Kwanini Warundi wanapenda kuwa wakimbizi?

Kwanini Warundi wanapenda kuwa wakimbizi?

Hawa wanapenda sana Tanzania,kuna warundi kibao wanajiita wachaga kisa wanaogopa kusema wametokea kigoma eti watarudishwa Burundi,wengine mapaka wana passport za Tanzania.Tanzania kuzuri,hawa Warundi wamepata njia ya kukimbilia kwetu kwa sababu ya tatizo la uchumi kwao na wala siyo haya maandamano yanayofanyika Bujumbura
 
Na tunaambiwa kuwa hizo vurugu ziko Bujumbura tu, sasa kwa nini wasikimbilie mikoa mingine ya mbali badala ya kukimbilia Tz? nafikiri wanaitumia hii kama chance ya kuvuka boda
 
Na tunaambiwa kuwa hizo vurugu ziko Kigali tu, sasa kwa nini wasikimbilie mikoa mingine ya mbali badala ya kukimbilia Tz? nafikiri wanaitumia hii kama chance ya kuvuka boda

Wewe tutusa Burundi hakuna mji unaoitwa Kigali kenge wewe.
 
Nimefuatilia mgogoro wa Burundi jinsi ulivyo nimegundua kuna tatizo kubwa kwa hawa wenzetu warundi tofauti na hili la Nkuruziza kutaka kujiongezea muda wa kuwa madarakani.

Burundi kwa sasa hakuna civil war ni maandamano ya kawaida ya kutaka kumng'oa Nkurunziza madarakani tena tunaambiwa maandamano hayo yanafanyika mji mkuu Bujumbura sehemu zingine hali ni shwari sana.

Inakuaje wengine wafungashe kukimbilia Tanzania maandamano tu yanakufanya ukimbie nchi yako kwenda kuwa mkimbizi tena mwanaume nae anaacha kwenda kuandamana kuwaunga mkono anakimbilia kuwa mkimbizi.

Hivi huko kwenye kambi za wakimbizi kuna nini cha ziada kinachowafanya hawa watu waende kuishi huko na kuacha nchi yao, kwangu mimi binafsi mgogoro huu ni mdogo mno kutoa wakimbizi.


View attachment 253787

Halafu kibwengo kama huyu aliwakimbia panya road leo anashangaa anayekimbia possible civil war!! Kweli Mitanzania mingi ni makenge kabisa.
 
Walishaionja joto ya jiwe wanaujua ugumu wa vita na sifikiri kwamba wanapenda kuwa wakimbizi...
 
unahoja ya msingi, tatizo la burundi laweza kuwa kubwa kuliko tunavyo dhani ni la kisiasa, yawezekana vurugu za kisiasa ikiwa ni kichocheo tu nyuma yake kuna tatizo kubwa la kijamii, mbona kenya juzi juzi walichapana hatukuona wakimbizi kama wa burundi
 
Burundi iwe tu part of tz, maana warundi wanaipenda sana TZ.
 
Hao hawaitwi wakimbizi kuna msamiati mwingine nimesahau kidogo ila wanawaita kwa jina la "waomba hifadhi" kama sikosei
 
Bhanunu huyu jamaa Molembe hajatumia akili yake kwa ufasaha, kama angejua hao Warundi vita imeshawaathiri kwa kiwango gani, na hao anaowaona ni wanaume leo, miaka ya 1993 wakati wa mauaji ya hatari ndo kwanza walikuwa watoto, wakapotezana na familia zao, wakapoteza rasilimali zao pamoja na wazazi wao kuuawa mbele ya macho yao, asingesema.

Halafu ajue anapojimwaga JF,Twitter, FB, Airtel, sijui radio gani, kule Burundi hayo yote yamefungiwa. Hao wanaokimbia hawana full information kama alizonazo, wao wanasikia watu wanauana Bujumbura tu, sasa kwa nini wasikimbie?

Kikwete kasema ukipewa akili changanya na zako. Molembe Jiongezee akili kidogo inaonekana umeshiba, mind you sijakutukana ila nimekushauri tu, hakuna anayependa kuwa mkimbizi asilani.

Heshima kwako mkuu,raia wa Burundi wana sababu lukuki za kuikimbia nchi yao,wengi tunapata habari juu juu tu lkn ukweli wanao wao wenyewe
 
Last edited by a moderator:
Hiyo nchi ifutwe tu iwe sehemu ya tz maana kuna haja gani kuwepo wakati nusu ya raia wake tunakaa nao hapa, wanazalia hapa na kukulia hapa mpaka mtoto anafikisha umri wa mtu mzima hapa hapa tz???

Hivi kila nchi yenye matatizo ya kukimbiwa na wananchi wake ingelikuwa inafutwa ingekuwaje?,haya bhana na wewe ni maoni yako.
 
Uvivu ndiyo unawakimbiza wanataka kula bure na kulala bila kodi nyarugusu pale pia unhcr walipeleka ulaya baadhi ya wakimbizi na kuwapa uraia wa nchi tofauti wanavizia channel kama hizo
 
Wapi warundi wengi wamebaki Burundi hao wanaokimbia wanakimbizwa na njaa ,umasikini, na wanajua kambini watakula bure watalala bure . hawana lolote mfano maandamano yako Bujumbura tena baadhi tu ya mitaa kama buyenzi nk/lakin utasikia MTU wa mikoa ya gitega ,ngozi kakimbia ASA unajiuliza kakimbia nini hamna/Ni njaa tu
 
Back
Top Bottom