umekuwa muongomuongo na kinyonga. Mara useme hili;mara ukane lile.umekuwa mwanasiasa mwigizaji kwelikweli.kigoma uliaga ubunge mara mbilimbili. Kiko wapi? Chadema uliapa kuwa wa mwisho kutoka. Kiko wapi? Kwani umepatwa na nini? Umebadilika zitto!
Nasubiri bunge livunjwe ili niwaone wabunge 50 wa ukawa watakohamia act-wazalendo kama ulivyojinadi. Isipokuwa kweli,nitajiunga na wasiokuamini na kukuona msaliti. Juzijuzi hapa umewaita watanzania mwembeyanga uwatajie waficha mabilioni uswisi.nikaona kurejea kwa dr. Slaa wa mwembeyanga aliyetaja mafisadi 11 wa tanzania. Pamoja na mbwembwe zote kwenye vyombo vya habari na magari ya matangazo,hukutaja.ukagawa bahasha yenye majina ya wahindi!
Uko wapi uthubutu wako? Uko wapi ushujaa wako wa buzwagi? Yuko wapi zitto? Sijui umekuwaje. Lakini,chunga sana usije ukawa tapeli!
Mzee tupatupa (kwasasa dodoma)