Kwanini wanajeshi wana kauli za kibabe?

Kwanini wanajeshi wana kauli za kibabe?

Hivi unafikiri ni kwanini unafanya code switching ya lugha ya kiingereza na kiswahili na sio lugha nyingine katika uandishi wako. Majibu ulioyapata yahusianishe na muktadha wa swali lako.

Sasa Hapa Tunajadili Ubabe Wa WAJEDA Wenu Wa TZ au Code Switching Ya English Na Kiswahili? Kama Vipi Ianzishie Uzi Wake.
 
Sasa Hapa Tunajadili Ubabe Wa WAJEDA Wenu Wa TZ au Code Switching Ya English Na Kiswahili? Kama Vipi Ianzishie Uzi Wake.

Unabidi ujue kwanini mwandishi kafanya hivyo na hayo ndio majibu kwa upande wapili. Kama uwezo wako wa kufikiri ni mdogo achana na comment niliyoitoa.
 
Si wanajeshi wote wapo wengi wastaarabu sana lakini wapo wengine unaweza kushangaa jinsi wanavyojiona wapo juu ya kila kitu.

Mara nyingi wanajeshi waliokwenda shule hawana shida wanajua wapo jeshini kwaajili ya kulinda mipaka ya nchi lakini wapo wale wanajeshi ambao shule imewapita kando hawa ndio shida.

Huna uhakika na ukiongeacho karibu kujipa mkesha wiki sita na mazoezi magumu yaambatanayo na kazi ngumu utaona nini sababu ,hali hiyo ni mwanzo tu has a pindi utokapo kozi ila baadae hupungua .chezea madoso wewe ?
 
Naunga mkono . Maofisa wa Jeshi ni waelewa sana na wanatumia reasoning kuliko hawa ma private na makoplo..

Kawachanganyie mada uone kwamba nyote hawa kupewa kariakooo Bali TMA izo mambo zingine muwe mnapiga kimya 2
 
Hawa jamaa wana lugha za kibabe saana na pia akiwa mmoja huwa wako weak saana ila uwakute kuanzia watano mtakubali mtaa mzima.

Wanajeshi na FFU wana ushirikiano saana tofauti na askari wengine wote wanajiona wababe na hawataki kusikia soja mwenzao kapewa kisago na RAIA. Watakuja kombania saba.
 
Eti nasikia hata kwenye mabedroom wako hivyo hivyo command kwenda mbele..utasikia. kuja hapa..lala chini..mguu upande..tulia bila kutingishika ... akimaliza tu anasema haya tawanyika!
 
Wewe mtutsi mke wa Matola rudi kwenu RWANDA au nenda forums za Rwanda tutolee utumbo wako hapa!


Ungenijua Nilivyo Masikini Wala Usingesema Kuwa Naingiza Pesa Hata Hivyo Nisipoisifia Republic Of Rwanda Niwasifie Akina Nani? Tz au?
 
Last edited by a moderator:
Unakusanya maoni ya watu uyapeleke wapi GENTAMYCINE ??!!

Watanzania nyuzi kama hii ni ya kususiwa haina lengo lolote zuri kwa wanajeshi wetu, ni ya kuchafua na kukashifu. . . . Kumbukeni jeshi lisilo na nidhamu na lenye unyanyasaji sio taswira nzuri kwa nchi na tasnia nzima ya ulinzi na usalama. . . kama wapo baadhi wana tabia hizo basi waripotiwe kwa hatua stahiki sio hapa panapolenga kuchafua jeshi. . . . .
 
Last edited by a moderator:
Wewe mtutsi mke wa Matola rudi kwenu RWANDA au nenda forums za Rwanda tutolee utumbo wako hapa!

Sasa Mimi Na Wewe Nani Atoke? Nimeanzisha Uzi Wangu Na MIGENYE Yako Imekuleta Ili Upakatwe Nami. Sasa Kati Yako Nami Utumbo Nani?
 
Hii inatokana na mazingira waliomo na hasa kuhusu masuala ya mafunzo na maisha yao ya kijeshi. Jeshini jambo la kwanza ni kutii amri. Ni suala la saikolojia. Unaishi kwa kuamrishwa na kutii amri. Jeshini hakuna masuala ya mjadala au debate. Ukiambiwa songa mbele ni lazima usonge mbele hakunacha kusema au kujibu usiniburuze.... Hakuna politics jeshini. Kule kama ni mkubwa ni mkubwa tu hakuna ujinga wa demokrasia na kadhalika ingawa of course ubabe kupita kiasi nao unaweza kuleta walakini. Kwa hiyo mwanajeshi akija uraiani anakuwa na saikolojia hiyo. Hata private uraiani anawaona raia kuwa nao wako chini yake kisaikolojia hivyo anaweza kuwapa amri.


Lakini utaona ipo tofauti kwa wale waliosomea karate au kungfu. Mafunzo ya karate yanaenda sambamba na uungawana, upole na kuwajali raia. Mafunzo ya karate yanasisitiza karate itumike tu kujilinda na siyo uchokozi. Katika mafunzo ya kungfu na karate ubabe hautakiwi. Nazungumzia kungfu na karate za kweli na siyo zile za wavuta bangi ... Kwa hiyo kisaikolojia kungfu na karate zina mafunzo ya upole na uungwana ..... Ubabe na ukali ni suala la saikolojia zaidi.
 
Back
Top Bottom