Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,248
- 6,509
- Thread starter
- #81
Mkuu umemalizaMimi ni mmoja wa watu walio na mpango wa kurudi kijijini kwao baada ya kustaafu. Kama kufanya hivyo ni ushamba niiteni vyovyote mtakavyoniita na wala sitojali.
Kwanini nimepanga kurudi nyumbani (kijijini) baada ya kustaafu?
1.Wengi tunajua kuwa mtu anapozeeka kumbukumbu za zamani, utotoni humrejea kwa kasi sana. Ndo maana kuna nyakati wazee hu-act childishly. Sasa nataka nikare-experience maisha hayo ya utotoni kwenye mazingira halisi nilipoishi nikiwa mtoto. Uzeeni mtu hu-flash back mwanzo wa maisha, kumbukumbu za wazazi wako, marafiki wa utotoni, majirani na village life as a whole hurejea kwa kasi kichwani. Narudi nyumbani...
2.Binafsi huwa najisikia vyema nirudipo likizo nyumbani. Na watu husema 'jambo unalopenda kufanya ukiwa likizoni ndo unalotakiwa kulifanya baada ya kustaafu'. Ndio maana huwa napenda kwenda likizo kijijini kwetu.
3.Nikifa napenda nizikwe karibu na wazazi wangu, na likely by 60 nitakuwa nimekaribia 'kurudisha mpira kwa kipa', death becomes real. Ndio maana kila likizo lazima nitembelee mahala ancestors wangu walizikwa na kupafanyia usafi inapobidi.
4.Village life is cheap! na kama mstaafu nitatakiwa kuwa makini na matumizi yangu. Vitu vingi ni bei chee! Fikiria bei za matunda, mboga mboga na nafaka kule Mbeya,n.k. Uzeeni natakiwa kula mlo wenye afya (matunda na mboga mboga kwa wingi), nikienda kuishi Mbeya, Njombe, Tarime, Kilimanjaro,n.k nitavipata kwa bei cheee kabisa!
5.Uzee unahitaji utulivu bwana! Hizi kelele za magari na kumbi za starehe si vitu wazee tunapenda. Purukushani za vijana wa mjini nazo ni taabu kwetu wazee. Halafu above 60 ni vigumu kwa mzee kuendana na hustle za mjini, believe it or not. Inatuwia vigumu sana sisi wazee kwenda sambamba na mabadiliko ya haraka ya mjini (lifestyles, language za vijana, etc).
Hadi sasa maandalizi yangu ya kuanza maisha ya kustaafu kijijini yakoje?
- Nitastaafu miaka 10+ ijayo. Sikutaka kujenga kwenye viwanja vya familia, ambavyo ni vingi tu, bali nilinunua uwanja wa almost ekari 2. Humo nimejenga nyumba yangu na nimepanda miti ya matunda kidogo na ya vivuli. Hivi karibuni nitamtuma gardener akanitengenezee bustani. Sipendi maisha ya mjini ya kujibanabana kwa space ndogo. Nataka niishi kwenye Village paradise kama Le Grand Villa.
-Nina ekari 78 kwa ajili ya kilimo cha mpunga na mazao mengine, bila kusahau ufugaji wa kuku wa kienyeji.
MWISHO! Kama kuna wimbo unanivutia basi ni ule uitwao 'NARUDI NYUMBANI' ulioimbwa na Hayati Dr.REMMY ONGALA wenye kibwagizo:
"🎼 I want to home, I need to go back home.
The place that is our home,
Good hopes are still home...
Narudi Matimila, Remmy Oooh narudi Kinshasa.
Eeeeh, narudi Songea. Oooh narudi Majimaji..🎼🎹🎻"