Kwanini vimbunga vingi vina majina ya kike?

Kwanini vimbunga vingi vina majina ya kike?

Analog

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2024
Posts
335
Reaction score
631
Katika hali ya kufikirisha kumekuwa na mtiririko wa vimbunga vingi kupewa majina ya kike, mbali na Hidaya kuna Katarina, Idai, Elida, Genevieve, Emilia, ingawa vipo kadhaa vyenye majina ya kiume na visivyo na jinsi kama jobo, erick, keneth na mengineyo.

Inafikirisha kwa kweli.
 
Naomba kujua kwa wale wataalamu wa haya mambo ni sawa kupewa majina ili kuweka kumbukumbu ya tukio hasa lakini ni kwanini hupewa majina ya wanawake tu.

Mfano;
Katarina
Irine
Anne
Pauline
Na Sasa pia tunaona jina la kike ni kwanini visiitwe wanaume au code name kama v.k 99 au P p 5?
 
Majina ya vimbunga ya kitanzania kama vingeanzia tanzania yangekuwa bhoke, manka, nyalande, ntiba, mwanjaa, sansa. Kimbunga mwamvua
 
Nadhani ni kutokana na kiherehere. Chenyewe kilitakiwa kiishie huko baharini ,lakini kinakuja pwani ya afrika
 
Naomba kujua kwa wale wataalamu wa haya mambo ni sawa kupewa majina ili kuweka kumbukumbu ya tukio hasa lakini ni kwanini hupewa majina ya wanawake tu.

Mfano;
Katarina
Irine
Anne
Pauline
Na Sasa pia tunaona jina la kike ni kwanini visiitwe wanaume au code name kama v.k 99 au P p 5?
Sio majina ya wanawake tu hata majina ya kiume Wanatoa hivyo ulivyotaja unavikumbuka kwasababu ndivyo vilivyoleta madhara zaidi.

Ni kweli zamani walikuwa majina ya wanawake tu,ila siku hizi hata majina ya wanaume pia wanatoa

Na tafiti zinaonyesha vimbunga vyenye majina ya kike vimeonekana kuwa na madhara zaidi kuliko vyenye majina ya kiume kwasababu watu wanavichukulia poa kutokana na hayo majina.
 
Naomba kujua kwa wale wataalamu wa haya mambo ni sawa kupewa majina ili kuweka kumbukumbu ya tukio hasa lakini ni kwanini hupewa majina ya wanawake tu.

Mfano;
Katarina
Irine
Anne
Pauline
Na Sasa pia tunaona jina la kike ni kwanini visiitwe wanaume au code name kama v.k 99 au P p 5?
Kila ukanda wanatumia namna yao ya kutoa majina,ukanda wa huku kwetu wanatoa majina kutokana na jinsia,huko maeneo ya mashariki ya mbali watoa kwa alphabetical order ya nchi zitakazo kumbwa.
Pia kuna bodi zinakaa kuchagua hayo majina sio mtu mmoja tu anakurupuka.

Pia wanatoa majina kama hivyo ili iwe rahisi kueleweka na kuwasiliana,imagine kimbunga kingeitwa Dysuadio ingekuaje.
 
Back
Top Bottom