Paka anampa Panya ushauri.
Hivi ushauri wa kujenga Makao makuu ya Chadema Dodoma hayakua ya maana kweli?
Tuache siasa za chuki na kutothaminiana.
Ndio maana Mbowe hathamini michango ya hali na Mali ya wabunge wenzake. Anaongelea yeye tu kuwa nimefungwa,nimetoa Mali zangu,nimefilisiwa na kila kitu kwa kujionea huruma yeye tu na kuona kuwa fidia yake ni kukalia kiti. Anasahau wenzake wamumizwa na wamepata nafasi zao kwa dhiki kubwa tofauti na yeye aliyerithishwa utajiri na hata Chama.
Alipaswa kuwasikiliza na kuwapa wenzake nafasi pia baada ya yeye kupata nafasi na muda wake wa miaka kumi kuisha. Huo ndio uungwana .
Mandela alifungwa miaka 27 lakini alipopata urais aliamua kungatuka baada ya awamu moja tuu.
Alijua wapo wengine wengi waliopambana wakati yeye akiwa Gerezani.
Chadema ingejenga Ofisi Dodoma kwa michango ya watu na sio kwa Hela zake toka mfukoni wala Ruzuku. Mbona watu walichanga mil. Mamilioni kuwatoa gerezani ndani ya siku tatu.
Chama chenye wanachama wengi kinashindwa vipi kuwahamasisha wanachama wake kujenga Ofisi zao kila mkoa.
Hivi makanisa na misikiti inajengwa ya nini kama haina umuhimu katika kujenga itikadi na imani?
Mbona mnakua na siasa nyepesi sana halafu mnataka kuingia Ikulu kufanya mambo mazito.
Mbowe hafai tena kuendelea kukijenga chama .
Ofisi ni center nzuri ya kujenga itikadi za vyama. Kila taasisi inapokua na Ofisi inakua na uhakika zaidi wa kufanya mambo yake.
Kuna wakati utafikia wananchi wataogopa hata kuipangishia Chadema nyumba za ofisi. Je , watafanyia wapi mambo yao?
Tuache ubishi na dharau zisizo na tija kwa kufuata mkumbo wa Mbowe.
Mbowe anatumika vibaya na makundi ndani ya CCM kuhakikisha kuwa 2025 chadema inakua taabani ili makundi hayo yapate nafasi ya kurudi tena madarakani ndani ya CCM. Mbowe ni mfanyabiashara hafanyi jambo lolote kwa hasara.
Najua ninachokisema.! Ndio maana viongozi wenzake ndio wanaokimbia mana wanajua nini kinaendelea. Sio muda mrefu Mbowe atakosa mpaka Katibu Mkuu mana yeye sio mfanyabiashara ni mwanasiasa mwenye kutamani kuona serikali mbadala inaingia madarakani wakati Mwenyekiti wake anavizia maslahi yake kiuchumi.
Subirini mtaona !
Mnyika anapotezewa kipaji Chake kwa manufaa ya Mbowe. Tundu Lisu anapotezewa kipaji chake kwa manufaa ya Mbowe.
Hakuna nia ya kushika Dola zaidi ya kushika uenyekiti. Dola linahitaji watu wengi wenye uwezo na Mbowe ndio anaowafukuza kutoka kwenye chama Chake.