Kwanini vitu vyangu vinapotea katika mazingira ya ajabu?

Status
Not open for further replies.

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,896
Wakuu,

Kuna mambo ambayo nimekuwa napambana nayo kwa muda mrefu sana katika maisha yangu. Nimejaribu njia nyingi, hasa za maombi hadi chumvi. Wakati mwingine naona kuna unafuu unakaribia kuja halafu ghafla narudi kule kule. Niliwahi kuleta uzi humu kuelezea hali yangu.

Kwenye masuala ya uchumi, nimefungwa vibaya sana hauwezi kuamini nikikwambia mambo niliyopitia. Unaweza kudhani mimi ni mzembe, mvivu au sina vipaji au akili ila ungenijua uwezo wangu pamoja na uchakarikaji wangu, utashangaa sana kwa nini sina mafanikio.

Kuna hili ambalo limeanza kujitokeza hivi karibuni. Kuna vifaa fulani vidogo ambavyo nilinunua kitambo kwa ajili ya shughuli ninazofanya. Nilikuwa nimepanga kuanza kuvitumia kuanzia mwezi uliopita. Sasa nimekuwa navitafuta katika chumba ambacho ni mimi pekee ninaingia, havionekani. Hii iliwahi kunitokea kwa kifaa kingine, nilikuwa nakihitaji sikukiona kabisa kila sehemu hadi mahitaji yalipokwisha ndiyo nikaja kukiona pale pale nilipokuwa nakitafuta.

Sasa nimetoa karibu kila kitu katika chumba nimechambua kila sehemu hivi vitu havionekani kabisa. Na naamini hivi vifaa vingeniletea mabadiliko makubwa sana katika maisha yangu.

Nimekuwa najizuia kuamini kwamba kuna watu (ndugu, rafiki au adui) wamenichezea kwenye mambo ya kiroho ila kuna mambo yanayonitokeaga nikiangalia vizuri naona kabisa kuna jambo haliko sawa nyuma ya pazia.

Kuna matukio mengi sana, na mengi yanafanana nikisema niyaorodheshe hapa sitamaliza. Kiufupi, namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema na naamini nitaweza kubadilisha hali yangu ila ni miaka sasa sina kipato pamoja na juhudi na maarifa yote niliyonayo.

Najiuliza, mpaka lini haya yataendelea? Ni lazima nibadili hii hali aisee!
 
Roho ya vizuizi..una mashambulizi.
Sali kataa hiyo roho..muombe Mungu atangulie mbele yako kila eneo la maisha yako..na uwe na mazoea ya kukiri kwa imani isaya 45:2,zaburi 107:20 na yohana 6:63..na hakika Mungu atakufanyia wepesi.
 
Mkuu usitafute sababu nje ya matatizo yako, usahaulifu ni tatizo common hata watu mashuhuri wenye brain heart kama kina einsten walishawahi kua nayo

Unaonesha ni namna gani umepagawa (frustrated) yani umefikia hatua ya kutumia chumvi kama recovery tool yaku retreive data zako halafu bado unataka kutuaminisha kua hujachanganyikiwa, seriously?

Mzee ukienda mahala kuchukua kitu ambacho ulidhani ulikiweka mahala hapo alafu ikatokea hujakiona, simply kuna mambo mawili, ni eidha uko high au hukumakinika kipindi unaweka, hivyo hujui exactly the right location you placed your things.

Au someone shifted them, usijipe immunity kwam,ba hakuna mtu mwingine zaidi ya wewe mwenye access ya ku-shift hivyo vitu, na sio lazima mpaka umjue au kusukumwa na personal experience kwakua huna mazoea ya kuwa na watu ambao wanaweza kuingia kwako wakati we haupo, basi hiyo ndo sababu inayokufanya ujione upo sahihi mpaka kufikiria sababu itakua ni uchawi kufikia hatua ya kufanya maombi na kupaka chumvi
 
Roho ya vizuizi..una mashambulizi.
Sali kataa hiyo roho..muombe Mungu atangulie mbele yako kila eneo la maisha yako..na uwe na mazoea ya kukiri kwa imani isaya 45:2,zaburi 107:20 na yohana 6:63..na hakika Mungu atakufanyia wepesi.
Mshauri vizuri, imagine kama hilo tatizo limemkuta ndugu yako unayempenda au ni vifaa vyako muhimu ulimuazima na unavihitaji kwa muda muafaka halafu anakuambia havioni unafikiri kwa wakati huo ushauri wa kwamba kusoma yohana na zaburi hautakua ridiculous?
 
Mkuu usitafute sababu nje ya matatizo yako, usahaulifu ni tatizo common hata watu mashuhuri wenye brain heart kama kina einsten walishawahi kua nayo

Unaonesha ni namna gani umepagawa (frustrated) yani umefikia hatua ya kutumia chumvi kama recovery tool yaku retreive data zako halafu bado unataka kutuaminisha kua hujachanganyikiwa, seriously?

Mzee ukienda mahala kuchukua kitu ambacho ulidhani ulikiweka mahala hapo alafu ikatokea hujakiona, simply kuna mambo mawili, ni eidha uko high au hukumakinika kipindi unaweka, hivyo hujui exactly the right location you placed your things.

Au someone shifted them, usijipe immunity kwam,ba hakuna mtu mwingine zaidi ya wewe mwenye access ya ku-shift hivyo vitu, na sio lazima mpaka umjue au kusukumwa na personal experience kwakua huna mazoea ya kuwa na watu ambao wanaweza kuingia kwako wakati we haupo, basi hiyo ndo sababu inayokufanya ujione upo sahihi mpaka kufikiria sababu itakua ni uchawi kufikia hatua ya kufanya maombi na kupaka chumvi
Achukue ushauri huu utamsaidia
 
Mkuu usitafute sababu nje ya matatizo yako, usahaulifu ni tatizo common hata watu mashuhuri wenye brain heart kama kina einsten walishawahi kua nayo

Unaonesha ni namna gani umepagawa (frustrated) yani umefikia hatua ya kutumia chumvi kama recovery tool yaku retreive data zako halafu bado unataka kutuaminisha kua hujachanganyikiwa, seriously?

Mzee ukienda mahala kuchukua kitu ambacho ulidhani ulikiweka mahala hapo alafu ikatokea hujakiona, simply kuna mambo mawili, ni eidha uko high au hukumakinika kipindi unaweka, hivyo hujui exactly the right location you placed your things.

Au someone shifted them, usijipe immunity kwam,ba hakuna mtu mwingine zaidi ya wewe mwenye access ya ku-shift hivyo vitu, na sio lazima mpaka umjue au kusukumwa na personal experience kwakua huna mazoea ya kuwa na watu ambao wanaweza kuingia kwako wakati we haupo, basi hiyo ndo sababu inayokufanya ujione upo sahihi mpaka kufikiria sababu itakua ni uchawi kufikia hatua ya kufanya maombi na kupaka chumvi
Hivi unadhani nimekurupuka tu na kuleta mada kama hiyo humu ndani au unataka tu kuonyesha wewe ndiyo unajua kutafakari mambo kisomi na kuwa hauamini makitu kama hayo yapo?

Nimewaza na kuangalia uwezekano huo wa mtu kuingia na kubeba hicho kifaa ambacho nakumbuka kilikuwa kwenye mfuko ila kama nilivyosema hicho chumba nina access nacho mimi pekee na huwa nakifunga muda wote. Nikawaza hata kama itokee kuna siku mtu aliingia labda nilisahau kufunga, kwa nini abebe hivyo ambavyo nina uhakika hatajua hata matumizi yake (ukiviangalia hata wewe unaweza kuvitupa tu) na aache vingine ambavyo ni dhahiri vingekuwa na thamani zaidi kwake? Hapo ndiyo inapokuja uwezekano wa yale niliyoyaelezea katika maelezo yangu.

Pia uwezekano wa kuwa nilimuazima mtu haupo na usilazimishe vitu ambavyo umeambiwa wazi na muhusika.

Ukiondoa hivyo tunabaki na nini?
 
Hivi unadhani nimekurupuka tu na kuleta mada kama hiyo humu ndani au unataka tu kuonyesha wewe ndiyo unajua kutafakari mambo kisomi na kuwa hauamini makitu kama hayo yapo?

Nimewaza na kuangalia uwezekano huo wa mtu kuingia na kubeba hicho kifaa ambacho nakumbuka kilikuwa kwenye mfuko ila kama nilivyosema hicho chumba nina access nacho mimi pekee na huwa nakifunga muda wote. Nikawaza hata kama itokee kuna siku mtu aliingia labda nilisahau kufunga, kwa nini abebe hivyo ambavyo nina uhakika hatajua hata matumizi yake (ukiviangalia hata wewe unaweza kuvitupa tu) na aache vingine ambavyo ni dhahiri vingekuwa na thamani zaidi kwake? Hapo ndiyo inapokuja uwezekano wa yale niliyoyaelezea katika maelezo yangu.

Pia uwezekano wa kuwa nilimuazima mtu haupo na usilazimishe vitu ambavyo umeambiwa wazi na muhusika.

Ukiondoa hivyo tunabaki na nini?
Kwa hiyo una amini wachawi wanahamisha vitu vyako?

Haya umeamini, ukatumia chumvi kama suluhu...hivyo vitu vimerudi?

Hapo umetumia chumvi haijafanya kazi lakini bado hutaki kukubali kua tatizo halihusiani na uchawi, utajenga imani nyingine kua hivyo vitu vimechukuliwa na wachawi wakubwa wasiozuilika na chumvi siyo?

Mimi nakushauri kitu kingine tena, install security camera kwenye nyumba yako afu utaona kama hivyo vitu vitapotea tena, kama ni mchawi basi usisahau kutuletea hapa tape inayoonesha mchawi akiyeyuka na mali zako
 
Kuna mambo hutokea kwenye maisha hadi unajiuliza kulikoni???wakati nasoma shule kuna nguvu fulani ya vikwazo dhidi ya maendeleo yangu shuleni!!NILITOBOA KWA TAABU SANA !!IMENIFANYA SASA NIISHI OBJECTIVE LIFE AND NOTHING TAKEN FOR GRANTED!!!
 
Wakuu,

Kuna mambo ambayo nimekuwa napambana nayo kwa muda mrefu sana katika maisha yangu. Nimejaribu njia nyingi, hasa za maombi hadi chumvi. Wakati mwingine naona kuna unafuu unakaribia kuja halafu ghafla narudi kule kule. Niliwahi kuleta uzi humu kuelezea hali yangu.

Kwenye masuala ya uchumi, nimefungwa vibaya sana hauwezi kuamini nikikwambia mambo niliyopitia. Unaweza kudhani mimi ni mzembe, mvivu au sina vipaji au akili ila ungenijua uwezo wangu pamoja na uchakarikaji wangu, utashangaa sana kwa nini sina mafanikio.

Kuna hili ambalo limeanza kujitokeza hivi karibuni. Kuna vifaa fulani vidogo ambavyo nilinunua kitambo kwa ajili ya shughuli ninazofanya. Nilikuwa nimepanga kuanza kuvitumia kuanzia mwezi uliopita. Sasa nimekuwa navitafuta katika chumba ambacho ni mimi pekee ninaingia, havionekani. Hii iliwahi kunitokea kwa kifaa kingine, nilikuwa nakihitaji sikukiona kabisa kila sehemu hadi mahitaji yalipokwisha ndiyo nikaja kukiona pale pale nilipokuwa nakitafuta.

Sasa nimetoa karibu kila kitu katika chumba nimechambua kila sehemu hivi vitu havionekani kabisa. Na naamini hivi vifaa vingeniletea mabadiliko makubwa sana katika maisha yangu.

Nimekuwa najizuia kuamini kwamba kuna watu (ndugu, rafiki au adui) wamenichezea kwenye mambo ya kiroho ila kuna mambo yanayonitokeaga nikiangalia vizuri naona kabisa kuna jambo haliko sawa nyuma ya pazia.

Kuna matukio mengi sana, na mengi yanafanana nikisema niyaorodheshe hapa sitamaliza. Kiufupi, namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema na naamini nitaweza kubadilisha hali yangu ila ni miaka sasa sina kipato pamoja na juhudi na maarifa yote niliyonayo.

Najiuliza, mpaka lini haya yataendelea? Ni lazima nibadili hii hali aisee!
Kaa utafakari kwa kina ulivipataje ?njia halali au njia haramu ?ukigundua JIULIZE pia,kabla ya kuvipata uliweka nadhiri(AHADI KWA MUNGU) ya aina yoyote ya sadaka au shukurani na je ulitimiza?
Huenda kuna jambo UMESAHAU mkuu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom