Kweli Lowassa na RA wana nguvu

Kweli Lowassa na RA wana nguvu

viongozi wangekua na uzalendo na nchi tusingekua hapa tulipo,hayo mnayoyafanya mnadhani 2015 mtawaambia nini wananchi waliowapa nafasi?
hata wale viongozi ambao kwa kiasi kikubwa wtz waliona kuwa wana mwelekeo nao hawana maana kitendo cha cdm kufunga ndoa na rachel kinatia aibu
 
kufanya kosa haimanishi na wewe ufanye kosa kitendo cha cdm kujeuka kuwa vuvuzela wa rachel ni aibu na i can assure that wtz wataelewa hii ndoa yenu na rachel na ndio tutakuwa tunaongelea kwamba zamani cdm ilikuwa na nguvu

Wewe waache wawachekee halafu 2015 wenzao wauze chama halafu wawaache njia panda. Cdm imeshaingiliwa na mdudu na anashambulia ghala na wenye ghala wanabaki kumsifia mtunza ghala. Subiri walie!
 
Nitazidi kum-blame Nape kwa mwendo alioanza nao, he had no positive tactics za kudili na hao watu. They are capable, intelligent, wealthy, well organised, powerfull, very strong-political wise, decissive & visionery.
Although Nape is young and energetic...muda wake bado wa kuwayumbisha au kuwanyooshea vidole hao wababe, wanamihimili almost ktk kila tasisi ya dola ya nchini mwetu.

EL the president of TZ under CCM, RA the Prime Minister of TZ under CCM. JK is serving their interests. JK and CCM without EL and RA will never breath a second!
 
Sasa kwa mfano mimi Nape huwa nakataa hoja zake zisizo natija,ubunifu wala tafiti.Je,hapo mafisadi watakuwa wamehusika vipi?Hebu tajaribu kuleta posts zenye arguments nzito.Tuache ku-base katika hoja nyepesi na Ramli
 
Sasa kwa mfano mimi Nape huwa nakataa hoja zake zisizo natija,ubunifu wala tafiti.Je,hapo mafisadi watakuwa wamehusika vipi?Hebu tajaribu kuleta posts zenye arguments nzito.Tuache ku-base katika hoja nyepesi na Ramli
Tumeamua kuwapuuza hao wanaolipwa kwa kazi za kuuza utu wao humu.zinapokuja habari za uchafu wa ccm huwa tunaushaidi na sio huo upuuzi.alafu angalia walivyojazana utajua tu wameambiana kuchangia this is too low jamani ficheni ukiazi wenu basi kidogo
 
Wewe waache wawachekee halafu 2015 wenzao wauze chama halafu wawaache njia panda. Cdm imeshaingiliwa na mdudu na anashambulia ghala na wenye ghala wanabaki kumsifia mtunza ghala. Subiri walie!
Nape hajui atendalo kama wanampango wa kuwafuka RACHEL wanasubiri nini? Kwanza huyo nape amewahi kuwataja hadharani hao mafisadi?juzi katibu wenu si kasema hafukuzwi mtu? Nape amekana hilo?wezi mnawajua mnawapa cku 90! Kama si usanii ni nini?
 
mkama p umetumwa na hutashinda kwakuwa unashindana na haki.hapo umeona utateka watu kwa mbinu kama hizi! Sisi tunalipua tu.
 
mkama p umetumwa na hutashinda kwakuwa unashindana na haki.hapo umeona utateka watu kwa mbinu kama hizi! Sisi tunalipua tu.

Ujadili hoja ukiona haina mashiko pitiliza.
 
Sasa kama ccm mmewagwaya mara muwape siku 90 ghafla mkahairisha..na hapo mna jesh,mahakama,polis,mgambo, magamba, mabomu sa si tufanyaje jaman..mafisadi na ccm ni sawa samak na maji..
 
Chadema wamewatajia...sasa malizien mnashndwa,. Mnataka kila kitu mfanyiwe...
 
Wewe huoni mlivyotekwa nao hata hapa jf, mnashambulia Nape badala ya RA na kundi lake.
Naaw!Hiyo vita ya ndani ni ya mafisadi vs mafisadi.Ni wanaotaka kula vs waliovimbiwa.Kwa upande mwingine,maadui wa nje ie upinzani,hajui namna ya kuwahandle.Ameonyesha udhaifu kwa kujikita kwenye siasa za ubaguzi ambazo hazilipi...Tatizo ni yeye na wala si JF.
 
Mkuu heshima kwako. Hili jambo mimi limekuwa likinishangaza kwa muda mrefu maana toka harakati hizi za kuwataka RACHEL wajiondoe, wale wasanifu wa orodha ya mafisadi walibaki kimya na hawakusika mpaka walipokuja na orodha ya Tabora na kuanza kuponda harakati hizo. Lakini hata sasa ukiangalia mikutano yao, hoja hii huisikii wakiisema kabisa na sasa mkakati waliokuja nao ni kumshambulia Nape ili ama kumtisha au kumkatisha tamaa asiendelee. Haya yalianza na magazeti ya Habari Corporation na Tanzania Daima. Magazeti yalipotulia wamekuja Chadema na Mtikila na sasa huo ndiyo wimbo. Sasa tumeelewa kwa nini nchi hii haina mtetezi maana kama hawa nao wananunuliwa na vipande thelathini, tena kirahisi basi hakuna aliyebaki. Hawa nao ni mafisadi kwa sababu ni beneficiaries wa proceeds za ufisadi lakini pia ni accessories after the fact maana wanasaidia kuhakiksha kwamba watanzania hawapati haki yao. Shame on Chadema!
Wakuu tumieni common sense sometimes.Huwezi kuona kuwa cdm would like to see that Rachels stays within ccm as much as they would like them to leave chama cha mapinduzi?Kama wakiondoka,ina maana ccm itarudisha imani kubwa sana kwa wananchi na watajiunga na ccm kwa kasi.Its a give and take kind of situation for cdm.Yani cdm wanaweza kupoteza wanachama kwa mafisadi hao kujiondoa ccm licha ya kwamba nia ni kuzuia mafisadi wasiendelee kulitafuna Taifa.
Na hilo la kuwataja wengine ndani ya ccm ni kama tactic tu ili kwamba hata kama hao Rachel wakiondoka,impact yake isiwe kubwa sana kwasababu ina maana itabidi wajivue magamba mengine.Ni tahadhari kwamba magambaz is everywhere in ccm....Kwamba hata mkiwafukuza hao Rachels haina maana kwamba mmekuwa safi.Simple,hayo mengine ni blah bla zenu tu za kisiasa.
 
Nakubaliana na wewe mkuu kwa asilimia 100. Tatizo ni kwamba wafuasi wao hawajui kwamba kuna hii ndoa iliyofungwa kati ya mafisadi na viongozi wao na kwa kiasi kikubwa sana, kuendelea kubaki kwao katika nafasi zao kutategemea namna Chadema watakavyoendelea kutoa msaada kwao.

Suala la kuja naorodha mpya ya mafisadi iliratibiwa na kutekelezwa na Rostam na alipoitayarisha orodha hiyo, ambayo ilikuwa imeandikwa kwa mkono wake mwenyewe (hand written) ndipo akapewa mfanyakazi wake anayeitwa Balati Goda na kumkimbizia Marando ambaye alikuwa akisubiri ndege iliyokodiwa na mafisadi hao Terminal 1 (uwanja wa zamani wa ndege) na kuelekea Tabora ambako ndiko ilikosomwa na Dr. Slaa. Hata gharama za kukodi ndege na gharama zote zilizotumika kuwanunua viongozi hao zinafahamika na wakati ukifika kila kitu kitawekwa wazi.

Chadema wanatakiwa kuelewa kwamba viongozi wao ndiyo wanaotumika kuendelea kuwafanya mafisadi waendelee kupumua na orodha hiyo mpya ilitolewa mahsusi kwa sababu mbili. Moja ni kuwachanganya wananchi ili waache kujadili kuondolewa kwao mafisadi hao baada ya azimio la Dodoma, lakini vile vile kutaka kuchafua watu wengine ili hatimaye ionekane kwamba hao nao wanatakiwa kuchukuliwa hatua au ikibidi wote waachwe. Watu wanafahamu kwamba ndoa hii ya mafisadi na Chadema imeanza muda mrefu na hata sasa mfano ulio hai ni jinsi gazeti la Tanzania Daima linavyotumiwa kama mdomo wa mafisadi na hata jinsi Absalom Kibanda anavyotumika na uhusika wake katika kuanzisha jarida la Umoja ambalo mmiliki au mfadhili wake mkuu ni Lowassa. Tunafahamu pia kwamba hata orodha ya Mwembe Yanga ilifanyiwa usanii na Rostam kwa kuongeza jina la Rais (tena kwa mkono) na Slaa akaenda kuisoma hivyo hivyo Mwembe Yanga.
The only way nitabadili mawazo kama nilivyoainisha kwenye bandiko langu lililopita,ni kama hayo niliyo ya highlight ni kweli.Nachelea kusema ni dirty politics...Yani kuna watu humu wamekuamini unaposema kwamba RA aliandika orodha zote za mafisadi?Huu ni uongo ambao ni very cheap.
 
CCM BANA WALE WANACHAMA SI WENU? KINAWASHINDA NN KUWAFUKUZA? au mlitaka chadema waje wawafukuzie? Achaneni ni mbinu ya miaka 47, hatumbumbaziki kirahis hvo..
 
Baada ya Nape kuwagusa mafisadi, sasa Nape anashambuliwa kama mpira wa kona, kutoka kila pande. Kwenye magazeti hadi mitandaoni. Ni kweli mafisadi hawagusiki, gusa uone.

Nimekua nasoma maoni yako,siamini kama unachukia ufisadi kwa ujumla wake. Mimi naona una chuki zako binafsi kwa akina Rachel. Maana naona kwako ww hao wakiondoka CCM basi unaona chama chako kitakua kimejisafisha. Tatizo la rushwa ktk CCM,serikali na jamii yetu kwa ujumla ni kubwa sana. Tuache kuwanyooshea vidole watu watatu eti hao wakichukuliwa hatua,mambo yetu yatakua sawa. Usipumbazwe na makundi yanayohujumiana na kuchafuana ndani ya chama chako kikongwe ktk kutafuta urais 2015.
 
EL the president of TZ under CCM, RA the Prime Minister of TZ under CCM. JK is serving their interests. JK and CCM without EL and RA will never breath a second!

You are entitled to your opinion, but you couldn't be more myopic.
 
Nimekua nasoma maoni yako,siamini kama unachukia ufisadi kwa ujumla wake. Mimi naona una chuki zako binafsi kwa akina Rachel. Maana naona kwako ww hao wakiondoka CCM basi unaona chama chako kitakua kimejisafisha. Tatizo la rushwa ktk CCM,serikali na jamii yetu kwa ujumla ni kubwa sana. Tuache kuwanyooshea vidole watu watatu eti hao wakichukuliwa hatua,mambo yetu yatakua sawa. Usipumbazwe na makundi yanayohujumiana na kuchafuana ndani ya chama chako kikongwe ktk kutafuta urais 2015.

Ni lazima uelewe kwamba katika kila jambo kuna vinara au ring leaders. Hawa watatu ndiyo mizizi ya rushwa na utawala mbaya katika miongo hii miwili. Mafisadi wengine tuanowasikia na kuwaona na mawakala na makuwadi wa hawa jamaa. Mimi nakubali kwamba hawa watatu wakiwa neutralized basi asilimia 75 ya tatizo litakuwa limetatuliwa na hawa kupe wengine watakufa baada ya ng'ombe kuchinjwa.
 
The only way nitabadili mawazo kama nilivyoainisha kwenye bandiko langu lililopita,ni kama hayo niliyo ya highlight ni kweli.Nachelea kusema ni dirty politics...Yani kuna watu humu wamekuamini unaposema kwamba RA aliandika orodha zote za mafisadi?Huu ni uongo ambao ni very cheap.

Hulazimiki kuamini hayo hasa kwa vile wewe una hulka ya u-Tomaso na kwa vile hutaki kuwashushia hadhi viongozi wako unaowaabudu sana. Lakini kwa wanaojua watakwambia kwamba hao miungu wako sasa ni manamba wa mafisadi tu!
 
Nimekua nasoma maoni yako,siamini kama unachukia ufisadi kwa ujumla wake. Mimi naona una chuki zako binafsi kwa akina Rachel. Maana naona kwako ww hao wakiondoka CCM basi unaona chama chako kitakua kimejisafisha. Tatizo la rushwa ktk CCM,serikali na jamii yetu kwa ujumla ni kubwa sana. Tuache kuwanyooshea vidole watu watatu eti hao wakichukuliwa hatua,mambo yetu yatakua sawa. Usipumbazwe na makundi yanayohujumiana na kuchafuana ndani ya chama chako kikongwe ktk kutafuta urais 2015.

Je ni kweli baada ya kuwagusa anashambuliwa kama mpira wa kona?
 
Back
Top Bottom