Hesabu rahisi zinaonyesha toka uchaguzi mkuu Oct 31, 2010 mapa leo ni siku 117 na mikoa kama Geita, Katavi, Njombe, Simiyu, Dar to mention a few haina wakuu wa mikoa na inaendelea salama.
Ili kupunguza matumizi ya kodi zetu, kuna haja kweli ya kuendelea na kada hii?
Nadhani ni muda mwafaka wa kuangalia ni jinsi gani tunajitawala na kujiletea maendeleo!
Ili kupunguza matumizi ya kodi zetu, kuna haja kweli ya kuendelea na kada hii?
Nadhani ni muda mwafaka wa kuangalia ni jinsi gani tunajitawala na kujiletea maendeleo!
Na Reginald Miruko, Mwananchi (email the author)
Alhamisi, Aprili 18, 2013
Dodoma. Serikali ya Chama cha Mapinduzi haitaachana na mfumo wa uongozi unaowatumia wakuu wa mikoa na wilaya, kwa sababu nafasi hizo ni muhimu katika kutawanya madaraka ya Rais.
Hayo yalielezwa bungeni juzi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia wakati akijibu hoja za wabunge kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Ghasia alisema CCM inayotawala inaona mfumo huo ni muhimu, labda iwapo watu wengine wanaoupinga wakishika madaraka wanaweza kuuondoa, jambo ambalo hata hivyo hadhani kama linaweza kutokea.
Vilevile Ghasia alisema watumishi kadhaa wa halmashauri ya Wilaya ya Mbarali wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi wamechukuliwa hatua mbalimbali za kisheria na nidhamu.
Alisema aliyekuwa mkurugenzi mtendaji suala lake limefikishwa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), mweka hazina amefukuzwa kazi na Ofisa Mipango amepewa onyo kali.
Kuhusu maombi ya wabunge wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu (Temeke) na Idd Azzan (Kinondoni) waliotaka mkoa huo ugawanywe na kupata wilaya zaidi, Ghasia alisema suala hilo linapaswa lianzie kwa wananchi wenyewe na Serikali italifanyia kazi.
Chadema kimekuwa kikipinga kuwapo kwa wakuu wa mikoa na wilaya kwa sababu hawatumikii wananchi zaidi ya mamlaka (Rais) iliyowaweka.
Awali, wakuu wa wilaya hawakuwamo kwenye Katiba, lakini baada ya suala hilo kuibuliwa na Mbowe, Serikali iliamua kufanya mabadiliko na kuwaingiza kutambulika kikatiba.