Kwanini Twiga awe nembo ya Tanzania?

Kwanini Twiga awe nembo ya Tanzania?

chifu77

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2014
Posts
902
Reaction score
597
Heshima kwenu wakuu.

Mataifa kadhaa duniani wamechagua baadhi wa wanyama kuwa nembo za nchi zao. Mfano Bald eagle (tai) ni nembo ya Marekani. Tai ni ndege anayepaa katika anga za juu sana kuliko ndege wote. Akiwa huko jicho lake linaweza kuona mbali hata mzoga wa sungura uliopo ardhini. Waamerika wanadai kwao tai anawakilisha nguvu, uhuru, akili na ujasiri wa kuona mbali.

Eagle1.jpg




Turudi hapa Tanzania. Mnyama wetu wa Taifa ni Twiga. (Giraffe). Neno giraffe limetokana na neno la kiarabu (xirefa) lenye maana ya anayetembea kwa maringo.

wt_giraffeneck_free.jpg


Je, kwanini wazee wetu waliamua kumchagua twiga?
Je, mchakato wa kuamua mnyama yupi atumike ulichukua miaka mingapi?
Je, kulikuwa na wanyama wengine au ndege waliopendekezwa zaidi ya twiga?
Je, watoto na wajukuu wetu wakitaka kujua habari kama hizi watazipata wapi? watazisoma wapi?

Nawasilisha.
 
Heshima kwenu wakuu.
Mataifa kadhaa duniani wamechagua baadhi wa wanyama kuwa nembo za nchi zao. Mfano Bald eagle(tai) ni nembo ya marikani. Tai ni ndege anayepaa katika anga za juu sana kuliko ndege wote. Akiwa huko jicho lake linaweza kuona mbali hata mzoga wa sungura uliopo ardhini. Waamerika wanadai kwao tai anawakilisha nguvu, uhuru, akili na ujasiri wa kuona mbali. View attachment 407474

Turudi hapa Tanzania. Mnyama wetu wa Taifa ni Twiga. (Giraffe). neno giraffe limetokana na neno la kiarabu (xirefa)lenye maana ya anayetembea kwa maringo.
View attachment 407475
Je kwa nini wazee wetu waliamua kumchagua twiga?
Je mchakato wa kuamua mnyama yupi atumike ulichukua miaka mingapi?
Je kulikuwa na wanyama wengine au ndege waliopendekezwa zaidi ya twiga?
Je watoto na wajukuu wetu wakitaka kujua habari kama hizi watazipata wapi? watazisoma wapi?

Nawasilisha.
Wenu katika ujenzi wa Tz ya viwanda viiiiingi.

Swali zuri sana,safi muulizaji wengi tupo gizani juu ya hili...
 
Katika kusahihisha sio mamabu zetu walio chagua huyo twiga bali ni mkoloni. Alifanya hivyo kwa nchi zote za Afrika mashariki Kenya wakiwa na Simba na Uganda Crane(Korongo). Angalia hii bendera ya Tanganyika kabla ya uhuru

tz~tgclr.gif
 
Na ndio maana fikra na mambo yetu yapo kitwiga twiga tuu, mambo hayaendi kabisa.
Hili jambo lina maana kubwa sana kwenye ulimwengu wa roho ila najiuliza Wamarekani nao wangefanya kumchagua Twiga kuwa mnyama wao wa taifa na sisi Tai je mambo yangelikua tofauti??
 
LABDA WABADILI N'A WAWEKE MNYAMA SIMBA LABDA HAO WANAO KUJA KUTUPORA MALI WATAOGOPA.......

OVA
Aisee bora simba ni mfalme wa nyika. Akiunguruma wengine kimyaaa.. sasa twiga yeye kutembea kwa maringo tuu... halafu hanaga haraka.
 
Aisee bora simba ni mfalme wa nyika. Akiunguruma wengine kimyaaa.. sasa twiga yeye kutembea kwa maringo tuu... halafu hanaga haraka.
Tumdai nembo awe simba basi mkuu

Ova
 
Labda wanaibwa sana, wanahisi miaka ijayo watapungua au kutoweka hivyo wanawachora ili kubaki nao kwenye kumbukumbu ya picha
Ni sawa ila kwa sasa wanyama ambao wanatangazwa kwamba wameibwa sana ni faru, mbwa mwitu na duma. Hawa twiga wahejaa maporini balaa
 
Back
Top Bottom