Kwanini Umiliki Biashara badala ya kumiliki mfumo wa kibiashara?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,495
5,531
Habari za wakati huu;

Leo nataka tuzungumzi kitu kinaitwa "Business Model"aka mfumo au muundo wa Biashara.Wajasiriamali wengi huwa wanakama katika Biashara kwa kujikita zaidi kujenga Biashara badala ya kujenga Business Model.Ndio maana wengi hujikuta wakifanya bashara za kuigizana bila kuwa na aina yoyote ya ubunifu.

Business MODEL nini.Business ni mfumo kamili wa kibiashara ambao unaonesha aina ya bidhaa/huduma,aina ya wateja,jinsi faida itavopatikana na jinsi ya kuhakikisha kwamba biashara inakuwa endelevu.Ili nieleweke vizuri nitatumia mfano wa duka la reja reja.Kwa kawaida katika maduka ya rejareja faida huwa ni kati ya asilimia 10 hadi 40 kwa bidhaa nyingi huku wastani wa bei ya bidhaa ukiwa ni kati ya shingi 50 hadi sh 40,000 kwa kutegemea aina ya bidhaa na mahali duka lilipo.Kwa kawaida Muuzaji akifanya mauzo ya TZS 1,000,000 basi faida yake itakuwa ni kati ya TZS laki 4 hadi laki moja.

Wastani wa Mauzo katika duka la rejareja ni asilimia kumi ya stock iliyopo.Yaani kama Kwenye duka lako kuna mzigo wenye thamani ya Milioni 10 basi unatakiwa mauzo yako kwa siku yasipungue TZS 1,000,000 ili uweze kuendesha biashara yako vizuri.Kama mauzo yako yakiwa chini ya hapo inamaana kwamba utakuwa unaingia gharama kubwa sana za kuhifadhi mzigo ambazo sio za lazima na ambayo inaweza kupelekea kupata hasara katika biashara yako.

Najua hii business model niliyoelezea hapa sio kila mtu ataielewa ila ninachotaka kusema ni kwamba unapokuwa na mzigo mkubwa dukani kwako na kwa mwezi hauzungusihi mara tatu basi ujue kuwa unafanya biashara ya kuhifadhi mzigo(Warehousing) na sio kuuza.Kwa kila siku mzigo unapokaa dukani kwako unakuingizia gharama za nafasi,ulinzi,na tarehe ya expiry inakaribia.Ni muhimu sana ulitambue hilo ili uweze kufanya biashara kwa kujiamini.

Business MOdel yako lazima izingatie gharama zote na malipo unayopata wewe.Unaweza kuwa unauza TZS laki 5 kila siku ambayo kwa mwezi ni sawa na milioni 15 kama unafanya kazi kila siku.Ila kama mzgo wako ulioko stoo unathamni ya milioni 200 basi unafanya biashara kichaa.

Karibuni tujadili zaidi kuhusu Business Model na jinsi ambavyo unaweza kufaidika kwa kuwa na Business MOdel nzuri katika Biashara yako
 
Unaweza kuwa unauza TZS laki 5 kila siku ambayo kwa mwezi ni sawa na milioni 15 kama unafanya kazi kila siku.Ila kama mzgo wako ulioko stoo unathamni ya milioni 200 basi unafanya biashara kichaa.
Mkuu hapa umechemka maana kuna biashara ambazo stock inajipandisha bei kadri siku zinavyoendelea,pia kuna biashara ambazo kuna kipindi bidhaa huadimika hivyo ukiwa na stock unauza bei kwa kujipangia

Kwahiyo kama vipi kaa na hiyo business model yako ya hapo Tokyo
 
Business model ni ufatiliaji wa biashara yako ?
Ufuatiliaji
Mkuu hapa umechemka maana kuna biashara ambazo stock inajipandisha bei kadri siku zinavyoendelea,pia kuna biashara ambazo kuna kipindi bidhaa huadimika hivyo ukiwa na stock unauza bei kwa kujipangia

Kwahiyo kama vipi kaa na hiyo business model yako ya hapo Tokyo
Mkuu,assumption yako ni sahihi.Ila tukubaliane kwamba biashara ambayo inasubiri bidhaa iadimike ni biashara ya kuweka stoo kama ambavyo watu hununua mahindi na kuweka store kusubiri wakati wa high demand ndo wauze.Hio ni model pia ya Biashara cha muhimu ni wewe mfanyabiashara uelewe model yako ilivyo ili kuepuka unnecessary losses.
 
Mpaka hapo sijaona hiyo mifumo ya kibiashara, nilitegemea uelezee labda mifumo ni moja mbili ila sijaambulia chochote
 
Mpaka hapo sijaona hiyo mifumo ya kibiashara, nilitegemea uelezee labda mifumo ni moja mbili ila sijaambulia chochote
Mkuu,Nitafanya Mpango niongezee nyama zaidi.Ila kwa ufupi Mfumo wa Biashara unautengeneza wewe kwa kuzingatia aina ya biashara na malengo.Ukiangalia baadhi ya replies zangu utaona kuwa nimekuwa nikisisitiza kuwa mfumo wa biashara(Business Model inategemea na aina ya biashara,malengo na uwezo"Kwa mfano kama mtaji wako ni mdogo sana lazima uwe makini na issue ya gharama ambazo sio za lazima.Mfano badala ya kuwa na Duka Kariakoo unaweza kuwa unakuja na MZigo wako na Gari unapaki Kariakoo unauzia wateja wako kisha Jioni Unarudi nao Nyumbani.Hio ni Business Model ambayo inakuondolea Gharama ya Fremu Kariakoo.Swali la kujiuliza ni Je ukiwa na Fremu na Usipokuwa na Fremu Wapi unatengeneza Pesa zaidi?
 
Mkuu,Nitafanya Mpango niongezee nyama zaidi.Ila kwa ufupi Mfumo wa Biashara unautengeneza wewe kwa kuzingatia aina ya biashara na malengo.Ukiangalia baadhi ya replies zangu utaona kuwa nimekuwa nikisisitiza kuwa mfumo wa biashara(Business Model inategemea na aina ya biashara,malengo na uwezo"Kwa mfano kama mtaji wako ni mdogo sana lazima uwe makini na issue ya gharama ambazo sio za lazima.Mfano badala ya kuwa na Duka Kariakoo unaweza kuwa unakuja na MZigo wako na Gari unapaki Kariakoo unauzia wateja wako kisha Jioni Unarudi nao Nyumbani.Hio ni Business Model ambayo inakuondolea Gharama ya Fremu Kariakoo.Swali la kujiuliza ni Je ukiwa na Fremu na Usipokuwa na Fremu Wapi unatengeneza Pesa zaidi?
Mkuu ubarikiwe, hapo nimekuelewa kabisa, Asante sana
 
Kwa sasa mleta mada hujui business model ni nini.

Kwa kifupi ni kwamba business model ni namna gani biashara yako inaleta thamani kwa wateja na kukupa mapato na faida. Mifano rahisi sana ni:
1. Utengenezaji (na Uuzaji) wa bidhaa
2. Usambazaji wa bidhaa
3. Uuzaji wa bidhaa kwa bei ya jumla
4. Uuzaji bidhaa kwa rejareja
5. Huduma ya kujiunga na kulipia kwa kila kipindi fulani (Subscriptions)

Na kadhalika. Yaani unazalisha XYZ au Unafikisha ABC au unapatia RST kisha mteja analipia.

So duka la Mangi business model yake ni Kuuza Bidhaa kwa rejareja (Retail); ananunua bidhaa mbalimbali kwa bei ya jumla ambayo ni ndogo na kisha anaziuza kwa bei ya rejareja ambayo ni kubwa kidogo na hivyo kumpa faida.

Viwanda vya kutengeneza magari, mabati, matofali, saruji, mafuta ya kula na kadhalika Business model yao ni kutengeneza hizo bidhaa na kuziuza kwa bei yenye faida ndani yake; yaani bei ya kuuzia = Gharama zao zote + Faida.

So mfanyabiashara kuelewa business model yake maana yake ni kwamba ajue yeye anapeleka thamani gani kwa wateja wake (Bidhaa, Huduma, Utaratibu, Mahali, Bei, Promosheni nk) ni kisha anapataje mapato na faida. That SIMPLE!
 
Kwa sasa mleta mada hujui business model ni nini.

Kwa kifupi ni kwamba business model ni namna gani biashara yako inaleta thamani kwa wateja na kukupa mapato na faida. Mifano rahisi sana ni:
1. Utengenezaji (na Uuzaji) wa bidhaa
2. Usambazaji wa bidhaa
3. Uuzaji wa bidhaa kwa bei ya jumla
4. Uuzaji bidhaa kwa rejareja
5. Huduma ya kujiunga na kulipia kwa kila kipindi fulani (Subscriptions)

Na kadhalika. Yaani unazalisha XYZ au Unafikisha ABC au unapatia RST kisha mteja analipia.

So duka la Mangi business model yake ni Kuuza Bidhaa kwa rejareja (Retail); ananunua bidhaa mbalimbali kwa bei ya jumla ambayo ni ndogo na kisha anaziuza kwa bei ya rejareja ambayo ni kubwa kidogo na hivyo kumpa faida.

Viwanda vya kutengeneza magari, mabati, matofali, saruji, mafuta ya kula na kadhalika Business model yao ni kutengeneza hizo bidhaa na kuziuza kwa bei yenye faida ndani yake; yaani bei ya kuuzia = Gharama zao zote + Faida.

So mfanyabiashara kuelewa business model yake maana yake ni kwamba ajue yeye anapeleka thamani gani kwa wateja wake (Bidhaa, Huduma, Utaratibu, Mahali, Bei, Promosheni nk) ni kisha anapataje mapato na faida. That SIMPLE!
Uko Sahihi,Isipokuwa umesema sijui kisha ukasema najua.Kwa maelezo yako ni kwamba unajua business model ni nini ingawa pia hujaingia kwa kina.Mfano niliotua kwa duka la Mangi unaonesha kuwa hata kati ya Mangi mmoja na Mangi mwingine kunaweza kuwa na tofauti katika kiwango cha faida na tija iwapo tu kutakuwa na tofauti katika Business Model in a deeper sence.Mifano uliyotaja ni Business model in simple sense.
 
Back
Top Bottom