Kwanini vyama vingi vinataka CHADEMA ife?

Kwanini vyama vingi vinataka CHADEMA ife?

Unawezaje kupambana na adui dhaifu kama ulivyoainisha na kushindwa kummaliza kwa miaka >28 na bado hauchoki?Hapo dhaifu ni nani?
Hamwezi kuishinda imani waliyonayo Watanzania kwa CDM kirahisi.Ni kwa kuwa hatuwezi kuambiwa lakini Nina uhakika gharama ya kuiangamiza CDM ni kuwa sana=Ufisadi wa Mali ya CCM na Taifa.Nadhani sehemu kubwa ya mapato halali na haramu ya CCM yanaenda kwenye hiyo project ya muda Mrefu ya kuiua CDM.
Pathetic reasoning and decision on Democratic Process.
Unajua fika, na ndio ulio ukweli, kuwa uchu wa madaraka kwa viongozi wa kisiasa, hasa nchi za dunia ya tatu, siyo tu kwamba ni chanzo cha uvunjifu wa amani katika hizo nchi, pia ndio chimbuko la migogoro ndani ya vyama vya siasa na hata michezo. Migogoro hiyo hutiwa chumvi zaidi na matumizi mabaya ya mali za vyama.

Kwa sababu kuu hizo, ni mtazamo finyu na hafifu kuendeleza fikra kwamba adui mkubwa wa CHADEMA yuko nje ya chama. Ni matatizo kiuongozi ndani ya vyama ya kutaka kuwa na madaraka makubwa ili kiongozi awe na nguvu ya maamuzi ya juu rasmali zake. Kwa Tanzania kuna mifano hai ikuhusu NCCR-Mageuzi, CUF na sasa CHADEMA inanyemelewa kumeguka na mzimu huohuo.

CCM, chama cha siasa kikongwe nchini pia kilifikia mahali kikaonesha dalili za kumeguka. Adui walikuwa ndani kwa ndani na hasa viongozi kugombea madaraka ili wajinufaishe na mali za chama. Matokeo ya uchunguzi wa mali za chama na kamati iliyoundwa na M/Kiti, ikiongozwa na Katibu Mkuu wa sasa, ni ushahidi wa jinsi viongozi wa vyama vya siasa wanavyofisadi mali za chama.

Hivyo basi, kwa CHADEMA, tuhuma za matumizi mabaya ya fedha dhidi ya Mbowe, M/Kiti wa chama, zinaweza kuwa za msingi na chanzo cha chokochoko zinazojitokeza kwa sasa. Suluhisho la kukiokoa chama wakati nchi ikielekea Uchaguzi Mkuu, ni kwa watuhumiwa kuweka wazi mambo wanayotuhumiwa ili kujenga imani ndani na nje ya chama.

Viongozi wakuu wa CHADEMA, hasa wa Kamati Kuu, ambao wanatuhumiwa kuodhi madaraka na maamuzi, wanapaswa kutambua kuwa Uchaguzi Mkuu ujao si wa kichama bali wa kitaifa. Wapiga kura ni pamoja na wasio wanachama wa chama chochote. Katika mazingira ya viongozi wa CHADEMA kutuhumiana hakika wanakiweka chama kwenye mtihani wa kukubalika na jamii.

Mnaomtetea Mbowe na genge lake, kwa kuhamisha lawama, hamumtakii mema na ni kama kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
 
Chadema wakishinda hili pambano watatisha sana
 
Kwanini vyama vyingi vinataka chadema ife?
Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi na kila chama kina haki ya kushiriki uchaguzi
Kila chama kina haki ya kusimamisha wagombea
Swali,ni je, kwanini vyama vyingi badala ya kutaka ccm iondoke madarakani vinataka chadema ndio ife?
Ukifanya utafiti usio rasmi utagundua cuf,nccr tlp na baadhi ya vyama viko tayari ccm iendelee kubaki madarani kuliko chadema kupata wabunge wengi au kushika dola,je vyama vyingine vya upinzani kutaka chadema ife lkn ccm ibaki madarakani viko sahihi?na kwanini unafikiri vinatamani chadema ife?
Chadema ni wasaliti wa Taifa, wabaguzi, watapeli na wahuni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua fika, na ndio ulio ukweli, kuwa uchu wa madaraka kwa viongozi wa kisiasa, hasa nchi za dunia ya tatu, siyo tu kwamba ni chanzo cha uvunjifu wa amani katika hizo nchi, pia ndio chimbuko la migogoro ndani ya vyama vya siasa na hata michezo. Migogoro hiyo hutiwa chumvi zaidi na matumizi mabaya ya mali za vyama.

Kwa sababu kuu hizo, ni mtazamo finyu na hafifu kuendeleza fikra kwamba adui mkubwa wa CHADEMA yuko nje ya chama. Ni matatizo kiuongozi ndani ya vyama ya kutaka kuwa na madaraka makubwa ili kiongozi awe na nguvu ya maamuzi ya juu rasmali zake. Kwa Tanzania kuna mifano hai ikuhusu NCCR-Mageuzi, CUF na sasa CHADEMA inanyemelewa kumeguka na mzimu huohuo...
Ufisadi ndani ya CDM mtuhumiwa No.1 ni Mwenyekiti Mbowe ila kwa wanaofisadi Mali za CCM mtuhumiwa siyo Mwenyekiti wake ni asiyejulikana na hatatajwa milele.IPO wapi ripoti ya kamati ya Bashiru? Pia utambue kuwa Mimi simshabikii Mbowe wala mwizi yeyote.
Umetaja uroho wa madaraka,kina waroho wa madaraka kulikoni wanaCCM hapa duniani? Mkitaka kuona ukali na ubabe wa CCM,gusia Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Hapo ndipo utafahamu kiwango chao cha uroho wa madaraka maana wanafahamu kuwa wakiruhusu hayo hawawezi kushinda Uchaguzi wowote.Wamezoea kushinda kupitia mifumo isiyo ya haki ndani ya NEC.
 
Mtoa mada umeuliza swali muhimu sana kwa siasa za nchi hii lakini pia inaonekana huijui vizuri CDM chini ya uongozi wa Mbowe.

Bila shaka hufahamu kwamba chama hiki kimekuwa kikitumia vibaya nafasi yake ya "chama kikuu cha upinzani". CHADEMA imekuwa na misimamo hasi dhidi ya vyama vingine vyenye ushawishi kama ifuatavyo.

1. CHADEMA imekuwa ikivitenga vyama vingine kuunda kambi ya upinzani kama ilivyokuwa kabla ya chama hiki kuwa chama kikuu cha upinzani. Kumbuka matumizi ya msamiati wa "kambi rasmi ya upinzani" hayakuwepo kabla ya uchaguzi wa 2010, bali kulikuwa na "kambi ya upinzani". Msingi wa matumizi ya msamiati huu, "rasmi", ni ubaguzi wa CHAFEMA dhidi ya vyama vingine vya upinzani vyenye wabunge. Ni kwamba msamiati huu ulilenga kuipambanua CHADEMA peke yake bungeni na kuminya wabunge wa vyama vingine vya upinzani.

2. Kuvisema vibaya vyama vingine. CHADEMA imekuwa ikitoa kauli za kejeli dhidi ya vyama vya upinzani na viongozi wake. NCCR na CUF vimeitwa "CCM B". James Mbatia aliitwa "mbunge wa viti maalum" kwavile aliteuliwa na Rais Kilwete kuwa mbunge. Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbowe amewahi kumtaja Lipumba kuwa ni "Politically Irrelevant" na "msaliti" eti kwavile tu alipinga maamuzi yake ya kumsimamisha Lowassa wa CCM kugombea urais kupitia UKAWA.

3. CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani na mshiriki wa UKAWA ilishindwa kupatanisha mgogoro wa CUF bali ilisimama upande Maalim Seif dhidi ya Lipumba. Zaidi makada wa CHADEMA walidhamiria kushiriki harakati kumuondoa Lipumba kwenye ofisi ya CUF Buguruni.

4. Kukiuka makubaliano ndani ya UKAWA kuhusu utaribu wa kumpata mgombea wa nafasi ya urais. CHADEMA ilitumia udikteta dhidi ya wana UKAWA (Lipumba na Slaa) waliotia nia kuwania nafasi hii kwa utaratibu wa kidemokrasia uliokubaliwa na vyama shiriki vya UKAWA na badala yake kumsimamisha kada wa CCM Lowassa katika nafasi hiyo.

Ukweli ni kwamba kwa mwenendo huu wa CHADEMA hakuna kiongozi au mkereketwa wa chama cha upinzani atakayeamini kwamba CHADEMA kina nia njema juu ya ustawi wa vyama vingine. Bali matumizi mabaya ya nafasi ya kuwa chama kikuu cha upinzani kwa kuvibagua vyama vingine imekuwa ni fursa (advantage) kwa ustawi wa chama tawala dhidi ya CHADEMA yenyewe na vyama vingine kwa ujumla.

Leo unapohoji kwanini vyama vingine vinatamani kuona CHADEMA imekufa ulitakiwa kwanza uoneshe kama harakati za chama hiki zinajenga "afya" kwa ustawi wa upinzani dhidi ya chama tawala.

Kiufupi anayeua CHADEMA ni CHADEMA yenyewe na si vyama vingine kwavile chenyewe kimekuw kikifanya jitihada za kuzima vyama vingine ili kichanuwe peke yake kwenye siasa za upinzani. Kwahiyo kila chama kinaitazama CHADEMA kuwa si chama rafiki bali ni adui kama ilivyo chama tawala.
 
Wanachi wanaomba tume huru ili Kama chadema itakufa ife kwa haki wananchi wapewe tume huru yao
Pia polis nao sasa waachie vyama uhuru wa kufanya siasa bila upendeleo
 
Kinakiliwa na wananchi ni kuwepo na uwanja sawa wa kufanya siasa kila chama sasa kipewe uhuru wa kufanya siasa kwa mujibu wa katiba
 
Je, vyama vingine haviwezi kujiimarisha bila chadema kufa? Ili nyumba yako ipendeze ni lazima ubomoe ya jirani?
 
Mbowe ndie anataka chadema ife ili asiwepo wa kuhoji matumizi ya ruzuku na michango ya bilioni nane alizotafuna

Anajua kikifa Hakuna was kuhoji anaingia zake mitini kimya kimya kusitafuna

Tunashukuru Takukuru kumuwahi na kugundua ujanja wake

Mbowe anatamani chadema ife hata leo
Kwa hiyo nae CAG mpya muongo?
 
Chadema inapendwa sana, tena bila sababu. Kwanza yale mavazi yao nikiyaona huwa nachanganyikiwa.
Nikisikiliza hoja zao bungeni, looh!
Chadema ipo mioyoni mwa watu. Haifi.
Kwa nini mnapenda kudanganya na kujidanganya ati []CHADEMA ipo mioyoni mwa watu[], wa nani? Chama chochote ni wanachana ambao ni watu wenye mitazamo, mahitaji na nia tofauti.

Mnasahau au mnadharau ukweli kwamba viongozi wana watu nyuma yao. Wanapohama chama na wengi wa wafuasi wao pia hukihama chama. Fanya hesabu ifuatayo, kujua idadi ya watu CHADEMA inapoteza kwa kuhamwa na kila:-
1) Mbuge x (Wanachama + wafuasi) kwenye jimbo
2) Diwani x (Wanachama + wafuasi) kwenye kata

Naamini idadi hiyo ni dhahiri itaathiri mategemeo ya CHADEMA kufanya vizuri kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka huu, ikizingatiwa wanaohama wanatoka kwa kulaumu uongozi na tuhuma dhidi ya M/kiti. Ikumbukwe pia hao wanachama na wafuasi pia wanao wafuasi wao na hao pia wana wafuasi.
 
1. Eti CHADEMA imeshiriki kumtoa Lipumba buguruni.??? Are you serious mkuu.
Huyu jamaa kwa mdomo wake alikiri kutokubaliana na kile kilichofanyika na hadi akajitoa mamlaka, leo hela alizohongwa sijui zimeisha au amepewa upya fedha nyingine , amekwenda kuimaliza kabisa CUF.

2. Kuna vyama huwezi kuviweka kama vyama vya upinzani, mf. TLP .. Ivi kweli mpinzani unaanza kumnadi unaeshinda nae ,, sasa kuna haja gani ya kushikana na vyama kama hivyo.

3. Mtasema CHADEMA waroho wa madaraka, sijui wezi na porojo kibao
Tuje kwenye uhalisia sasa, ivi kuna waroho wamadaraka kama CCM.angalia uchaguzi mkuu unavokua na shida hasa kwenye majimbo wanayoshinda upinzani matokeo hutangazwa kwa mbinde tena kwa kuchelewa.
Ukija kwenye wizi hapo,, CCM ni namba moja kwa kweli, trillions of money zimeibiwa na hao wana CCM

4. Huwezi kumpenda competitor wako mkuu. CCM wanaonesha kuvikubali vyama kama NCCR, TLP na CUF kidogo, kwa sasa kwasababu wanaamini havina athari yeyote kwao. Ndio maana utaona kutwa vinatetewa na hao wa kijani kua ni vyama vinavojielewa.
Ila ukitaka kujua Ccm hawajai kua na jema, kumbukia ile CUF ya mwaka 2000-2005, kila figisu ziliwalenga wao
 
CHADEMA yenyewe inapambana na vyama vyote vya siasa,hata Membe akihamia ACT huo urafiki wa mashaka unaisha.
 
Kwa nini mnapenda kudanganya na kujidanganya ati []CHADEMA ipo mioyoni mwa watu[], wa nani? Chama chochote ni wanachana ambao ni watu wenye mitazamo, mahitaji na nia tofauti.

Mnasahau au mnadharau ukweli kwamba viongozi wana watu nyuma yao. Wanapohama chama na wengi wa wafuasi wao pia hukihama chama. Fanya hesabu ifuatayo, kujua idadi ya watu CHADEMA inapoteza kwa kuhamwa na kila:-
1) Mbuge x (Wanachama + wafuasi) kwenye jimbo
2) Diwani x (Wanachama + wafuasi) kwenye kata

Naamini idadi hiyo ni dhahiri itaathiri mategemeo ya CHADEMA kufanya vizuri kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka huu, ikizingatiwa wanaohama wanatoka kwa kulaumu uongozi na tuhuma dhidi ya M/kiti. Ikumbukwe pia hao wanachama na wafuasi pia wanao wafuasi wao na hao pia wana wafuasi.
Mbona unateseka.
Utakufa mapema, relax!
 
Hakuna chama kinataka CHADEMA kife ila, kwa mujibu wa viongozi wanaokihama, chama kimeonesha kina:
• uongozi dhaifu;
• viongozi wasaliti;
• viongozi waoga;
• viongozi wasiojitambua;
• ufisadi wa mali ya chama usiothibitiwa; na
• kikundi cha viongozi, wanachama na wafuasi wasio na adabu, wao lugha ya matusi imekuwa ndiyo sifa moja kuu na imefanywa pia moja ya itikadi ya chama.
SIO KWELI. MPANGO WA 2015 ULIPANGWA KUIANGAMIZA CHADEMA
 
Kwa sababu ndiyo chama cha upinzani wa kweli na vingine ni matawi ya CCM
 
Kwanini vyama vyingi vinataka chadema ife?

Mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi na kila chama kina haki ya kushiriki uchaguzi

Kila chama kina haki ya kusimamisha wagombea

Swali,ni je, kwanini vyama vyingi badala ya kutaka ccm iondoke madarakani vinataka chadema ndio ife?

Ukifanya utafiti usio rasmi utagundua CUF, NCCR, TLP na baadhi ya vyama viko tayari CCM iendelee kubaki madarani kuliko CHADEMA kupata wabunge wengi au kushika dola. Je, vyama vyingine vya upinzani kutaka CHADEMA ife lkn CCM ibaki madarakani viko sahihi?

Na kwanini unafikiri vinatamani CHADEMA ife?
Vyama mamluki
 
Huu ukweli unapigwa vita kwa nguvu zote.
Kuna Kisacoss Fulani kwenye Eneo Fulani kilikua kinaitwa Talanta. Kilikua kinawanachama wasio na elimu ya kutosha lakini kiliongozwa na wasomi na wajanja wajanja wa kuwashawishi wakulima na wafanyabiashara wadogo wadogo na hata wa kati kujiunga. Kikafanikiwa sana. Baadae viongozi wake na mhasibu wao walianza kujichukulia fedha na kuanzisha miradi yao binafsi na kujitajirisha huku wakiwaaminisha watu kuwa kuna wanachama hawajarudisha marejesho ya mikopo yao na pia watu hawatoi michango yao. Wakati huo wao wanazidi kuneemeka na wakawa wanawaziba midomo wale walikua wanahoji kuhusu mgao wa hisa zao na faida ya sacoss yao. Ulafi wa viongozi ndio ulioua ushirika wao .Mwishowe Saccos ikafa na sasa wana mgogoro mkubwa upo kwa mkuu wa Wilaya.
Ccm wameifilisi nchi
 
Back
Top Bottom