Kwenu mawifi, wake wa kaka zetu

Kwenu mawifi, wake wa kaka zetu

Ukiwa na mawifi waswahili wasio na kazi, kazi kupiga umbea tu na kufuatilia maisha ya wifi yao na kaka yao basi wafwaaaa!!!

Kaka yako akishaoa utambue majukumu yameongezeka kwake na ana kazi ya kujenga kwake pia, mtasaidiwa lakini kama mnavyotaka, bali kwa nafasi inayopatikana. Mkishatambua hilo basi walaa hakuna taabu. Kuna mawifi hawana jema, hata ufanyeje wataongea, weka nta masikioni fanya yaliyo ya msingi.
Mmh jamani, imbombo jilipo
 
Ndugu relux then uliza maswali ya msingi
Nimekuuliza hayo maswali ILI MASWALI NA MAJIBU YAKE WANAWAKE WAOTE WAYASOME .... HALAFU WAJUE KWAMBA KILA MWANAMKE ANA PANDE MBILI.... Mmoja yeye ni WIFI kwa walioolewa na kaka zake (yake) na vile vile yeye ni Wifi kwa dada wa mumewe... HIVYO MALALAMIKO YOTE HAYO YANATOKA KWA MWANAMKE KWENDA KWA MWANAMKE....
 
Tatizo nyie mawifi zetu...

Kabla hamjaolewa...mnakuja tunawafahamu

Mnaonyesha upendo kumbe wa uongo

Mnafua

Mnapika

Mnashiriki kazi kupita kiasi

Mnamhudumia mama mkwe hadi anakuombea heri

Mkiolewa mnageuka miba

Kwa nini baadhi yenu ni miba kwenye familia mnazowakuta???

Hatuwakatazi kuvaa kunywa ni nyumba yako na mumeo

Tunahitaji ule upendo wa mwanzo uendelee

Baadhi yenu mnaingia kwenye familia kwa kujihami na attitudes

Vibaya hivyo
Ulishawahi ona mgombea anaomba tena kura baada ya uchaguzi? Subiri ukafanye hivyo utakakoolewa.

Baada ya ndoa majukumu yake kwa familia yake yanaanza kwahiyo anakuwa anachoka, akija kwenu kaja likizo jamani sio mumgeuze house girl ebo!!! Hebu mumpetipeti wifi yenu sio kumtumikisha aamke saa10 yeye kuku?
 
Tehe tehe kumekucha.....kuna hii keshfa .....eti mawifi wanawatafutia kaka zao side chicks kuwakomoa mke wa kaka yake....!!!!!!!! Aiseeee hiyo nimepewa live sasa hivi na mke mkereketwa.
 
Ulishawahi ona mgombea anaomba tena kura baada ya kampeni? Subiri ukafanye hivyo utakakoolewa.

Baada ya ndoa majikumu yake kwa familia yake yanaanza kwahiyo anakuwa anachoka, akija kwenu kaja likizo jamani sio mumgeuze house girl ebo!!! Hebu mumpetipeti wifi yenu sio kumtumikisha aamke saa10 yeye kuku?
Haha me hata kampeni sipigi wallah
 
Haha me hata kampeni sipigi wallah
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hizo habari za kuniamsha saa10 hapana jamani, nitaamka muda wangu wa kawaida na nitafanya shughuli kwa nafasi, sio mawifi wamenyoosha miguu mie busy kutoka jasho. Wakinyoosha tunanyoosha wote tusogoe vizuri[emoji85] [emoji85] [emoji85]
 
Back
Top Bottom