Wiyelelee
JF-Expert Member
- Nov 9, 2012
- 1,071
- 347
Jana wakati Mh. Tundu Lissu anawasilisha maoni ya wachache Bungeni, alichambua vizuri sana maoni ya wasomi maarufu nchini, wakiwemo Mh. Mwakyembe, Prof. Issa Shivji, na wengine ambao hakuwataja. Kinachonishangaza ni pale mtu msomi ameandika kitabu (Prof. Shivji) na Mwakyembe (PhD. Dissertation yake) lakini leo anatetea kingine. Ndo maana leo naamini msemo wa Marehem Prof. Chachage aliposema ma professor wa kweli ni wachache sana, kwa vile wengine wamekuwa so easy and loose! Aibu sana! Nini kinawafanya wawe hivyo? Je wakirudi tena darasani wanafunzi watashila lipi?