Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi

Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi

unalaani kama nani,ucpanic bibie mwenye kulaani ni yule Aliye2umba!tena yeye ka2kumbusha 2waheshimu wazazi!...wewe unaleta ujenda wako hp,kwan mzaz ni mama2?baba sio mzazi ee!.Futa hyo kauli ndg

Hebu nipishe usiniparamie kwa mbele mie nikatapika bure.....
........ Kama imekuuma chukua kunywa maji unyamaze!!!!!!!!!!
 
  • Thanks
Reactions: ram
Majaribu2013 aje hapa awaombe radhi dada/mama/watoto na shangazi zetu. Binafsi sikufurahishwa na yaliyoandikwa katika ile habari!
 
Last edited by a moderator:
Nimesikitishwa sana hadi nimetoa machozi kwa hiki kilichokuwa kinaendelea kwenye uzi wa Wanawake wanajiuza.

Wanaume mnataka nini? Mmekosa hata staha kwa hao wachache mnaowajali mkabaki mnashabikia haya. Najua watakuwepo wa rika mbali mbali na mmeonyesha ushirikiano mzuri kweli. Mmeona mnayowafanyia humo vyumbani haitoshi mpaka mje kuanika u.p.u.m.b.a.f.u wenu hapa.
Haikutosha kutoa fedheha hizi kwenye vijiwe vyenu ambavyo sisi hatupo mkatuhabarisha na kutuweka katika madaraja.

Kuna mwanamke anakuwepo kwenye vikao vya kupanga mahari?
Kuna mwanamke anapenda yaliyomkuta yeye yamkute na bintiye?
Kuna kahaba anayefundisha mwanae wa kike kazi?
Ni wanawake wangapi wanalea watoto bila baba zao?
Wanajiuza ehh?

Mnatutukana nyumbani, vijiweni na humu pia.
Mnaendelea kushirikiana kudhalilisha utu wa wanawake.
Eti wanawake wanajiuza!

Si ni nyie kwa u.m.a.l.a.y.a wenu mnaoenda mnatafuta mabikra wachanga na kuwahadaa na vijimali vyenu, leo hawawezi sahau siku waliyotoa utu wao kwa wanaume waliodhani wanaheshimu. Mnasimama kusema wanajiuza.

Si ni nyie mmewazalisha wake zenu,mkisisitiza watoto waitwe kwa majina yenu hamjali familia zenu mnaondoka mnapeleka pesa kwa makahaba wawafanyie mnayotaka. Leo mnasema wanawake wanajiuza.

Si ni nyie mnaozalisha mabinti wa watu kwa hila za ahadi za ndoa halafu mnatelekeza watoto, mnadai siyo “wife material”. Kabla alikuwa malkia huyu, leo anajiuza.

Si ni nyie mnaita wake zenu m.a.l.a.y.a na pengine kuwapiga ngumi mkijificha kwenye sura ya “kichwa cha familia” halafu baadaye mkiwaletea watoto wa matunda ya ufuska wenu mkitaka wawalee, leo mnasema wanajiuza.

Si ni nyie mlio maofisini na vyuoni mnawajaribu wanawake waliobahatika kusoma mkitaka mlale nao ndo mwape stahili yao. Hao nao hujiuza!

Si ni nyie mnaogongana na watoto wenu mkishindana kuwatumia “mahousegirl” kama vyombo vya kujistarehesha bila gharama. Hii ni part time ehh?

Si ni nyie mnawabaka watoto wadogo pengine watoto wa ndugu zenu bila haya wakipata mimba mnawalazimisha kutoa mimba wangali vigoli. Wanajiuza hawa ehh?

Si ni nyie mnasema mnapenda huduma ya kikahaba na kuwalazimisha pengine wake wenu kushiriki mkiwatumia kinyume cha maumbile kukidhi haja zenu, eti akulidhishe kimapenzi. Hawa wameliwa kwa kujiuza,eeeh!

Si ni nyie mnaowafuata watoto wanaolingana na watoto wenu mnabebwa kwenye vifua vya watoto hawa bila aibu. Wanajiuza?

Si ni nyie mnawalaghai mabinti wanapiga picha za ngono. Picha hizo sura za mabinti hawa tu zinaonekana za kwenu huwa mnaficha. Malipo ya kujiuza hayo ehh?

Si ni nyie kwa tamaa zenu mnabaka hadi viumbe vingine ili mridhishe hamu zenu. Hapa bei sokoni iko juu ehh?

Si ni nyie mnaokaa vijiweni kutathimini ya nani tamu ipi hajaguswa mnawekeana dau kumpata bikra. Mpango wa kupata bidhaa adimu ehh?

Jamani mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Kama wazazi mmetuita m.a.l.a.y.a tungali wadogo wakati hatujui mtu mme, tumeshuhudia mkiwanyanyasa mama zetu kwa tabia zenu mbaya huku mkitaka wawape heshima tumekua katika jamii ambayo mwanamke si mtu ni bidhaa, wengine mmewachagulia maisha mkiwanyima hata elimu achilia kina sie tusiojua sura za baba zetu. Mnataka nini?

Naandika haya baada ya moyo wangu kushindwa kuvumilia kuendelea kutukanwa namna hii. Nakataa udhalilishwaji huu.

Ole wenu! Ole wenu! Ole wenu mnaojipa moyo kuwa wanawake wanajiuza na kuendelea kuwafanyia maovu.
.



Mbona unaangalia upande mmoja wa Tshiling?
Na nyie mnavyokuwa na bwana zaid ya mmoja tuwaitaje? Kuwa Malay.a sio mpaka ujiuze..

Mnavyobambikia wanaume watoto? Tuwaitaje..

Afterall kuombwa tigo hujashikiwa bunduki ni kutokuwa na msimamo ndio yanayowakuta.

Wapo hadi w/wake wanaokaa vijiweni such as Saloon na kupiga umbea ya flani kibamia, haujui kazi mara yule m/ume suruali.

Kupigwa picha ya uchi na kukubali ni kuwa na akili yako finyu, kwann usimwambie na mimi nataka picha yako ya uchi?

Tunapenda huduma yenu ya kikahaba kwakuwa mnaenda kujiuza, sitisheni hiyo biashara ya kuuza utu tuone m/ume ataenda kufanya nini. Kisingizio eti maisha magumi mpaka unauza utu wakati kuchoma vitumbua unaona aibu.

Tunawaacha na kuwaita sio"Wife Material" kutokana na tabia zenu mlizonazo such as Tamaa kuwa m/ume zaidi ya mmoja, kiburi n.k


Kikubwa mbadilike na nyie mnaojiona wanawake wa kisasa mbona hamjiulizi miaka ya nyuma hamkuitwa Malay.a na kwanini sasa hivi ndio mnaitwa hivyo.
 
Wanaume wenyewe malioo kibao wengine wameoa kumbe nyuma ya panzia mashoga,wakipata wanawake wenye kipato wanakua nae kwa c kwamapenz bali apate tu pesa bila kujali hisia za mwanamke na still wanatudharau eti tunajiuza, kama unaona hatuna mapenzi ya kweli acha kujishughulisha na mapenzi.
 
Mbona unaangalia upande mmoja wa Tshiling?
Na nyie mnavyokuwa na bwana zaid ya mmoja tuwaitaje? Kuwa Malay.a sio mpaka ujiuze..

Mnavyobambikia wanaume watoto? Tuwaitaje..

Afterall kuombwa tigo hujashikiwa bunduki ni kutokuwa na msimamo ndio yanayowakuta.

Wapo hadi w/wake wanaokaa vijiweni such as Saloon na kupiga umbea ya flani kibamia, haujui kazi mara yule m/ume suruali.

Kupigwa picha ya uchi na kukubali ni kuwa na akili yako finyu, kwann usimwambie na mimi nataka picha yako ya uchi?

Tunapenda huduma yenu ya kikahaba kwakuwa mnaenda kujiuza, sitisheni hiyo biashara ya kuuza utu tuone m/ume ataenda kufanya nini. Kisingizio eti maisha magumi mpaka unauza utu wakati kuchoma vitumbua unaona aibu.

Tunawaacha na kuwaita sio"Wife Material" kutokana na tabia zenu mlizonazo such as Tamaa kuwa m/ume zaidi ya mmoja, kiburi n.k


Kikubwa mbadilike na nyie mnaojiona wanawake wa kisasa mbona hamjiulizi miaka ya nyuma hamkuitwa Malay.a na kwanini sasa hivi ndio mnaitwa hivyo.

ngoja niondoke hapa.. hivi kumbe na huyu mwanangu atakuja kunitukana siku moja??,hiv kumbe kuzaliwa mwanamke ni kuwa malaya,
kweli Jf ni home of Great thinkers
 
Majaribu2013 aje hapa awaombe radhi dada/mama/watoto na shangazi zetu. Binafsi sikufurahishwa na yaliyoandikwa katika ile habari!

Haya nakuongezea na nyingine hii hapa:-
Updates 2
============================== ====================
Nimepata PM nyingi sana za malalamiko, nimeona post kama mbili zimeanzishwa kuipinga hii post bahati mbaya zimekuwa post za hasira ma matusi badala ya kuiface hoja. Najua pia wengi sana watakuwa wamebofya report abuse vya kutosha, na hata kunichongea sana kwa mods ili thred ifutwe lakini mods wanakili wameuchunguza uzi na kuona wacha darasa liendelee. Napenda nitumie muda huu kuongezea tu machache kama kujibu hoja za wanaolalamika.

1. Kuna ukweli kwamba neno "KILA" limeleta picha tofauti lakini si picha ya mantiki, na kwa kudhihirisha kuwa wanawake wamekamatwa pabaya ni pale wanapokuja na hoja nyepesi ya kushadadia neno "KILA" huku wakiacha mada na mantiki kamili ya uzi. Wengine wamediriki hata kusema sina nidhamu kwa mama yangu, na nimemtukana mama yangu sijui hayo nimeyaandika wapi? Kama ni kosa na kujeneraizi mbona nanyinyi mnajeheraizi kwa kuniambia nimetukana mama yangu? Unajua mama yangu yuko wapi? anafanya nini? ana umri gani? Kwanini mnamface mama yangu? kwani ndo kaandika hii thred? mniface mimi mwenyewe.

2. Ukweli uko hivi, hili neno "KILA" limejumuisha wanawake wote wanaojihusisha na ngono, kama mama yako, dada yako, bibi yako hajihusishi na ngono wanini kumuunganisha kwenye thred ambayo haijamtaja? Lakini pia nimesikitika sana kwamba mnasahau ukweli ulivyo, hebu angalia hapa chini:-

=======>>>> Kusema kweli kwa mwanamke anayejiheshimu, anayeshughulika na mambo ya maana asiye na tabia za kuelekea na haya niliyoyasoma hawezi kukaa kukoment mada za ujinga ujinga huku JF, nyinyi mnaotukana na kuonyeshwa kukerwa na hii mada mmekoment mada ngapi za kipuuzi na kipumbavu humu ndani? siyo nyinyi mnaoshadadia kila mada ya huku MMU ya kuchangia bila kukosa? hili tu linaonyesha nafsi zenu zilivyo na utayari wa kuunajisi usafi mnaoutetea.

========>>> Kama kweli inawauma, mnasahau msemo usemao samaki mmoja akioza wote wameoza? Kama mna nia na mnasema mpo wanawake wasafi na wenye tabia njema pambaneni na hao wanawake wanaowachafulia jina kwa kuwaelimisha, kama wataendelea sifa inabaki vilevile kwa wanawake wote, acheni kulia lia vinginevyo jibadilisheni jinsia. Waelimisheni hao dada zenu, na machangu n.k wajiheshimu wasijiuze.

========>>> Kama mnabisha hao wanaojiuza wanatoka wapi? Si kwenye familia zenu nyinyi ambao mnajidai wasafi? mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Daima boga huzaa boga na nguruwe huzaa nguruwe, kama wazazi au wanawake mngekuwa mnatabia nzuri ongezeko la maasi ya wanawake kujiuza lingeongezekaje??? Jichunguzeni siyo kuja kunililia mimi hapa nimewadhalilisha angalia uovu unaofanywa na wanawake wenzenu mlie nao hao maana kama kuna mamba mto Ruaha basi tutasema Mto ruaha una mamba!

======>>> Kusema kweli wanawake mmeharibika mno siku hizi na mnatumia kigezo cha maisha magumu, ni aibu sana kwa wanawake, je wewe unayejidai ni msafi ulishawahi kumuonya hata dada poa mmoja au kumpa elimu juu ya tabia yake hiyo? Hata hili tu linatosha kuwaingiza kwenye lawama kwamba mmewaangalia tu wenzenu wanawachafua, unataka nani akuite msafi wewe wakati wanawake wenzako wanainajisi jinsia yako na wewe unaangalia tu? Ulishawahi kusikia tamko au wanawake wanaandamana kupinga wenzao wanaojiuza? fungeni kinywa cha kulalamika angalieni kwa undani mnaelekea kubaya zaidi.

=====>>> suala la ngono au tendo la ndoa siyo baya lenyewe lipo tu, na lipo kwa ajili ya furaha ya wote mwanamme na mwanamke, wote wanahitaji hicho kitu hakuna anayekataa, shida inaanzia pale nyinyi mnapoinuka na kwenda barabarani kuomba hela ili mfanyiwe ngono upuuzi mkubwa sana huu, au kuwatafuta wanawaume mkisha lala nao mnaomba pesa hii ndiyo imesababisha ongezeko kubwa la umalaya hapa nchini.

====>>> Sikatai mnunuzi pia anashida, lakini utanunuaje au utanunua wapi kama bidhaa hiyo hakuna? Hakuna mwanamke anayeweza kusimama sasa hivi mbele ya jukwaa akawatetea wanawake wengine kama ni samaki ameoza sana na kama ni embe limeoza sana hata likisafishwaje halifai kwa kula tena.

=====>>> Namalizia kwa kusema kwamba kama wewe ni msafi, kama mama yako ni msafi, kama mama yangu ni msafi, kama dada yako ni msafi nyamaza hakuna ujasiri wawanawake kusimama mbele siku hizi kujitetea, wengi wenu mmeoza tena mnaoshinda kwenye mitandao ya kijamii ndo hatari sana, mnatongezewa facebook tu mnakubali, hakuna lolote la kujieleza ninasema hakuna lolote la kujieleza, wanawake mmelifikisha mbali sana taifa hili, hata laana na mapigo mengi ya nchi hii yanatokana na rate ya uasherati kuwa kubwa. Mbona zamani haikuwa hivyo????

Mnisamehe tracy, sister, charminglady, na wengine wote. Rekebisheni jamii yenu imeoza.
 
ngoja niondoke hapa.. hivi kumbe na huyu mwanangu atakuja kunitukana siku moja??,hiv kumbe kuzaliwa mwanamke ni kuwa malaya,
kweli Jf ni home of Great thinkers

Kama una mabwana wengi we ni Malay.a tu hata uwe nani. Ndio mana mna kauli mbiu yenu Baba wa Mtoto anamjua mama tu.
 
Wanaume wenyewe malioo kibao wengine wameoa kumbe nyuma ya panzia mashoga,wakipata wanawake wenye kipato wanakua nae kwa c kwamapenz bali apate tu pesa bila kujali hisia za mwanamke na still wanatudharau eti tunajiuza, kama unaona hatuna mapenzi ya kweli acha kujishughulisha na mapenzi.


Hahahah jiwe gizani hilo inaitwa...pole bi dada ila acha kuwa na bwana zaidi ya mmoja hata kama hana hela mvumilie. Unapenda Less Wig wakati bwana hana uwezo ndio kisa cha kwenda umegwe na kibabu?
 
...si nyie nyie mnaoanza kuomba namba za simu...
...si nyie nyie wakati wa ugomvi/kutoelewana mnatuc watu kwa kutumia MAKU...NGESEM
..si nyie nyie manaopachika mimba halafu ukiambiwa UNAruka mita 100....baada ya toto kukua mnaanza kujirudi na kuja kuomba msamaaaa

...WANAUME ACHENI hizoooooooooo...mnabOA
 
Kama una mabwana wengi we ni Malay.a tu hata uwe nani. Ndio mana mna kauli mbiu yenu Baba wa Mtoto anamjua mama tu.
hata mwanaume mwenye wanawake zaidi ya mmoja ni malay.. ila siwezi kukaa chini na kusema all men are dogs..

na kusema ati mtu akikataa jambo ndo limemgusa uko soooooo wrong ndugu yangu,kama ulisoma psychology hata kidogo tu utaelewa sio lazima jambo likukute ndio likuumize na kama uko hivyo wewe ni selfish wa kutupwa..kwani ukikuta mtoto katupwa jalalani utasema sio wangu so it doesnt hurt?au hujawahi ona watu wanamvisha kichaa nguo sababu tu it hurts seeing another human being in that state?

Usifanye experience yako iwe ndo pie kwenye maisha ya watu,.ndio maana kuna maneno like kama,baadhi, etc kwasababu tu maisha yako sio maisha ya mwingine.
Kama unahitaji mtu au baadhi ya watu wabadilike,show them the cause and effect(positive and negative|)sio ushadadizi
 
majaribu 2013...
Kuna sababu yoyote inakufanya uwafikirie wanawake kwenye hali hasi kiasi hicho, au lengo lako ni kurekebisha baadhi ya dada/mama/shangazi na watoto wetu?

.>>> Tunajua wapo ila hawawauzii wanawake wenzao, wanatuuzia sisi kwa hiyo tujiangalie pia. Pia kuwasema hao walioolewa, wenye waume zao kuwa wanajiuza? Kwani wahudumiwe na nani?

Kama wewe ni mkristo naomba usome kitabu cha mwanzo, wakati Mungu anaamlaani Adam baada ya kuanguka dhambini,. HAKIKA KWA JASHO LAKO UTAKULA, NA MIIBA ITAKUCHOMA(sijaichukua kama ilivyo ), na mwanamke alilaaniwa vipi, KWA UCHUNGU UTAZAA! sasa wewe ungependa mwanamke ndo akupe na kukutafutia chakula?
Kutafuta rizki ni jukumu la mwanaume, mwanamke anabaki kuwa msaidizi.... hapa nazungumzia mume na mke, hao wanaojiuza huko buguruni mimi sina la kuchangia.
 
Last edited by a moderator:
hata mwanaume mwenye wanawake zaidi ya mmoja ni malay.. ila siwezi kukaa chini na kusema all men are dogs..

na kusema ati mtu akikataa jambo ndo limemgusa uko soooooo wrong ndugu yangu,kama ulisoma psychology hata kidogo tu utaelewa sio lazima jambo likukute ndio likuumize na kama uko hivyo wewe ni selfish wa kutupwa..kwani ukikuta mtoto katupwa jalalani utasema sio wangu so it doesnt hurt?au hujawahi ona watu wanamvisha kichaa nguo sababu tu it hurts seeing another human being in that state?

Usifanye experience yako iwe ndo pie kwenye maisha ya watu,.ndio maana kuna maneno like kama,baadhi, etc kwasababu tu maisha yako sio maisha ya mwingine.
Kama unahitaji mtu au baadhi ya watu wabadilike,show them the cause and effect(positive and negative|)sio ushadadizi


Wapo walioguswa kwa namna moja ama nyingine. Wapo waliomba hela humu kwa PM hata mtu hamjui (tumeshuhudia threads nyingi tu) kisa tu wameanza kuwasiliana. Na vilevile sikusema wote so sijaGenerize that why nimetumia Kama, na Asilimia.

Hiyo yote haisaidii kikubwa ni mlio na hizo mambo mbadilike.
 
Majaribu2013 aje hapa awaombe radhi dada/mama/watoto na shangazi zetu. Binafsi sikufurahishwa na yaliyoandikwa katika ile habari!

Unafikiri ni yeye tu mwenye mawazo ya ajabu hivyo? Kuna wenzie 'team waliojizaa wenyewe' nao walikuwa wanam support.
Mpo wachache mliokuwa mnajaribu kuwafumbua macho lakini wao aaa,aliyewachana midomo atawafunza thamani ya mwanamke siku moja
 
majaribu 2013...
Kuna sababu yoyote inakufanya uwafikirie wanawake kwenye hali hasi kiasi hicho, au lengo lako ni kurekebisha baadhi ya dada/mama/shangazi na watoto wetu?

.>>> Tunajua wapo ila hawawauzii wanawake wenzao, wanatuuzia sisi kwa hiyo tujiangalie pia. Pia kuwasema hao walioolewa, wenye waume zao kuwa wanajiuza? Kwani wahudumiwe na nani?

Kama wewe ni mkristo naomba usome kitabu cha mwanzo, wakati Mungu anaamlaani Adam baada ya kuanguka dhambini,. HAKIKA KWA JASHO LAKO UTAKULA, NA MIIBA ITAKUCHOMA(sijaichukua kama ilivyo ), na mwanamke alilaaniwa vipi, KWA UCHUNGU UTAZAA! sasa wewe ungependa mwanamke ndo akupe na kukutafutia chakula?
Kutafuta rizki ni jukumu la mwanaume, mwanamke anabaki kuwa msaidizi.... hapa nazungumzia mume na mke, hao wanaojiuza huko buguruni mimi sina la kuchangia.

Umesema Mkuu! At least we think the same! Ila usishangae sana, Wanaokwepa majukumu wengi wana mentality ya UMARIOO!!
 
Last edited by a moderator:
ina maana daddy umeshindwa kusoma riwaya hiyo hapo juu?
acha nikwambie yaonesha macho yako yameshaanza kuzeeka
huyo mama ameshindwa kuvumilia ameona bora ajianike hapo
kwani amedhalilishwa na mumewe, na kufanyiwa kitu mbaya
siujui mpaka hapa umeshaelewa au bado niendelee kukusimulia?
Hivi kuna jambo gani linaendelea hapa...
 
Back
Top Bottom