Kwenye uchumi Mzee umejifunga goli, taka usitake

Kwenye uchumi Mzee umejifunga goli, taka usitake

TumainiEl

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
7,275
Reaction score
14,315
Tunasifia mafanikio ya ujenzi wa miundombinu mikubwa ila upande wa pili unajua kabisa100% umeharibu na huenda itatuchukua miaka mingi kusimama tena.

Naipenda serikali yangu ila kwenye uchumi ndugu zangu figure hazitubebi na kama tungeweka data wazi, walahi huenda mkuu asingekaa kwenye kiti.

Sector ya ndege nina uhakika baada ya huyu, ajaye atazipiga mnada. Niaminini mimi; na hii ndio tafasiri ya "je, nikiondoka mimi wataweza?" Akimanisha kuna siri anaijua moyoni.

Mradi wa umeme huenda tukautafutia wafadhili, yani tuta-hire some of area kupinguza cost nje ya hapo Kwa umeme tuliosambaza kwa ilani za kisiasa bila kuangalia tathimini, walahi nawaambia Tanesco itakosa pesa ya kujiendesha ikizingatiwa tangu mwanzo ilishindwa kujiendesha kwa faida.

Tetesi zinasema Wakati tunapigiwa Debe ya umeme kutokatika ila tusijuwe nini kipo nyuma ya haya yote ndipo mtasikia kuna mgodi wa umeme umezimwa kwa matengenezo makubwa yatakayoigharimu serikali billion of Dollars. Haya yatatokea kwenye utawala huu mwishoni au mwanzo mwa utawala mpya, yaani 2025.

Zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi. What next? Wekeni akiba, ada itarudi ni siku chungu na za huzuni, weka akiba ya haya maneno. Hivi sasa hospi na watu havilingani. Dr vs Wahudumiwa havilingani Jiulize why. Ila zaeni, serikali ipo.

Kwanini kuna Tetesi eti miradi ya awamu ya 5 ni white elephant? Umewahi jiuliza why? Basi mimi sijui, embu tuombe uzima wachumi watatujuza, ila weka akiba.

Ajira kwa Jakaya tuliambiwa ni Boom linatesa nchi ila amini hii ajira kwa mwendo huu itatikisa taifa. Sijuwi kama unajua wahitimu ni wengi kuliko nafasi, na ilidhaniwa wakipunguza vyeti fake basi wangeajiri, wapi! Wewe, hesabu hazidanganyi.

Pray for Tz
 
Mzee maoni kama haya uwa anayaota akiwa usingizini tu aki amka ana jifanya ajui
 
Mtoa post itakua una element za ubeberu 😄😄😄
 
Ccm ni chama cha kishetani hawana tena maarifa ya kufikiria watz, wamebaki wanafikiria deals zao tu kwa sasa Kupitia kwenye haya majenzi makubwa ya kifisadi na manunuzi makubwa yasiyo na faida yoyote km ya ndege
 
Anyway kwa anayoyafanya president yanafaida mbelen .....uchumi haukui kama mchicha broo hyo ni long process😃😃
 
Wakubali wakatae! kwenye uchumi na hali ya maisha ya Watanzania kwa ujumla, Serikali ya awamu hii imefeli kwa kiwango kukubwa!

Ajira hazieleweki, maisha ya wafanyakazi yamekua ni magumu, wakulima wa korosho walidhulumiwa fedha zao, wafanyabiashara nao wanalia na kodi za kubambikiwa na TRA!
 
Me nilisha funga kakibanda kangu sitaki stress aisee corona + jiwe = kuchomoa battery kwenye gari lililo pata ajali lenye petrol lita 30,000🤔
 
Mmmmmh
Siamini Kama na wewe unaweza andika haya!
Ila kweli muda ni mwalimu mzuri, tunaanza kuongea lugha moja!
 
Nafasi
Ameua sector binafsi , hali ni mbaya . nakwambia hadi wakandarasi, manesi, mabaharia, kilimo wanaomba Ajira za walimu. Mpaka sasa waombaji ni 80,000+, jibu tosha kuwa hali ni mbaya.
zimetangazwa 13,000 ila waombaji wenye sifa wanaweza kufikia 130,000.Hapo sifahamu watatumia mbinu ya kuwauliza vyama vyao,ukiwa CCM upewe bali ukiwa siyo unarukwa.Haya ni majanga kwa wahitimu.
 
Nafasi

zimetangazwa 13,000 ila waombaji wenye sifa wanaweza kufikia 130,000.Hapo sifahamu watatumia mbinu ya kuwauliza vyama vyao,ukiwa CCM upewe bali ukiwa siyo unarukwa.Haya ni majanga kwa wahitimu.
Kazi kweli kweli.
 
Back
Top Bottom