Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Ripoti kutoka Mashariki ya Kati, zinaeleza kwamba, Waislamu wengi wanaota ndoto za Yesu.
Katika ndoto hizo wanamuona Yesu akiwa na sura ya utakatifu, amevaa mavazi meupe, akihubiri amani na upendo na kuwaambia wamfuate.
Ndoto hizo zimesababisha idadi kubwa ya Waislamu kuongoka na kuigeukia imani ya Kikristo.
Kwa mujibu wa ripoti hizo, karibu asilimia 25 ya Waislamu walioongoka na kuwa Wakristo walieleza kwamba ndoto za Yesu ndio sababu kuu iliyowafanya kumwamini Yesu na kukubali kuwa ni Bwana na Mwokozi wa ulimwengu.
Ripoti hizo zinaeleza pia kwamba kulingana na sheria za kidini katika nchi hizo, watu hao walioamua kuwa Wakristo wanakabiliwa na adhabu kali na hata kifo. Hata hivyo, watu hao walioota ndoto hizo za Yesu wana ujasiri wa ajabu na wako tayari kufurushwa katika familia zao na kubeba gharama ya kuongoka kwao!
Sources:
CBN News
Mission Network News
Mission Frontiers
TrentStone
Katika ndoto hizo wanamuona Yesu akiwa na sura ya utakatifu, amevaa mavazi meupe, akihubiri amani na upendo na kuwaambia wamfuate.
Ndoto hizo zimesababisha idadi kubwa ya Waislamu kuongoka na kuigeukia imani ya Kikristo.
Kwa mujibu wa ripoti hizo, karibu asilimia 25 ya Waislamu walioongoka na kuwa Wakristo walieleza kwamba ndoto za Yesu ndio sababu kuu iliyowafanya kumwamini Yesu na kukubali kuwa ni Bwana na Mwokozi wa ulimwengu.
Ripoti hizo zinaeleza pia kwamba kulingana na sheria za kidini katika nchi hizo, watu hao walioamua kuwa Wakristo wanakabiliwa na adhabu kali na hata kifo. Hata hivyo, watu hao walioota ndoto hizo za Yesu wana ujasiri wa ajabu na wako tayari kufurushwa katika familia zao na kubeba gharama ya kuongoka kwao!
Sources:
CBN News
Mission Network News
Mission Frontiers
TrentStone