ajabu sana, kila kukicha tunajitahidi kuleta taarifa za kutishia kila anayeonesha dhamira ya kutaka kujaribu kupingana na madawa ya kulevya, tunavunjana moyo sana watanzania.
Kila kinachofanyika linaibuka tabaka la watu kudai hicho sio, flani anaonewa.

Utasikia kuna siasa ndani yake.

Ivi jamani tunataka nini hasa?

Mnatishia kuhusu ukubwa wa mtandao, mnatishia kuhusu gharama, eti mnajilinganisha na nchi ya Marekani katika ishu ya madawa ya kulevya huu ni utoto Mkubwa.

Sisi hata iweje biashara za madawa ya kulevya hapa kwetu haziwezi kufikia hata nusu ya kiwango cha madawa ya kulevya huko USA.

Kwa sasa kila anayeonekana kuunga mkono kinachoendelea kuhusu dawa za kulevya utasikia ni ccm huyo!

Sio kila mtu ni mwanasiasa, kuna watu hata habari za siasa hawataki kuzisikia hata vitambulisho vya kupigia kura walishagoma kujiandikisha.

Wapinzani nao wanaamini kazi yao ni kupinga kila kinachofanywa na serikali.
Naomba nikujibu kwa hoja hizi
-vita ya madawa ya kulevya haikuanza leo Tanzania...kwa taarifa yako na kumbukumbu zangu ilikuwa way back late 80's
-kumekuwa na majaribio kadha ya kuuzima huu mtandao Tanzania since then lakini umezidi kuimarika siku hadi siku awamu hadi awamu
-kuna list ya
watu 500 iliwahi kutolewa wakati wa Kikwete lakini haikuwahi kufanyiwa kazi....jiulize ni kwa nini
-kuna makosa mengi ya kisheria yametendeka kwenye kuwataja watuhumiwa....hapa kifuatacho ni kesi za fidia ambazo most likely watuhumiwa watashinda
-Mgawanyo wa kimadaraka haukuzingatiwa kwanini waziri wa ulinzi na mambo ya ndani wasihusishwe?
NB: kuepusha yote haya crackdown za namna hii hufanyika kwa siri sana
Kuna mengi ya kujadili hapa nitarejea ngoja niienjoy jibapa langu kwanza
 
Taarifa zenyewe za list tumeishia kuiona kwa Makonda.

Madawa yenyewe yanayoingizwa nchini usikute yanayokamatwa ni 10% ya yote yanayoingizwa.

So hakuna mwenye uhakika wa kama hao maDon wameinvest vya kutosha hapa nchini kwenye hayo majeshi Yao.
Hakika majeshi yao hayaonekani kwa macho,huwatumia hawahawa askari wetu...lakini bado nina imani kubwa na nidhamu ya majeshi yetu kulinganisha na kwingine.
 
Hakika majeshi yao hayaonekani kwa macho,huwatumia hawahawa askari wetu...lakini bado nina imani kubwa na nidhamu ya majeshi yetu kulinganisha na kwingine.
Ukiweka imani kwao na kuwaamini mia mia kwenye ishu ya mmadawa subiria mastaajabu. Hii vita yafaa kutilia shaka kila mmoja na kufanya uchunguzi wa kina kwa kila alotiliwa shaka kabla ya haya maigizo ya tv
 
Hii vita ya mkuu wa mkoa sidhani km itakuwa endelevu ingawa amefanya jambo jema


Nadhani angeunda kitengo maalum kushughulikia hili suala kwa muda mrefu
Yote Yale Yale tu vitengo vingapi vinaishia mitini tena bila taarifa wala kauli yeyote
Danganya toto
 
Hakuna anayeweza, wala atakayeweza kuitokomeza biashara hii hawa watu ni hatari ulipo wapo.
Na muda utaongea atakaa kimya muda si mrefu.
Asitoe kibanzi kwenye jicho la mwenzake hali ya kuwa kwake kuna boriti.
Kwa sababu yake pia watu wanayajua. Kama ni mkweli hasa amtaje mtoto wa....
 
Hakuna anayeweza, wala atakayeweza kuitokomeza biashara hii hawa watu ni hatari ulipo wapo.
Na muda utaongea atakaa kimya muda si mrefu.
Asitoe kibanzi kwenye jicho la mwenzake hali ya kuwa kwake kuna boriti.
Kwa sababu yake pia watu wanayajua. Kama ni mkweli hasa amtaje mtoto wa....
Mtoto wa. .....
 
Back
Top Bottom