Kweli hali ya pesa ni ngumu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,638
Reaction score
220,410
Kuna kiwanja cha jirani yangu kiko wazi. Nilimuuliza malengo yake aliniambia kwa kweli tangu mzee wake aondoke duniani ramani yake haisomeki. Mzee alikua Don serikalini. Nilimgusia kama anaweza kuniuzia hiyo ilikua 2012 aliniambia nimpe milioni 60. Mume wangu aliniambia kwa bei hiyo achana nae.

Juzi amenitumia ujumbe tukutane tuongee. Tulipokutana anasema yuko tayari kwa milioni 3 tuamdikishiane anipe kiwanja. Hapa nilipo sijaamini nilichokisikia.
 
Chukuaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niuzie mimi kwa million 4
 
Umekula bingo bi dada
 
Changamoto kubwa ilikuwa ni miradhi kwani watoto wote walikua wanamtegemea dingi. Lakini alikabidhiwa yeye akiwa mtoto mkubwa wa kiume.
Kama cha familia nakushauri achana nacho...hiyo M3 yako ni kubwa sana nina madhara ya kununua vitu vya familia hasa mambo hayo. Ukiweza nenda nae RITA ama mahakamani mirathi ina mambo sana. Nashauri tu pesa ni yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu uko sahihi zaidi. nmewahi kununua shamba kikaniletea dhahama kama hzo ila mwisho wa siku nlikipata, na kufidiwa gharama zangu za usumbufu, since then nko makini sana!
 
Changamoto kubwa ilikuwa ni miradhi kwani watoto wote walikua wanamtegemea dingi. Lakini alikabidhiwa yeye akiwa mtoto mkubwa wa kiume.
Achana nacho hicho. Kitakuletea kesi au mara ujenge ukute nyumba hailaliki. Tafuta kiwanja ambacho kiko clean like a whistle hata kama ni huku kwetu Mwanagati. Sio lazima ukae Ilala
Kibamba kuna viwanja vya mkopo. Unalipia milioni unusu zilizobaki utalipa baada ya miaka 2.
 
Temana nacho da mkubwa, juzi kati hapa nimeshuhudia nyumba zikivunjwa maeneo ya Olasiti Arusha mambo ya mirathi tena kwa wamasai ambao wao kwa mila yao mwanamke harithi kitu ila alishinda dada kesi na wote waiokuwa wameuziwa na kujenga mabungalow yao palivunjwa kama masihara watu walikua wanazimia kama mbu waliopuliziwa HIT ⚡
 
Alkasusi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…