Loading failed
JF-Expert Member
- Sep 14, 2023
- 1,945
- 5,849
Ndugu zangu
Hivi viumbe tunu ya mioyo yetu sijui akili zao zipo wapi. Japokuwa mimi ni muhanga wa kataa ndoa ila sikatai kuishi na mwanamke, nitaishi na mwanamke uchumba sugu hakika.
Hivi karibuni baada ya kupata matatizo niliona kabisa mwanamke ana umuhimu mkubwa, u-bachelor ni upumbavu na ujinga mwingi na hata kama ndoa sitaki basi niishi uchumba sugu.
Hakika nikaperuzi katika wale waliokuwa wanakula hela zangu, nikakutana ma mmoja wao aliekuwa ananijali mno, akifatilia kwa karibu maendeleo yangu, na kunitia moyo. Nikaona huyu mmoja amewazidi wenzake na kupanga kwenda kwao hata na sukari kilo kwanza nifanye namna ya kumchukua, huyu binti bila hiana alikubali ila chakushangaza nakuja kufika kwao ananiambia kapata dharura na nionane na wazazi wake. Kweli niliheshimu kwa busara nikakaa na wazazi wake na kupiga piga story fupi sana nikaaga nikaondoka maana mwenyeji wangu hayupo.
Hakika najiuliza sana moyoni kwanini anitelekeze kwa wazazi wake ilihali anajua ninaenda kwa ajili yake na kwa lengo la kusoma mazingira ili nimchukue tukaishi uchumba sugu.
Wakuu nipeni akili hapa ili nichanganye na zangu walau.
Hivi viumbe tunu ya mioyo yetu sijui akili zao zipo wapi. Japokuwa mimi ni muhanga wa kataa ndoa ila sikatai kuishi na mwanamke, nitaishi na mwanamke uchumba sugu hakika.
Hivi karibuni baada ya kupata matatizo niliona kabisa mwanamke ana umuhimu mkubwa, u-bachelor ni upumbavu na ujinga mwingi na hata kama ndoa sitaki basi niishi uchumba sugu.
Hakika nikaperuzi katika wale waliokuwa wanakula hela zangu, nikakutana ma mmoja wao aliekuwa ananijali mno, akifatilia kwa karibu maendeleo yangu, na kunitia moyo. Nikaona huyu mmoja amewazidi wenzake na kupanga kwenda kwao hata na sukari kilo kwanza nifanye namna ya kumchukua, huyu binti bila hiana alikubali ila chakushangaza nakuja kufika kwao ananiambia kapata dharura na nionane na wazazi wake. Kweli niliheshimu kwa busara nikakaa na wazazi wake na kupiga piga story fupi sana nikaaga nikaondoka maana mwenyeji wangu hayupo.
Hakika najiuliza sana moyoni kwanini anitelekeze kwa wazazi wake ilihali anajua ninaenda kwa ajili yake na kwa lengo la kusoma mazingira ili nimchukue tukaishi uchumba sugu.
Wakuu nipeni akili hapa ili nichanganye na zangu walau.