Ni kama motisha kwa sababu ya majukumu yao..Ukumbuke au tukumbuke kuwa kazi za Jeshi na polisi ni sensitive na ambapo muda wote anakuwa kazini kwa hiyo ukimuona askari ujue yupo kazini.. Na wasiotozwa nauli, ninavyofahamu mimi, ni wale ambao wako kwenye uniform au sare za kazi...ukivaa kama raia yaani pasipo kuwa na sare askari atalazimika kulipa nauli labda yeye mwenyewe ajitambulishe na kwa staha na siyo kushurutisha...Polisi na jeshi ni vyombo vya dola na vina heshima kubwa...ukivaa uniform ya jeshi au polisi ni heshima kubwa...wanajeshi wamejitolea kufa kwa ajili ya nchi, na wameapa kufa kuilinda nchi...hivyo ni lazima tuwape somesort of motisha...tunawaheshimu...tunasema wewe askari wa JWTZ unatulinda, kazi yako ni kubwa na uko tayari kwa ajili yetu, kwa hiyo hatukutozi nauli...Mtu wa TRA hajaapa kufa kwa ajili ya nchi, wala mwanasiasa, wala mwandishi wa habari, wala mcheza sinema...Kuaapa kufa kwa ajili ya nchi siyo suala la mchezo hata kidogo...Askari yupo kazini mahali pote...jambazi akiibuka ndani ya daladala na kutaka kupora watu askari au polisi anakuwa kazini immediately kumdhibiti jambazi huyo....wahuni na magaidi wakitaka kuleta fyoko fyoko ndani ya basi la mwendokasi kama yupo askari wa JW au polisi analazimika kujitoa mhanga kuwalinda raia wengine. Raia anakuwa salama pale askari anapokuwepo karibu. Ni vizuri tuwapende askari wetu. Ni kazi sensitive.
Wanafunzi wetu wana utaratibu wa kulipa nauli kwa punguzo....ila kama mambo yakiwa mazuri wanaweza pia kupanda bure kwa utaratibu mzuri wa kuwa na mabasi yao....kuna kazi nyingine nazo ni muhimu kama vile waalimu wanaoelimisha jamii yetu...nao tunawaheshimu...nao tunaweza tukasema, kama alivyojaribu kufanya RC Makonda kwa Dar es Slaam, kwamba ninyi waalimi ni watu muhimu, tunawamotisha kwa kazi yenu nzuri kwa nchi na taifa letu...msilipe nauli...ni lazima tuheshimu profession muhimu...tusizidharau...
Kuwa askari ni kazi kubwa...Askari haogopi ovyo ovyo..siyo kama mwanamuziki mmoja wa kizazi kipya aliponeshwa bastola tu mahali fulani alikimbia na kupotea kwa muda katika eneo hilo