Wewe endelea kujiondoa stress kwa kujidanganya na ACT ya waigizaji!ACT ndio chama makini cha Upinnzani, hivi vingine vinachumia tumbo tu.
Sana, hakuna utetez halisia, posho wanazitumbua tu.ACT ndio chama makini cha Upinnzani, hivi vingine vinachumia tumbo tu.
Ulikuwa na hoja nzuri ila matumizi ya X yamenifanya nikudharau.Pamoja na maxuri yote uliyosema na kujiuliza ila usisahau kuwa LIMBU NDIYE ALIKUWA MPINI WA CDM KUMUUA ZITO na bahat mbay ameshindwa hivyo hawana njia nyingine zaid ya kuendeleza tuhuma hewa na chuki za kipuuz kama SIFA za chama chao ZILIVYO
Kuthibitisha hilo eti eti eti na yeye kagombes ubunge mwanzs kupitia chama kilichomtuma kumuua xito(CDM) Maskini Limbuuuu....Mboweeer...Slaaaa...
Lisuuuuu....AIBIKENI NA CHAGADEMA YENUU
Tatizo uongo wewe unageuza JF ni platform ya kumtukana Zitto safi sana Mods hizi nyuzi za uongo uongo dawa ni kuziunganisha tu.
Hivi eti huyo ni afisa wa CDM anatweet kitu kama hicho na misukule inaamini kua hata kama ni kweli ZZK anatumika ni wajinga kiasi gani ifikie hadi kuwakilisha CCM tuache majungu Vijana Chapeni kazi.ZZK ni nani hadi kila akifanya yake mnapagawa? Huo muda si mngewambia vijana namna ya kujikomboa.Mtoi ni kilaza sana na hii inaonyesha makao makuu ya CDM ilivyokumbatia vilaza natamani sana wachukue nchi tuone hao vilaza watapewa nafasi gani.
Acheni siasa maji taka wakati huu ni Lala Salama.
Dah kweli, huyu jamaa msaliti sana. Mtu mbaya kweli kweli kwenye mageuzi ya nchi hii, Simshangai lakini watu wa kigoma ndivyo walivyo. Amemfukuza limbu, akabadili jina la chama, akabadili katiba, ndani ya siku sita akajipa cheo cha uungu wa chama, au nuru kama anavyoita yeye. Inawezekana kweli siku sita tu ndani ya chama unapata cheo kikubwa kuliko wote? Ajabu pia ni mpinzani gani anaondolewa bungeni, wabunge wa ccm wanalia machozi na kuomboleza? Ni mpinzani huyo au mwenzao? Hivi kweli tundu lissu leo afukuzwe bungeni, wabunge wa ccm watalia kwa ajili yake na kuomboleza? Ukipata jibu hilo, utajua zitto ni nani..
ACT ndio chama makini cha Upinnzani, hivi vingine vinachumia tumbo tu.
Zitto Zuberi Kabwe amekuwa akishambuliwa mara kwa mara kwa tuhuma mbalimbali ambazo zimekuwa zikirudiwa rudiwa bila ushahidi.Amekuwa akiitwa msaliti lakini bila ushahidi dhahiri.Pamoja na kufukuzwa ndani ya Chadema na kujiunga na ACT ambayo ni haki yake kikatiba lakini bado mashambulizi yanaendelea.
MASWALI YA KUJIULIZA;
1.Je, ana athari gani katika siasa?
2.Je, ni kweli ni tuhuma za usaliti tu ndizo zinazofanya aendelee kushambuliwa?
3.Je, ni hofu ya kushika nguvu ya upinzani?
4.Je, ni uwezo alionao katika kujenga hoja?
5.Je, kama hana madhara katika siasa za upinzani kwa nini anashambuliwa kwa tuhuma zisizothibitishwa?
- Sijawahi ona kokote siasa inakofanywa mwanachama wa chama kimoja kwa wakati huohuo ni mwanzilishi wa chama kingine cha siasa, sijawahi.
- Sijawahi kuona mtu anajiunga na chama fulani baada ya siku tano anapewa uongozi mkuu wa chama hicho, sijawahi
- Sijawahi kuona popote siasa inapofanywa, mwenyekiti wa chama yupo chini ya mtu fulani. Yahani kikatiba kabisa kuna mtu yupo juu ya mwenyekiti, hii pia sijawahi kuona.
- Sijawahi kuona popote pale chama cha upinzani kukipinga chama cha upinzani na si chama tawala. AGAINST CHADEMA TANZANIA(ACT). Kwa maneno au hata vitendo. Chama kinafanya sherehe kikipata wafuasi wa upinzani kuliko wa chama tawala.
- Sijawahi kuona chama cha upinzani kinafadhiliwa na chama tawala kiuchumi na kimikakati. Tumefanya uzinduzi wa chama chako Zuberi kwa gharama kubwa sana, air time ITV, chakula, ukumbi expensive, na mbwembwe nyingi. Lakini mbona hujawahi kuchangisha pesa toka kwa wanachama wako? Kama kuna mtu anachangia ni nani huyo? Mtamlipaje baadae?
- Sijawahi ona chama cha upinzani popote pale siasa inapofanywa, wafuasi wake ni wale wanachama na wafuasi wa chama tawala. Le mutuz, laki si pesa, musa alani n.k, hii nayo sijawahi ona.
Kwa yote hayo juu Zuberi kwa nini nisikuite kwamba wewe ni msaliti halisi wa demokrasia hapa nchini. Kama kweli wewe siyo msaliti mbona hujawahi kujitokeza na kukataa zile namba za simu walizozitoa chama chako cha zamani kuwa zilitumika katika ufisadi? Mbona sijasikia kuikana ile akaunti ya benki wa yule dada kule ujerumani?
UKINIJIBU HAYO KWA UFASHA WEWE KWELI SI MSALITI.
Ushujaa ulikoma mara tu baada ya kuingia kwenye ile kamati ya madini.Uko wapi ushujaa wako wa Buzwagi?