Kwasababu umelipia haimaanishi utumie yote

Kwasababu umelipia haimaanishi utumie yote

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
1,353
Reaction score
2,231
KWASABABU UMELIPIA HAIMAANISHI UTUMIE YOTE

Siku hizi ukinunua kifurushi cha mawasiliano kwenye mitandao ya simu, unapewa meseji 250 kwa siku.Ukisema utume meseji zote hizi, hata kama utatumia dakika moja kutuma meseji itakuchukua dakika 250 ambazo ni sawa na masaa manne.

Sasa kama utatumia masaa manne kutuma meseji kwa siku kila siku inabidi uwe unafaidika sana na zoezi hilo.Lakini vinginevyo hutumi meseji zako zote kwa sababu umezilipia, unatuma zile unazohitaji.

Ukienda kula hotelini, mezani utakuta kuna chumvi, iko pale na unaweza kutumia vyovyote utakavyo. Lakini huwezi kuweka chumvi yote kwenye chakula kwa sababu ipo pale na umeshailipia kwenye chakula.

Chochote unachofanya kwenye maisha usifanye kwa sababu kipo, au kwa sababu kila mtu anafanya. Ila fanya kwa sababu ndicho unachohitaji kufanya.
 
Na kwenye papuchi? Maana najua ndo ulipopalenga japo imehit arround the bush
 
Back
Top Bottom