Kwanini wanawake hamna huruma?

Hehehe nilijua mtafikia hapa.

Bando la kwake.
Device ya kwake
Akili ya kwake
Maoni yake.

Sisi haswaa mimi siyo shuzi lake. Maana hanilipi kwa kumjibu kwenye utopolo wake
Sio lazima ujibu,unaweza soma ukapita kimya kimya
 
Sio lazima ujibu,unaweza soma ukapita kimya kimya
Mwanaume kulalamika lalamika ni dalili ya udhaifu.

Halafu usijitie ukiranja wa kunipangia la kufanya. Wewe unga mkono kivyako. Mimi napinga kivyangu.

Mnawalalamikia wanawake huku mkiendekeza taamaa zenu za kizinifu.

Piga nyeto hautoingia gharama ya kulipia chakula kisha kisiliwe
 
Daah kutokana na maelezo yako hayo,ebu fanya uchunguzi WA kiaina huenda mkeo anagawa baadhi ya vitu Kwa jirani au nduguze

Haingii akilini bajet ya mafuta Lita 5 halafu ulivyoleta Lita 10 zote zikaisha,that means ukileta Lita 15 nazo zinaisha hahahah

Nasema hayo kwakuwa Nina uzoefu na Bibi yangu mzaa Baba, yeye bwana analetewa mazagazaga yote lkn bwana huwa anagawa chakula ovyo ovyo Tu

Sasa wengine hufanya hivyo kuonyesha yeye mambo Safi au huruma iliyopitiliza ambayo ina kukosti wewe.

Naomba hili nalo usili dharau,huenda chakula kinaenda Kwa shoga yake au jirani zake
Hapa nazani Kuna tatizo ndio sehemu ya kuangalia Kwa Makini

Nakumbuka tukiwa wadogo nyumbani Tulikuwa tuna dada wa kazi alikuwa na Tabia hio

Bi mkubwa alikuwa ananunua Kg 50 za mchele Sukari kg50 Maharage yalikwepo ya kutosha Mahindi yapo ya kutosha

Lakini hata miezi miwili haifiki Mchele na Sukari na mafuta unakuta yameisha kuja Kufanya uchunguzi Kumbe huyo Dada alikuwa anapika chakula kingi alafu anwaga anagawa vitu Kwa marafiki zake kuanzia mchele Hadi Maharage I mean Kila kitu

@memmata alingalie hili Kwa umakini

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Siku zote misemo yangu
" ukitaka kufa maskini basi kaishi na maskini"
kuna vijana niliwaleta nyumbani waje tusaidiane na walipotoka familia zao wanashindia muogo walio lima yani nyama na wali wanasikia kwenye redio.ila leo wanampangia dada wakazi eti hawataki maharage sio chakula chao ni nyama wanazotaka.
Hahahah sisi tuna ndugu wakifika nyumbani wanakwambia wao hawali kande au Maharage wakati maisha yao huko Wanakotoka ni Kwa Hovyo kweli

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Aah kumwaga chakula siyo vizuri, inabidi mtu ujue kukadiria bana na hata kikibaki basi kitunzwe vizuri kwa matumizi ya baadaye. Chakula kakimwagwi ni dhambi hiyo watu wanatamani hata wapate uji tu wewe unatupa chakula😒

Hapo kwenye kutolewa out then unakula kidogo unaacha, mimi nikishiba naomba kufungiwa kitanisaidia nikirudi home, kwanza tuchakula twa out hata siyo twingi hivoo, nakula namaliza vizuri tu, kuku nusu anishinde? Aah wadada tuache kuigiza maisha 😂 ukirudi home unafakamia kiporo kikubwa eti kuku wa out unashindwa kumaliza.
 
Mwanaume kulalamika lalamika ni dalili ya udhaifu.

Halafu usijitie ukiranja wa kunipangia la kufanya. Wewe unga mkono kivyako. Mimi napinga kivyangu.

Mnawalalamikia wanawake huku mkiendekeza taamaa zenu za kizinifu.

Piga nyeto hautoingia gharama ya kulipia chakula kisha kisiliwe
Wewe huna tamaa,akilalamika wewe inakuuma nini?
 
Ulishawahi kutoka na mwanamke wa mjini sister du fulani out? Akiletewa menu anaagiza nusu kuku na chips alafu anakula kiupaja kimoja na vichips kadhaa anajifuta na tishu kwa mikogo vingereza vingi alafu anakwambia ameshiba!

Wanaume tumeumbwa mateso hadi kwenye ndoa yanatukuta haya. Leo naongelea wanawake walioolewa au wanaoshi na wanaume kama familia, kwanini wengi wao wana tabia hii? KUTUPA CHAKULA!!!

Nikijitolea mfano mimi binafsi nimetoka familia masikini, Mungu kanijaalia nna kipato cha kubadilisha mboga kwa sasa. Kwakuwa chanzo kikuu cha mapato ni mshahara basi huamua kununua vyakula vya jumla kila mwisho wa mwezi mf. mchele,unga, mboga kama maharage, dagaa, samaki, nyama ya ng'ombe, kuku n.k yani kiufupi mwisho wa mwezi friji inakuwa top kwa mazagazaga na huwa tunapanga kabisa na mke wangu anunue vitu kiasi gani lakini matumizi ya vitu hivi yanakuwa ya hovyo sana hadi kupelekea kitu fulani kuisha mapema kabla ya muda mliojiwekea. Na hata ukimuuliza kuhusu pesa ya matumizi uliyompa tofauti na ya manunuzi ya vitu hivyo utaambulia patupu.

Kuna jambo wanawake hawawezi kubajeti kabisa hasa kipimo cha chakula. Unakuta mchana wanapika ugali mkubwa hadi jioni unatoka kazini unakuta hotpot limejaa ugali na mboga kibao zimebaki wote wameshakula na mimi huwa sili nyumbani mchana siku za kazi. Usiku pia wanapika wali kibao unabaki, asubuhi hauliwi wote sababu kuna mkate au mwanamke kajisikia kupika tambi au chapati, mchana unakuta sufuria limelowekwa na mpunga kibao mwisho wa siku wanapewa kuku wale....

Nimeongea kwa ujumla wanawake maana hiki ni kilio cha wanaume wengi tunaofatilia mambo ya jikoni. Siwafichi mimi huwa nafatilia mambo ya jikoni.

Nna rafiki zangu wengi, ndugu zangu na jamaa wanaoishi maisha ya shida sana, mfano jana nilipigiwa simu na rafiki yangu ananiambia hadi muda huo (saa 2 usiku) hajajua watoto watakula nini akaniomba nimsaidie kumtumia buku mbili tu japo anunue mkate. Si kwamba napesa nyingi lakini najua uhalisia wa anachoniambia sababu haya maisha nimeyaishi nilipambana nikamtumia hela ya kula siku hiyo.

Nikirudi kwa mke wangu mimi hajali kabisa unaweza kushangaa baada ya siku 15 tu anakwambia mchele karibia unaisha, namuuliza mmetumia mchele kilo 30 kwa siku 15?! Jibu lake rahisi anajibu 'unadhani mimi naumwaga, si watoto wako wanakula!' Mwanamke mwenyewe katoka familia hizi hizi kama zetu sijui kwanini hana uchungu!

Lakini si wote kuna wanawake wanajua kubajet aiseee... Kama shemeji yangu mama Alice nakumbuka wakati huo tunaishi nae nyumba moja na mume wake(rafiki yangu). Huyu mwanamke hatumii kwasababu vipo tu, nisiseme mengi.

Kama kusema nilishasema sana sasa hivi naumia tu maana ukizidi kuongea hawachelewi, utasikia "We mwanaume una gubu kweli, mambo ya jikoni yana kuhusu nini?"

Ah! Basi bana, namwachia Mungu
Hii ni changamoto hasa kwa familia ambayo bado inajipanga kimaisha, Unakuta asilimia kubwa ya kipato inaishia kwenye mahitaji ya nyumbani.

Mama wa watoto wangu huwa namwambia kwa uharibifu huu isingekuwa watoto kuna wakati nigegoma kutoa matumizi kabisa.
 
Basi atumie chakula vizuri la sivyo atapimiwa
Kuto tumia chakula vizuri ni kawaida kwa wanawake waki Afrika, Mama yangu mimi anayo tabia hiyo utakuta ana pika ugali mwingi tunakula mwingine ana utupa asubuhi alijitahidi kupika chakula kidogo alishindwa mpa leo akipika chakula lazima kibaki na asubuhi kina mwagwa, Mara nyingi ni ugali maana wali ukilala ni rahisi kuliwa tena asubuhi kuliko ugali.
 
🥲I feel you ..Saivi ndo nakumbuka enzi tukiwa wadogo mama akiwaekea chakula mkashindwa kumaliza mnapanga mstari mnafungua mdomo mnalishwa kilazima 😅nilikua nachukia ila nimekua sasa namuelewa na naishi na hio mentality.
 
Kama kusema nilishasema sana sasa hivi naumia tu maana ukizidi kuongea hawachelewi, utasikia "We mwanaume una gubu kweli, mambo ya jikoni yana kuhusu nini
Inasikitisha sana mwanaume kukosa sauti kwa familia yako..
 
mtu asiyejua bajeti ni wa kumwogopa,dawa yao ni moja hakuna kumwaga chakula,yaani hiyo ni order nikikuta mnamwaga chakula nawakatia huduma imeisha hiyo,.ama wazoeshe kutumia vipimo kulingana na idadi yao.
Bora hata wewe kuna huyu ndugu yangu yeye ndani kuna kuku,badae anahamu ya kitimoto,mshahara 500 per month
 
Tunapoishi ni mbali kabisa na familia zetu labda kama anagawa kwa mashoga zake na kwa majirani zangu sina shaka nao sababu ya life style zao. Lakini nisitoe majibu mapema nitalifanyia kazi pia
Kuna rafiki yangu mke wake huwa anawauzia majirani mchele, mkaa, mafuta nk. Jamaa huwa analalamika vitu vinaisha mapema lkn nashindwa kumwambia kwamba mke wake huwa anauza
 
Kuna rafiki yangu mke wake huwa anawauzia majirani mchele, mkaa, mafuta nk. Jamaa huwa analalamika vitu vinaisha mapema lkn nashindwa kumwambia kwamba mke wake huwa anauza
Wewe sio jirani mwema hata kidogo!

Tena unasikia mwanaume mwenzako analalamika hlf unakausha
 
Kulalamikia vitu kama hivi ni ushamba
kwa mtu mwenye malengo ya mbele,kwa mtu asiye na malengo anaishi ilimradi tu ndo atasema ni ushamba,na pia nikupe siri tu hata matajiri unaowaona leo wanamwaga bia ni watu wa bajeti sana,yeye hata mia anataka ajue imetumikaje
 
Back
Top Bottom