Yesu wenu apige marufuku vyama vya upinzan kufanya siasa asimgizie Mbowe
Yesu wenu ainjinie kununua wabunge na viongoz wa vyama vya upinzan unasema Mbowe
Yesu wenu aongoze kupotea ka akina Ben Saanane, Kanguye, kuteka watu na kuua mseme Mbowe
Hatuwezi kutumia uovu wa MTU mwingine yeyote kujenga mfumo mwingine mbaya zaidi.
Najua mnanielewa sana Ila mnatetea shetani wenu kama wale wanaomtetea yesu wao. Chadema chini ya Mbowe nawahakikishia kitafutiliwa mbali na watanzania wataendelea na maisha yao na maendeleo makubwa yataonekana. Kukwete alifanya mengi mazuri mpaka katiba mpya.
Badala ya kuzungumzia mambo ya msingi kama mifumo ya Elimu na mifumo ya siasa inayotupa viongozi wahovyo na walevi mkaanza kuzungumzia madaraka ya urais na namna ya kushinda chaguzi tuu matokeo yake CCM ikashtuka.Sasa katiba mpya tumeikosa na walevi waliotuingiza mkenge wanazidi kutumika kuua Demokrasia.
Jambo usilolijua ni kuwa Mbowe anatumiwa na Makundi ndani ya CCM kuangamizana. Magufuli anajua kila kitu ndio maana anawafungua Macho watanzania ili wachukue Tahadhari dhidi ya Wanasiasa wabinafsi wanaowahadaa wananchi.
Magufuli hajawahi kuwachukia Wapinzani ndio maana kuna watu kama akina Heche wapo na wanapambana kwa akili. Mbowe ameshindwa kuifundisha CCM namna bora zaidi ya kuleta maendeleo kwa kuwashirikisha wananchi wenyewe.
Hivi Jimbo la Hai ni jimbo la kusubiri serikali ilete fedha za kujenga miundo mbinu. Mbona Mbatia amehamasisha wapiga kura wake mpaka wanaweka barabara lami?
Unataka Rais amkubali Mlevi Mbowe au Mbunifu na Mzalendo kama Mbatia? Hivi wabunge wote wa upinzani wangetumia Mbinu ya Mbatia kujiletea maendeleo kwenye majimbo yao nani angekubali kuwahujumu wapinzani zaidi ya kuijenga nchi bila kugombania fito.
Chini ya Mbowe ni bora Chadema ife kabisa na nitahakikisha inakufa mana hatuwezi kamwe kuongozwa na Mhuni,Mlevi,Mzinzi, muuaji,Mwizi,tapeli wa kisiasa, muongo,dikteta, beberu, Mhujumu uchumi, mkabila ,muuaji na mpinga maendeleo.
Show ya kwanza ni kumnyang'anya jimbo la Hai. Akikosa bunge la kupinga maendeleo huku akiwa anasahau kuwa analipwa na serikali anayoitukana na kukejeli hapo itabidi arudi kwenye ofisi ya SACOS yake na kule tutahakikisha inatumia mpaka hela zake toka mfukoni kulipa kodi ili ajue umuhimu wa kujenga ofisi aliouchezea wakati akiwa analipwa Ruzuku.
Mbowe alitaka kutumia Uhuru wa Demokrasia ndani ya nchi kumhujumu mh. Magufuli kwa faida ya makundi ndani ya CCM.
Haiwezekani Mbowe azungumzie Demokrasia ndani ya nchi wakati yeye haonyeshi hata dalili ya kuruhusu Demokrasia kwenye kiti kidogo kama cha uenyekiti kwenye hiyo Sacos yake.
Hivi ni kipi kirahisi? :- Kuachia wengine kiti cha uenyekiti baada ya muda kuisha au kuachia Urais? Kama Mbowe anaamini hakuna Mtanzania popote wa kuwachia Chadema anashangaa nini Akina Mkamia wakisema Mh. Magufuli hana mbadala wa kumwachia Ikulu kutokana na msimamo wake dhidi ya Wezi na wahujumu uchumi ,ujenzi wa reli ya kisasa, ndege, umeme na maendeleo makubwa aliyoyafanya kwenye jiji la Dodoma ,Chato, Dar es Salaam, na kwingineko?
Au ni lipi Mbowe analolilalamikia kuhusu Uhuru wa kidemokrasia toka kwenye serikali ya Magufuli lakini kwenye chama chake halifanyiki tena kwa faida yake mwenyewe.??