KijanaHuru
JF-Expert Member
- Jan 7, 2017
- 1,822
- 2,290
Habari ya siku nyingi ndugu zangu, ngoja niende kwenye hoja moja kwa moja
Masuala ya ugomvi na migogoro ya ndoa kwa wazazi wetu ni mambo ambayo huwa tunakumbana nayo mara kwa mara na kwa asilimia kubwa sana japo sio kila familia au kila mtoto huweza kuyapitia haya mambo.
Ila niwape angalizo ndugu zangu katika masuala ya matatizo ya kifamilia ya wazazi usije hata siku moja ukaegemea upande wa mtu mmoja hata kidogo, kubwa unaloweza kulifanya ni kumfariji tu yule aliyeathirika zaidi kuwa na moyo mmoja wakusimama naye na kuhakikisha msongo na kukata tamaa isiwe sehemu yake.
Ukimchukia baba na akajua sababu ya mama au ukimchukia mama akajua sababu ya baba nakuhakikishia ndugu yangu nenda hata kwa mwamposa na shehe unayemjua wewe hii laana itakutafuna sana tena sana utakuwa ni mtu wa hatua mbili mbele tatu nyuma pasipo hata kuwa na suluhisho.
Narudia tena Mzazi awe na kosa au asiwe na kosa ila ukaingilia ugomvi wao ukamchukua mmoja wapo na akakufuta katika akili yake na moyo wake umekwisha kabisa.
HIli suala halina tiba yoyote zaidi ya kwenda kujiungamanisha na mzazi wako tena kabla hajaondoka hapa duniani na kama haujajifungamanisha naye akaondoka katika maisha haya hata ungekuwa mlokole wakuhamisha milima kwa maombi utahusika tu kwenda kutambika kumuomba msamaha mzazi wako.
Ndugu zangu hili suala limekaa kiroho sana namna ambayo huwezi tambua kiwepesi wepesi, laana ya kuingilia ugomvi wa wazazi na mzazi akaju umeegemea upande mmoja na akakukatia tamaa hii laana hakuna kiumbe wakuitoa chini ya jua na ulimwengu mzima zaidi ya mzazi wako,
Lasivyo itaendelea kuwasumbua hadi watoto wako pamoja na wajuu zako,
Na mara nyingi hizi laana zao zikisha kukalia wewe katika maisha hautaona la maana lolote wala hautakuwa na ahueni mahusiano yatakusumbua kama sio mahusiano basi maendeleo itakuwa shida kama sio maendeleo kipato kugumu kama sio kipato kigumu basi ipo sehemu ya muhimu kwako utakwama na hautaweza kujinasua hata kidogo,
Ukienda kuombewa na kuroga kwa waganga utapata ahueni ya mwezi mmoja tu na wala hautapata jibu la moja kwa moja hata siku moja.
Laana Hii ikikuvaa inatoka kwa njia moja tu wewe kwenda kwa mzazi wako ili arudishe moyo wako tena kwa ajili yako.
Sababu kubwa ya laana ya mzazi kuwa na nguvu nikwasababu kiroho kwa hapa duniani wazazi ndio miungu yako , wawe hai wasiwe hai wazazi wako ndio alfa na omega wako hapa duniani,
Siku nyingine nitakuja kueleza aina za laana ambazo wazazi wanaweza kukuachia,
Ukiwa na swali lolote unaweza ukauliza jisikie huru kabisa.
NASISITIZA HAKUNA MTUMISHI WALA SHEHE WALA MUNGU WALA SHETANI ANAYEWEZA KUITOA HII LAANA.
Muwe na jioni njema...!
Masuala ya ugomvi na migogoro ya ndoa kwa wazazi wetu ni mambo ambayo huwa tunakumbana nayo mara kwa mara na kwa asilimia kubwa sana japo sio kila familia au kila mtoto huweza kuyapitia haya mambo.
Ila niwape angalizo ndugu zangu katika masuala ya matatizo ya kifamilia ya wazazi usije hata siku moja ukaegemea upande wa mtu mmoja hata kidogo, kubwa unaloweza kulifanya ni kumfariji tu yule aliyeathirika zaidi kuwa na moyo mmoja wakusimama naye na kuhakikisha msongo na kukata tamaa isiwe sehemu yake.
Ukimchukia baba na akajua sababu ya mama au ukimchukia mama akajua sababu ya baba nakuhakikishia ndugu yangu nenda hata kwa mwamposa na shehe unayemjua wewe hii laana itakutafuna sana tena sana utakuwa ni mtu wa hatua mbili mbele tatu nyuma pasipo hata kuwa na suluhisho.
Narudia tena Mzazi awe na kosa au asiwe na kosa ila ukaingilia ugomvi wao ukamchukua mmoja wapo na akakufuta katika akili yake na moyo wake umekwisha kabisa.
HIli suala halina tiba yoyote zaidi ya kwenda kujiungamanisha na mzazi wako tena kabla hajaondoka hapa duniani na kama haujajifungamanisha naye akaondoka katika maisha haya hata ungekuwa mlokole wakuhamisha milima kwa maombi utahusika tu kwenda kutambika kumuomba msamaha mzazi wako.
Ndugu zangu hili suala limekaa kiroho sana namna ambayo huwezi tambua kiwepesi wepesi, laana ya kuingilia ugomvi wa wazazi na mzazi akaju umeegemea upande mmoja na akakukatia tamaa hii laana hakuna kiumbe wakuitoa chini ya jua na ulimwengu mzima zaidi ya mzazi wako,
Lasivyo itaendelea kuwasumbua hadi watoto wako pamoja na wajuu zako,
Na mara nyingi hizi laana zao zikisha kukalia wewe katika maisha hautaona la maana lolote wala hautakuwa na ahueni mahusiano yatakusumbua kama sio mahusiano basi maendeleo itakuwa shida kama sio maendeleo kipato kugumu kama sio kipato kigumu basi ipo sehemu ya muhimu kwako utakwama na hautaweza kujinasua hata kidogo,
Ukienda kuombewa na kuroga kwa waganga utapata ahueni ya mwezi mmoja tu na wala hautapata jibu la moja kwa moja hata siku moja.
Laana Hii ikikuvaa inatoka kwa njia moja tu wewe kwenda kwa mzazi wako ili arudishe moyo wako tena kwa ajili yako.
Sababu kubwa ya laana ya mzazi kuwa na nguvu nikwasababu kiroho kwa hapa duniani wazazi ndio miungu yako , wawe hai wasiwe hai wazazi wako ndio alfa na omega wako hapa duniani,
Siku nyingine nitakuja kueleza aina za laana ambazo wazazi wanaweza kukuachia,
Ukiwa na swali lolote unaweza ukauliza jisikie huru kabisa.
NASISITIZA HAKUNA MTUMISHI WALA SHEHE WALA MUNGU WALA SHETANI ANAYEWEZA KUITOA HII LAANA.
Muwe na jioni njema...!