Mwanaume rijali mtu wa miraba minne km Mwana Mtoka Pabaya kamwe hawezi kujidhalilisha kupita mtaa hadi mtaa na kadi za michango akiomba fedha kwa mwanaume wenzake.
Tabia mbaya sana ya kukosa aibu
Bora umesema wenzako na wewe, waache wenye nazo wafanye wee unakereka nini? Ni siku haitajirudia kamwe wacha waenjoy to the fullest
Huwa najiuliza mwisho wake lini Watanzania wa hali ya kati na chini kimaisha, hasa mijini, wataachana na ulimbukeni wa kufanya gharama kubwa za harusi?
Tukio ambalo linachukua mamilioni halafu linafanyika within few hrs watu wanakula wanakunywa wanaondoka, bajeti ya milioni 9 baada ya honey moon maharusi wanayaanza maisha kwa taabu kulipa madeni n.k., kwanini Watanzania hatubadiliki?
Wazungu miaka ya nyuma walishapita humu wakabadilika miaka mingi ilopita karne hii wakihudhuria harusi zetu wanatushangaa na kutuona ni matajiri sana kumbe hamna kitu!
Kweli hatukatai wapo wanaojiweza kifedha wacha wafanye, lakini wenzangu na miye unajikamua unafanya sherehe kubwa na mnaendelea katika circle ya kuchangiana the whole year unajikuta unachangia harusi tu, sijui kama kuna wanaopiga hesabu ya hizo kadi familia iliochanga kwa mwaka na si kana kwamba ina mwisho, no, na mwaka ujao hivyo hivyo.
Tuamke Watanzania, tufanye harusi za gharama ndogo, kama ni swala la kuchangishana basi tuchangishane ada-fees-watoto wakasome vyuoni Malaysia, London na US, matunda yatakuja onekana. Wakenya wenzetu waliliona hili mapema, leo wengi ni maboss ktk nchi yetu wenyewe!
Tubadilike Watanzania! Harusi nacho ni chanzo cha kutiana umasikini!
Kwa hiyo unafanya mwenyewe?
mimi nilishasema kabisa, kikubwa ni ndoa tu. ila msosi watu watakula ubwabwa hata kilo 200 na nyama na soda baaaaas kwisha, hata mil 1 haizidi kulisha watu wakashiba mpunga wakaenda zao, ila tarumbeta send off, kitchen part na utumbo mwingine NO!
na kwa nilivojaribu kufanya utafiti wangu kwa ndoa zilizofanya harusi za matarumbeta na mbembwe nyingi hua zina migogoro sana, ila ndoa za kimaskini nyingi naona zina dumu sana, sijui ni kwa nini
Bora umesema wenzako na wewe, waache wenye nazo wafanye wee unakereka nini? Ni siku haitajirudia kamwe wacha waenjoy to the fullest
Feminine way of asking questions. YES, hata wewe unapaswa kufanya mwenyewe. Kitu cha kufanya kwa michango ya watu ni kama msiba au nyumba yako ikiezuliwa na kimbunga sababu hayo huna ghafla pasipo kuyatarajia.
Km swali lako lililenga kunikejeli wala sitajali, jamii yetu imejaa watu wasiotaka kufikiri.
Kujaza watu wasiokufahamu kwenye sherehe yako ya ndoa, kukodi ukumbi, magari ya kifahari na pilikapilika zingine ambazo zisizo na lazima havimzuii mwanaume **** ujauzito mke wake.
Ndoa ndio ya lazima, harusi jipime uwezo
Michango ya harusi wanawake ndani ya nyumba hugeuka maajent. Kila siku swali kwa mume ni kuulizwa kama mchango kwa fulani umeshalipa. Kina mama nia kubwa ni kwenda kuoneshana vito na mavazi! Na gharama zipo kwenye muda wa vikao, nauli na zawadi. Kwa mwaka familia zetu hutumia hela nyingi kwa harusi huku tuko nyumba za kupanga.
Kwaiyo kama mtu ana uwezo unataka asiji enjoy? Msio na uwezo jikuneni mkono unakofika
Wanaongelea michango ya harusi ,mbona una kichwa kigumu ! kama una uwezo inakuhusu nini?