Kwanini wazungu wanakua/wanapata maendeleo wakiwa wadogo?

Bongo ukitaka kutoboa, tumia akili yako zaidi, itegemee akili yako zaidi

Ukitegemea mifumo zaidi basi jua unacheza kamali
 
Kuna bwamdogo aliajiriwa na kampuni ya Electromotive diesel (EMD) La Grange Illinois huko huko USA ni mchafu Sana katika ishu za electronics katika age ya 20.. Huku kwa age hiyo bado ndo tupo darasani tunakalili hizo diode, transistor, IC na microprocessor inavyofanya kazi..

Hatari sana!
 
Ni jambo la kawaida unakuta kijana wa miaka 19 hadi 23 amesha Settle kwenye career yake, kwa mfano kijana wa kizungu kabla ya miaka 20 tayari ana hold computer certificate zenye kuheshimika like OSCP etc, na anafanya mambo makubwa, wakati huku kwetu unakutana na mwanafunzi wa Computer engineering miaka 20 ndio kwanza anaaza kujifunza HTML ni nini,
How do they choose their career path?
Fulsa na mifumo ipo vzr ulaya,taasisi za kiuchumi zipo kusaidia sio kisiasa kama huku kwetu,na hii inachangiwa na mfumo mzuri wa kisiasa na demokrasia.
Fulsa zipo kwa kila mtu bila kujali connections za kisiasa
 
Mfumo wa elimu wa hovyo..imagine unatumia nusu ya maisha yako darasani kukaririshwa madesa wala sio kuvumbua na kubuni vitu vipya.

#MaendeleoHayanaChama
Wale wanaoota ndoto za darasani sijui kufanya mtihani au ndoto za shuleni ambapo watafsiri ndoto huwaambia kuwa utakutana na changamoto kwa kipindi hicho na blah blah zingine, Mimi huwa nawaambia kwa kiasi kikubwa sana sisi waTz tunaspend muda mrefu sana masomoni na unatutraumatize ndio sababu ya hizo ndoto, ni kitu kinachojirudia rudia sana akilini, na pengine kufanya mitihani ni kitu ambacho wengi wetu tulikuwa tunakiogopa sana katika maisha yote ya shule.

Binafsi huwa naamini hivyo na huwa natamani niwaulize ambao hawajaenda darasani kabisa kama na wao huota hizo ndoto.
 
Jibu ni misingi na mifumo ya maisha. Walipofika katika hatua ya maendeleo ni level ya kujitambua unaishi Ili utoe mchango gani kwenye jamii. Kwetu mifumo bado inajaribu kuleta uhakika wa kupata chakula, macazi na makazi.

Bado tunasafari ndefu , kizazi Cha sita kutoka hiki cha Sasa ndo kitaanza kiishi maisha hayo .
 
Kwasababu nyingi tu ambazo zinachangiza mojawapo ikiwa ni ya Mfumo wao wa Kielimu na Maisha kwa Ujumla wake.

~ Umri.
~ Muda wa kukaa darasani.
~ Vipaumbele vya Kitaifa.
~ Huduma za Afya.
~ Urahisishwaji wa upatikanaji wa huduma za msingi za kijamii.
~ Ushirikishwaji wa watoto wote (Sio wa Wakubwa tu) katika yote yanayowahusu watoto.
~ Kufanyia kazi mapendekezo ya Wananchi/ Wazazi walio wengi.
 
"Mlee to to ktk njia impasayo nae hataiacha hata atakapokua mzee" the bible says
 
Back
Top Bottom