Kwasasa itakugharimu TZS 27,600 tu kama nauli ya kufika hapa mkoani kwetu Kigoma

Kigoma Region Tanzania

JF-Expert Member
May 25, 2021
229
593
Kusafiri na reli ni zaidi ya safari, maana utapata fursa ya kuona mandhari nzuri ya nchi ya Tanzania, uoto wa asili, mbuga za wanyama, huduma bora za chakula katika mgahawa ndani ya treni pamoja na huduma za afya.

Usafiri umepangiliwa kwa kuzingatia ratiba zilizowekwa kwa mpangilio ukilinganisha na aina nyingine za usafiri.

Treni hii ya Ordinary inatoka Dar es salaam siku ya Jumapili saa 9:00 Alasiri na huwasili Mkoani Kigoma siku ya Jumanne saa 12:20 asubuhi.

Nauli
Daraja la 3 mtu mzima ni TZS 27,600, mtoto ni TZS 13,800
Daraja la 2 mtu mzima ni TZS 55,600, mtoto ni TZS 27,800
Daraja la 1 mtu mzima ni TZS 76,100, mtoto ni TZS 38,050
*Watoto wenye umri kati ya 0-3 hawalipiwi nauli

Nakukaribisha Kigoma, nitakupokea station.

Kigoma_station.jpeg

Kigoma Railway station

Usafiri wa Train ya Kigoma (TRC) ni nafuu zaidi ukilinganisha na aina nyingine za usafiri kutokana na kuwepo kwa madaraja tofautii ambayo yanatoa fursa kwa watu wa vipato vya aina zote kusafiri.

1689338748518.png

Kazuramimba village

Unapokuwa kwenye mabehewa ya abiria unapata nafasi ya kuhama kutoka behewa moja kwenda behewa linginena kufurahia muonekano mzuri wa maeneo asilia na vivutio mbalimbali.
Njoo Kigoma utembee hata kwa siku mbili.

1689338892727.png

Karibu Kigoma

Treni hii ya Ordinary haina ubaguzi wa mizigo, unaweza kununua vitoweo ukasafiri navyo.
Mwanamke akiuza jogoo wake kwa mwanaume huyu kwa gharama ya shilingi 5,000

1689338978548.png

Jogoo wa 5000

Treni hii ya Ordinary ina Mabehewa ya Daraja la Kwanza Kulala, Daraja la Pili Kulala, Daraja la Pili Kukaa na Daraja la Tatu ikiwa na behewa maalum la Mgahawa kwa ajili ya Chakula na Vinywaji. Maisha ni rahisi sana.

1689339232459.png


Pata fursa ya kukutana na watu wapya ndani ya Treni ni furaha tupu.
Kigoma inapendeza.

1689339320791.png


Unaruhusiwa kununua chochote utakacho kwa bei nafuu kabisa, ukitaka Muhogo mbichi, ndizi mbivu, miwa n.k
Ukiwa ndani ya Behewa la Treni wewe ni Tajiri, lazima uletewe bidhaa za kununua.

1689339353014.png


.....................
Hili ndio jengo la station, wewe panda train ya Deluxe au Ordinary njoo Kigoma utembee, watu wa mji huu ni wenye ukarimu.
Kwenda sehemu sio lazima uwe na jambo maalumu, kuja kupaona Kigoma hilo ni jambo kubwa sana utakua umefanya maishani mwako. Kukanyaga ardhi hii maarufu ni jambo lenye historia kwako,
Njoo hapa Kigoma. Upate vitu vipya vya kufungua akili.

1689339479835.png
 
Kusafiri na reli ni zaidi ya safari, maana utapata fursa ya kuona mandhari nzuri ya nchi ya Tanzania, uoto wa asili, mbuga za wanyama, huduma bora za chakula katika mgahawa ndani ya treni pamoja na huduma za afya.

Usafiri umepangiliwa kwa kuzingatia ratiba zilizowekwa kwa mpangilio ukilinganisha na aina nyingine za usafiri.

Treni hii ya Ordinary inatoka Dar es salaam siku ya Jumapili saa 9:00 Alasiri na huwasili Mkoani Kigoma siku ya Jumanne saa 12:20 asubuhi.

Nauli
Daraja la 3 mtu mzima ni TZS 27,600, mtoto ni TZS 13,800
Daraja la 2 mtu mzima ni TZS 55,600, mtoto ni TZS 27,800
Daraja la 1 mtu mzima ni TZS 76,100, mtoto ni TZS 38,050
*Watoto wenye umri kati ya 0-3 hawalipiwi nauli

Nakukaribisha Kigoma, nitakupokea station.

View attachment 2687808
Kigoma Railway station

Usafiri wa Train ya Kigoma (TRC) ni nafuu zaidi ukilinganisha na aina nyingine za usafiri kutokana na kuwepo kwa madaraja tofautii ambayo yanatoa fursa kwa watu wa vipato vya aina zote kusafiri.

View attachment 2687809
Kazuramimba village

Unapokuwa kwenye mabehewa ya abiria unapata nafasi ya kuhama kutoka behewa moja kwenda behewa linginena kufurahia muonekano mzuri wa maeneo asilia na vivutio mbalimbali.
Njoo Kigoma utembee hata kwa siku mbili.

View attachment 2687815
Karibu Kigoma

Treni hii ya Ordinary haina ubaguzi wa mizigo, unaweza kununua vitoweo ukasafiri navyo.
Mwanamke akiuza jogoo wake kwa mwanaume huyu kwa gharama ya shilingi 5,000

View attachment 2687818
Jogoo wa 5000

Treni hii ya Ordinary ina Mabehewa ya Daraja la Kwanza Kulala, Daraja la Pili Kulala, Daraja la Pili Kukaa na Daraja la Tatu ikiwa na behewa maalum la Mgahawa kwa ajili ya Chakula na Vinywaji. Maisha ni rahisi sana.

View attachment 2687821


Pata fursa ya kukutana na watu wapya ndani ya Treni ni furaha tupu.
Kigoma inapendeza.

View attachment 2687822

Unaruhusiwa kununua chochote utakacho kwa bei nafuu kabisa, ukitaka Muhogo mbichi, ndizi mbivu, miwa n.k
Ukiwa ndani ya Behewa la Treni wewe ni Tajiri, lazima uletewe bidhaa za kununua.

View attachment 2687824

.....................
Hili ndio jengo la station, wewe panda train ya Deluxe au Ordinary njoo Kigoma utembee, watu wa mji huu ni wenye ukarimu.
Kwenda sehemu sio lazima uwe na jambo maalumu, kuja kupaona Kigoma hilo ni jambo kubwa sana utakua umefanya maishani mwako. Kukanyaga ardhi hii maarufu ni jambo lenye historia kwako,
Njoo hapa Kigoma. Upate vitu vipya vya kufungua akili.

View attachment 2687825
Kigoma ni pazuri. Nilikuwa huko siku chache zilizopita. Nilitembelea makumbusho ya Dr. Livingstone.

Kuna hali ya hewa nzuri ya ubaridi kiasi na ukijani unaovutia.

Kumbe michikichi inafanana na minazi! Niliona huko kwa mara ya kwanza siku hiyo.
 
Mkuu daraja la kwanza kulala kuna vitanda vingapi ? Huna hata kapicha utupie hapa ? Mpaka kigoma inachukua saa ngapi kutokea Dar ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom