Kweli Waafrika Ndivyo Tulivyo - We Aint 'Capitalist Niggers'!

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,604
1,704
Baada ya kufikiria kwa kina nimegundua kumbe ni kweli waafrika ndivyo tulivyo. Pamoja na jitihada zote za Chika Onyeani, Mtunzi wa Capitalist Nigger (Bepari Jeusi) kujaribu kutusaidia tuwe na tabia hizo za 'kukata shingo' (cut-throat) za Kibepari ili tupate maendeleo ya kibepari kama Ulaya na Marikani tumeshindwa na tunazidi kushindwa. Kwa nini? Kwa sababu sisi sio Wabepari. HIyo sio asili yetu. Naam ndio tulivyo - Wajamaa!
 
How do u defend ur statement kuwa sio asili yetu? Sisi tumei-practice muda gani, na hizo nchi nyingine nazo zime-practice muda gani?
 
How do u defend ur statement kuwa sio asili yetu? Sisi tumei-practice muda gani, na hizo nchi nyingine nazo zime-practice muda gani?

Tume practice mda wote kama wao walibyo practice lakini tumeshindwa !! tofauti yao na yetu ni takrabani miaka mia hivi 1884-1960. kwa mda huu tu ndio tulipractice na wao .Nafikiri japo sina uhakika ndani ya miaka hiyo AFrika ndio ilikuwa na maendeleo kuliko wakati wowote.
 
How do u defend ur statement kuwa sio asili yetu? Sisi tumei-practice muda gani, na hizo nchi nyingine nazo zime-practice muda gani?

Hata u-practice miaka milioni 100 kitu ambacho sio asili yako hakitageuka asili yako - waulize Wahaiti ambao ni Waafrika/Weusi wenzetu waliopata uhuru miaka 300 iliyopita! Kwa ufupi hakuna haja ya kujihangaisha ku-practice kitu ambacho sio asili yetu. Let us just stick to what is in our nature i.e. Ujamaa by adapting it to the contemporary setting, that is, by moving toward Ujamaa Mamboleo!
 
Hata u-practice miaka milioni 100 kitu ambacho sio asili yako hakitageuka asili yako - waulize Wahaiti ambao ni Waafrika/Weusi wenzetu waliopata uhuru miaka 300 iliyopita! Kwa ufupi hakuna haja ya kujihangaisha ku-practice kitu ambacho sio asili yetu. Let us just stick to what is in our nature i.e. Ujamaa by adapting it to the contemporary setting, that is, by moving toward Ujamaa Mamboleo!

Toa mfano wa jamii yoyote ya Kiafrika au yenye asili ya Afrika ambayo ina practice au ambayo imewahi ku practice ujamaa na kupata maendeleo ya hali ya juu.

NB: I'm loving this topic coz it's right up my alley...wooo hoooo
 
Toa mfano wa jamii yoyote ya Kiafrika au yenye asili ya Afrika ambayo ina practice au ambayo imewahi ku practice ujamaa na kupata maendeleo ya hali ya juu.

NB: I'm loving this topic coz it's right up my alley...wooo hoooo

Hata ukiachana na ujamaa
Kile kitendo tu cha kuiba fedha na kwenda kuzificha nchi nyingine ama kujenga mijumba nchi zingine hasa za ulaya wakati mhusika hanafamilia huko nako pia kunahitaji kufanyiwa tafiti.? ya kuthibitisha ndivyo tulivyo.
 
Hata ukiachana na ujamaa
Kile kitendo tu cha kuiba fedha na kwenda kuzificha nchi nyingine ama kujenga mijumba nchi zingine hasa za ulaya wakati mhusika hanafamilia huko nako pia kunahitaji kufanyiwa tafiti.? ya kuthibitisha ndivyo tulivyo.

Unajua nini mtu wangu? Hoja ya Ndivyo Tulivyo wala haihitaji nguvu wala akili nyingi kuitetea. Unachohitaji ni macho na masikio tu. Nenda bara Afrika kusini mwa jangwa la sahara halafu angalia 'observe' tu mifanano 'similarities' ya maisha na kijamii. Utagundua kuwa hakuna tofauti kubwa sana. Sasa unadhani hii ni ajali tu?
 
More salt to the non-healing African wound!!

But is it denial, acceptance or just a mere acknowledgement?!
 
Tanzania ipo wapi sasa, Katiba yetu ya ujamaa lakini mambo yetu ya kibepari. sasa tupo wapi na ndio maana leo watu wamelewa madaraka
 
Baada ya kufikiria kwa kina nimegundua kumbe ni kweli waafrika ndivyo tulivyo. Pamoja na jitihada zote za Chika Onyeani, Mtunzi wa Capitalist Nigger (Bepari Jeusi) kujaribu kutusaidia tuwe na tabia hizo za 'kukata shingo' (cut-throat) za Kibepari ili tupate maendeleo ya kibepari kama Ulaya na Marikani tumeshindwa na tunazidi kushindwa. Kwa nini? Kwa sababu sisi sio Wabepari. HIyo sio asili yetu. Naam ndio tulivyo - Wajamaa!

Mkuu naomba niuliza ili nielewe vizuri. Unasema sisi siyo wabepari asili yetu ni ujamaa? Tanganyika ilikuwa ina tawaliwa na machief ambao walikuwa na nguvu isiyo pingika na wananchi kwa maana hiyo mfumo ulikuwa wa kifalme zaidi na si ujamaa, tofauti na nchi zingine zenye wafalme ni kwamba hatukuwa na mtu mmoja kutawala nchi nzima bali utawala ulikuwa wa kikabila. Zanzibar napo hivyo hivyo walikuwa na Sultan kitu ambacho si ujamaa. Sasa unaposema asili yetu ujamaa una maanisha nini? Kama sija kuelewa naomba unieleweshe mkuu.
 
Wakuu,
Naona tunaelekea kuzuri....Mwanzo mzuri wa fikra endelezi unaaza hapa JF!
shukran sana Companero kwa kuaznisha mada hii..
 
Kwanini hizi mada zimeunganishwa? Au ndio tulivyo? Hii mada ilikuwa ni mpya kabisa na ingeruhusiwa kuendelea pekee yake.
 
I have come to realise, the only problem with afrikans is implementation and maintenance
 
Mkuu naomba niuliza ili nielewe vizuri. Unasema sisi siyo wabepari asili yetu ni ujamaa? Tanganyika ilikuwa ina tawaliwa na machief ambao walikuwa na nguvu isiyo pingika na wananchi kwa maana hiyo mfumo ulikuwa wa kifalme zaidi na si ujamaa, tofauti na nchi zingine zenye wafalme ni kwamba hatukuwa na mtu mmoja kutawala nchi nzima bali utawala ulikuwa wa kikabila. Zanzibar napo hivyo hivyo walikuwa na Sultan kitu ambacho si ujamaa. Sasa unaposema asili yetu ujamaa una maanisha nini? Kama sija kuelewa naomba unieleweshe mkuu.

Hiyo historia umeisoma wapi? Iliandikwa na nani? Inafundishwa na nani?

Soma Long Walk to Freedom cha Nelson Mandela uone machifu wa Kixhosa walivyokuwa wanadhibitiwa katika Mbongi (Baraza). Pia soma Citizens and Subjects cha Mahmood Mamdani uone jinsi Ukoloni ulivyosimika mfumo wa Machifu wenye hizo nguvu zisizopingika unazoziongelea. Pia msikilize George Ayittey, mtunzi wa Africa Unchained, katika Mhadhara wake wake wa TED alioutoa Arusha - hasa sikiliza uchambuzi wake wa jinsi jamii za Kiafrika zilivyokuwa zimegatua madaraka (decentralize power). Ukimaliza nenda kaongea na mabibi na mababu wanaokumbuka historia waliyoelezwa na babu na bibi zao kuhusu utawala wa Kiafrika kabla ya kuja kwa Mkoloni.
 
Hiyo historia umeisoma wapi? Iliandikwa na nani? Inafundishwa na nani?

Soma Long Walk to Freedom cha Nelson Mandela uone machifu wa Kixhosa walivyokuwa wanadhibitiwa katika Mbongi (Baraza). Pia soma Citizens and Subjects cha Mahmood Mamdani uone jinsi Ukoloni ulivyosimika mfumo wa Machifu wenye hizo nguvu zisizopingika unazoziongelea. Pia msikilize George Ayittey, mtunzi wa Africa Unchained, katika Mhadhara wake wake wa TED alioutoa Arusha - hasa sikiliza uchambuzi wake wa jinsi jamii za Kiafrika zilivyokuwa zimegatua madaraka (decentralize power). Ukimaliza nenda kaongea na mabibi na mababu wanaokumbuka historia waliyoelezwa na babu na bibi zao kuhusu utawala wa Kiafrika kabla ya kuja kwa Mkoloni.

George Ayittey is an acerbic angry black man...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom