Kwanini wanajeshi na Polisi hawalipi nauli?

Kwanini wanajeshi na Polisi hawalipi nauli?

Kaulize pale Central Police au Lugalo Military Camp ama pale Ngome utapewa majibu mubashara kabisa.

Ila usisahau kuleta mrejesho hapa JF.
Ungejibu swali la mleta mada kama Great Thinker ingependeza zaidi!
 
Uchochezi hausaidii wasipolipa kinakuuma nini na hauna gari,umezaliwa umeyakuta heshimu
 
Mkuu mimi hata sishangai, unakuta mtu kama waziri anapata mshahara wa zaidi ya 20m@month lakini anakaa nyumba, ya bure huduma kama umeme, maji na mlinzi analipiwa na serekali. Wakienda hata sehemu za burudani wanaingia bure, kibaya zaidi hata wapambe wanaokuwa nao pia wanaingia bure. Halafu eti wanasimama mbele ya watu pila aibu wanasema wamejitolea kupigania wanyonge. Pumbavu kabisa unapata mshahara wote huo na huduma za bure kisha unasema umejitolea kupigania wanyonge!?
Soma mjomba au pambana na njaa yako
 
LIKE Niku ADD ,

Mkuu,
Sina uhakika na hayo uliyoandika.

Nimemuelekeza mahala.pa kupata majibu sahihi.

Ila tu, atuletee mrejesho mubashara hapa JF.

tatizo mkuu majeshi yetu yapo kisharishari sana mtu unaweza ukaenda kwa nia njema tu ya kujuzwa ila wakakufikiria unaleta utani.
 
Ungejibu swali la mleta mada kama Great Thinker ingependeza zaidi!

Idimi,

Mkuu laiti ungeelewa kuwa jibu hilo la Poise ndilo la ki great thinker hakika usingenilaumu.

Elewa kuwa Jeshi au Polisi wana vituo/ ofisi/kambi kila eneo la kitawala ...

Yeye muuliza swali anashindwa nini kwenda na kupata majibu mubashara kabisa kutoka kwa first hand sources of information!?

Wote waliojibu wametoa majibu mengi ya kufikilika na kudhania.

Ila majibu sahihi yapo kwenye maeneo niliyokutajia.

Hata nawe na mleta uzi, mnaweza mkaenda pale kwenye kambi/vituo au ofisi na mkapata majibu mubashara.

Ila kumbukeni tu kuleta majibu humu JF.
 
Ni kama motisha kwa sababu ya majukumu yao..Ukumbuke au tukumbuke kuwa kazi za Jeshi na polisi ni sensitive na ambapo muda wote anakuwa kazini kwa hiyo ukimuona askari ujue yupo kazini.. Na wasiotozwa nauli, ninavyofahamu mimi, ni wale ambao wako kwenye uniform au sare za kazi...ukivaa kama raia yaani pasipo kuwa na sare askari atalazimika kulipa nauli labda yeye mwenyewe ajitambulishe na kwa staha na siyo kushurutisha...Polisi na jeshi ni vyombo vya dola na vina heshima kubwa...ukivaa uniform ya jeshi au polisi ni heshima kubwa...wanajeshi wamejitolea kufa kwa ajili ya nchi, na wameapa kufa kuilinda nchi...hivyo ni lazima tuwape somesort of motisha...tunawaheshimu...tunasema wewe askari wa JWTZ unatulinda, kazi yako ni kubwa na uko tayari kufa kwa ajili yetu, kwa hiyo hatukutozi nauli...Mtu wa TRA hajaapa kufa kwa ajili ya nchi, wala mwanasiasa, wala mwandishi wa habari, wala mcheza sinema...Kuapa kufa kwa ajili ya nchi siyo suala la mchezo hata kidogo...Askari yupo kazini mahali pote au popote pale...jambazi akiibuka ndani ya daladala na kutaka kupora watu askari au polisi anakuwa kazini immediately kumdhibiti jambazi huyo....wahuni na magaidi wakitaka kuleta fyoko fyoko ndani ya basi la mwendokasi kama yupo askari wa JW au polisi analazimika kujitoa mhanga kuwalinda raia wengine. Raia anakuwa salama pale askari anapokuwepo karibu. Ni vizuri tuwapende askari wetu. Ni kazi sensitive.

Wanafunzi wetu wana utaratibu wa kulipa nauli kwa punguzo....ila kama mambo yakiwa mazuri wanaweza pia kupanda bure kwa utaratibu mzuri wa kuwa na mabasi yao....kuna kazi nyingine nazo ni muhimu kama vile waalimu wanaoelimisha jamii yetu...nao tunawaheshimu...nao tunaweza tukasema, kama alivyojaribu kufanya RC Makonda kwa Dar es Slaam, kwamba ninyi waalimi ni watu muhimu, tunawamotisha kwa kazi yenu nzuri kwa nchi na taifa letu...msilipe nauli...ni lazima tuheshimu profession muhimu...tusizidharau...

Kuwa askari ni kazi kubwa...Askari haogopi ovyo ovyo..siyo kama mwanamuziki mmoja wa kizazi kipya alipooneshwa bastola tu mahali fulani alikimbia na kupotea kwa muda katika eneo hilo


!
!
Kuna aliyewalazimisha kufanya hivyo?
Wengi wapo kule kutokana na ukosefu ya ajira mtaani. Wanalipwa vizuri zaidi ya wafanyakazi wengi tu muhimu. Walipe nauli.
Wakati wanapambana na hali zao wasitingishe za wengine
 
MKUU UNAVYOHOJI HUDUMA ZA MWANAJESH NI SAWA NA KUHOJI HATIMA YA USALAMA WA JAMHURI

MKUU, PATA PICHA WAZIRI ANALIPWA ZAIDI YA M.12 KWA MWEZI, MARUPURUPU, NYUMBA BURE, MLINZI BURE NA USAFIRI BURE

HALAFU MWANAJESHI UMLIPE LAKI 7 NA NAULI ALIPE? PANGO ALIPE? N.K?

HVYO KUPANDA DALADALA BURE NI KAMA KUWAPA MOTISHA NA KUTAMBUA MCHANGO WAO.

LAKIN KWA NATURE YA KAZ YA JESH KWA BONGO, MWANAJESH ANALIPWA KAWAIDA SANA NA HAWEZ KUKAA NA MIHELA, HVYO DALADALA BURE HUSAIDI WAO KUWAH KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA WAKATI PASIPO KISINGZIO CHA USAFIRI.

HVYO BINAFS NAISHAURI SERIKALI IWARUHUSU WANAJESH
1. KUPANDA BURE GARI YOYOTE, IWE YA MASAFA MAFUPI AU MAREFU
2. PIA WARUHUSIWE HATA KUSAFIRI KWA MELI, NDEGE BURE
3. WAPATE HUDUMA ZA AFYA BURE

WANAJESH NDYO WANAOTULINDA, WAKIANZA KUSUMBUA KUDAI MASLAH HATA HAPA JF HAUTAKAA...
 
Idimi,

Mkuu laiti ungeelewa kuwa jibu hilo la Poise ndilo la ki great thinker hakika usingenilaumu.

Elewa kuwa Jeshi au Polisi wana vituo/ ofisi/kambi kila eneo la kitawala ...

Yeye muuliza swali anashindwa nini kwenda na kupata majibu mubashara kabisa kutoka kwa first hand sources of information!?

Wote waliojibu wametoa majibu mengi ya kufikilika na kudhania.

Ila majibu sahihi yapo kwenye maeneo niliyokutajia.

Hata nawe na mleta uzi, mnaweza mkaenda pale kwenye kambi/vituo au ofisi na mkapata majibu mubashara.

Ila kumbukeni tu kuleta majibu humu JF.
Ndg. Na hii 'TEKA TEKA' na 'KAMATA KAMATA', 'POTEZA POTEZA' HOJI HOJI, inayoendelea nchini kwa kila anaehoji masuala ya "sirikali" unaweza kuwa na guts za kwenda pale Oysterbay ama Central kuhoji kwa nini askari hawalipi nauli? Si utaishia lupango kwa kesi ya uchochezi?
 
Soma mjomba au pambana na njaa yako

Tuliosoma ni wengi, ama wasomi wote wana ajira hapa nchini? Hapa sio suala la kusoma ni suala la kubadili huu upendeleo usio kuwa na sababu. Ukisema waliosoma utakuwa hujui unaloongea. Sasa unasema soma kisha upate kazi uanze kulipwa mshahara usiondana na wengine na wakati mwingine ukiangalia tija yako hakuna kwa taifa.
 
Askari halipi nauli lakin mwanae asiekua ba kazi analipa 200 kwenda shule🙂🙂
 
Hili swala la bure kwa kigezo eti ni motisha mimi sikubaliani nalo. Haya mambo ni hongo isiyo rasmi. Polisi na jeshi vimetumiwa na watawala kwa muda mrefu kulinda maslahi ya watawala wachache. Mimi ingekuwa serikali imeweka usafiri wa umma na askari wake wanautumia bila kulipa, kwa mbaali ningekubali. Lakini hata chombo cha mtu binafsi wanataka wapande bure tena kibabe hapo hapana.
Kazi zote zingeheshimiwa ili kuwe na usawa. Hata hili la kuwajengea nyumba askari wakati wanalipwa mshahara ni upunguani wa wananchi tu. Tulipaswa tukatae ujinga huu. Na hili hata kwa walimu na wataalamu wa afya. Kwanini mtu kasoma ka hitimu kaajiriwa na analipwa mshahara alafu ajengewe nyumba ya kuishi?! Au apande usafiri wa kumpeleka ofosini na kurudi bure?! Mshahara wake unakazi gani?! Kwanini analipwa sasa?! Bora kama serikali ingekuwa ikilipia nauli zao au walipie kidogo tofauti iwe subsidized na serikali lakini isiwe bure.
Tunalia hatuendelei kama taifa wakati kuna unyonyaji kila kona. Pesa ambazo zingenunua dawa eti wanajenga nyumba za polisi, wanajeshi,walimu na wahudumu wa afya. Mbona kada zingine hazijengewi nyumba?! Au kutokuvaa uniform?! Wahasibu na ma engineers wangekuwa wanavishwa uniform labda nao wangejengewa nyumba. Serikali mpya kila baada ya miaka kadhaa hakuna maono mapya. Kutokuwa serious na issues kunatufanya kuwa taifa la wendawazimu. Ka nchi kadogoo lakini vyeo vingii output ya vyeo ni ziro. Jeshi la wananchi linae brigedia, sasa na jeshi la zimamoto nalo lina brigedia hahaha hii shida nchi hii na niujinga. Vyeo na majeshi yote wanataka kila huduma wapate bure at our expense.
Natamani apatikane kiongozi atoe ujinga huu, nauli bure,kujenga nyumba za watumishi.
 
Ndg. Na hii 'TEKA TEKA' na 'KAMATA KAMATA', 'POTEZA POTEZA' HOJI HOJI, inayoendelea nchini kwa kila anaehoji masuala ya "sirikali" unaweza kuwa na guts za kwenda pale Oysterbay ama Central kuhoji kwa nini askari hawalipi nauli? Si utaishia lupango kwa kesi ya uchochezi?

Idimi ,

Mkuu,
Hamna tatizo kabisa.
Wewe nenda utapata majibu mubashara kabisa.

Ila ulete mrejesho hapa JF platform.
 
MKUU UNAVYOHOJI HUDUMA ZA MWANAJESH NI SAWA NA KUHOJI HATIMA YA USALAMA WA JAMHURI

MKUU, PATA PICHA WAZIRI ANALIPWA ZAIDI YA M.12 KWA MWEZI, MARUPURUPU, NYUMBA BURE, MLINZI BURE NA USAFIRI BURE

HALAFU MWANAJESHI UMLIPE LAKI 7 NA NAULI ALIPE? PANGO ALIPE? N.K?

HVYO KUPANDA DALADALA BURE NI KAMA KUWAPA MOTISHA NA KUTAMBUA MCHANGO WAO.

LAKIN KWA NATURE YA KAZ YA JESH KWA BONGO, MWANAJESH ANALIPWA KAWAIDA SANA NA HAWEZ KUKAA NA MIHELA, HVYO DALADALA BURE HUSAIDI WAO KUWAH KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA WAKATI PASIPO KISINGZIO CHA USAFIRI.

HVYO BINAFS NAISHAURI SERIKALI IWARUHUSU WANAJESH
1. KUPANDA BURE GARI YOYOTE, IWE YA MASAFA MAFUPI AU MAREFU
2. PIA WARUHUSIWE HATA KUSAFIRI KWA MELI, NDEGE BURE
3. WAPATE HUDUMA ZA AFYA BURE

WANAJESH NDYO WANAOTULINDA, WAKIANZA KUSUMBUA KUDAI MASLAH HATA HAPA JF HAUTAKAA...

likandambwasada ,

Mkuu,
Kabisa bila hao vijana kujitoa kwa ajili yetu hali ingekuwa tete sana.

Wanahitaji kuangaliwa zaidi ya ilivyo hata hivi sasa pale uchumi wa nchi yetu ukiwa umekua vizuri.

Hongera na pongezi kwa vyombo vyetu vyote vya ulinzi na usalama.
Kazi yenu ni nzuri.
 
Ni bora tujue kama kuna tamko la katiba,au tangazo la Rais huko nyuma linafuatwa au ni mazoea tu yaliyojengeka mara baada ya vita ya kagera.
Tena wengine hata akivaa nguo ya nyumbani anaapply ukauzu mpaka anaonyesha kitambulisho.
 
Ni kama motisha kwa sababu ya majukumu yao..Ukumbuke au tukumbuke kuwa kazi za Jeshi na polisi ni sensitive na ambapo muda wote anakuwa kazini kwa hiyo ukimuona askari ujue yupo kazini.. Na wasiotozwa nauli, ninavyofahamu mimi, ni wale ambao wako kwenye uniform au sare za kazi...ukivaa kama raia yaani pasipo kuwa na sare askari atalazimika kulipa nauli labda yeye mwenyewe ajitambulishe na kwa staha na siyo kushurutisha...Polisi na jeshi ni vyombo vya dola na vina heshima kubwa...ukivaa uniform ya jeshi au polisi ni heshima kubwa...wanajeshi wamejitolea kufa kwa ajili ya nchi, na wameapa kufa kuilinda nchi...hivyo ni lazima tuwape somesort of motisha...tunawaheshimu...tunasema wewe askari wa JWTZ unatulinda, kazi yako ni kubwa na uko tayari kufa kwa ajili yetu, kwa hiyo hatukutozi nauli...Mtu wa TRA hajaapa kufa kwa ajili ya nchi, wala mwanasiasa, wala mwandishi wa habari, wala mcheza sinema...Kuapa kufa kwa ajili ya nchi siyo suala la mchezo hata kidogo...Askari yupo kazini mahali pote au popote pale...jambazi akiibuka ndani ya daladala na kutaka kupora watu askari au polisi anakuwa kazini immediately kumdhibiti jambazi huyo....wahuni na magaidi wakitaka kuleta fyoko fyoko ndani ya basi la mwendokasi kama yupo askari wa JW au polisi analazimika kujitoa mhanga kuwalinda raia wengine. Raia anakuwa salama pale askari anapokuwepo karibu. Ni vizuri tuwapende askari wetu. Ni kazi sensitive.

Wanafunzi wetu wana utaratibu wa kulipa nauli kwa punguzo....ila kama mambo yakiwa mazuri wanaweza pia kupanda bure kwa utaratibu mzuri wa kuwa na mabasi yao....kuna kazi nyingine nazo ni muhimu kama vile waalimu wanaoelimisha jamii yetu...nao tunawaheshimu...nao tunaweza tukasema, kama alivyojaribu kufanya RC Makonda kwa Dar es Slaam, kwamba ninyi waalimi ni watu muhimu, tunawamotisha kwa kazi yenu nzuri kwa nchi na taifa letu...msilipe nauli...ni lazima tuheshimu profession muhimu...tusizidharau...

Kuwa askari ni kazi kubwa...Askari haogopi ovyo ovyo..siyo kama mwanamuziki mmoja wa kizazi kipya alipooneshwa bastola tu mahali fulani alikimbia na kupotea kwa muda katika eneo hilo
Well said
 
Back
Top Bottom