Wapambe wa Lowassa sasa wahofia afya yake
Baada ya zoezi la CCM la kujivua gamba kushindwa, Waziri Mkuu wa zamani aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond, Edward Lowassa, sasa amejitamba kuwa yeye ndiye Rais ajaye wa 2015.
Watu waliokaribu na Lowassa wameniambia kuwa sasa hivi Lowassa ameshaiweka CCM mfukoni kwake kutokana na utajiri wake mkubwa wa kifisadi ambao umemuwezesha kuwanunua viongozi karibu wote.
"Sikiliza wewe, wajumbe wengi wa Kamati Kuu wako kwa Lowassa, NEC yote iko kwa Lowassa na zaidi ya asilimia 70 ya wajumbe wa mkutano mkuu wanamtii Lowassa. Hakuna cha kumzuia awe Rais 2015," mmoja wa wajumbe wa timu ya kampeni ya Lowassa alisema.
"Kikwete alivyoshindwa kutekeleza azma yake ya kujivua gamba imedhihirisha kuwa hana control au authority yoyote CCM. Hiki chama kiko kwenye himaya ya Lowassa."
Wapambe wa Lowassa wamesema kuwa ameikamata kanda nzima ya Ziwa na Zanzibar ambazo kwa ujumla wake zinawakilishwa na zaidi ya asilimia 50 ya wajumbe wa mikutano ya kitaifa ya CCM.
"Kitu pekee kitakachoweza kumzuia Lowassa asiwe Rais ni matatizo yake ya afya tu. Huyu mzee yuko very weak, akikushika mkono unatetemeka. Hata akishika kikombe cha chai, nusu ya chai inamwagika kutokana na kutetemeka kwake."
"Ini lake liko hoi, huyu mzee ni alcoholic sasa ... Anakunywa sana pombe kali, hasa Hennesy."
Baadhi ya wapambe wa Lowassa wamesema kuwa anaumwa kiharusi (stroke) ndiyo maana alikimbilia kwenda kwa Babu kule Samunge kupata kikombe. Pia Lowassa amekwenda mara mbili kwa mchungaji wa Nijeria, Joshua Emmanuel, katika jitihada zake za kuimarisha afya yake ili atwae uongozi wa nchi na kutimiza lengo lake kuu -- kuwa tajiri mkubwa kuliko wote kwenye bara zima la Afrika.