Kwanini tung'ang'anie vyeti tusinganganie madawa?

mtoa uzi ujue kabisa kuna watu wamefungwa, wengine wamepata shock na kufa, wengine wamefukuzwa kazi kisa wamegushi, sawa tuseme waliokufa washatangulia mbele za haki hawa waliofungwa na kufukuzwa nao warudishwe makazini na haki zao wapewe, kwani hatukuwahi kusikia wameua au kashfa na walikuwa wanafanya kazi kwa uadilifu kabisa, kama atazidi kumkingia kifua watz wote bila kujali itikadi za vyama hawatakaa kimya,
 
Kama unafikiri Makonda ana pambana madawa ya kulevya umepotoka,Makonda ana pambana na watu binafsi wanaopambana na madawa kulevya wapo na wanapambana kisayansi na hawana pyeepyepye kama za Makonda wako huyo,na kazi ya kupinga madawa ya kulevya siyo ya leo ilianza kabla hata Makonda hajaliona jua.
 
Ni kama vile huelewi jambo ulilolileta hapa!
 
vijana wengi tumejaa chuki juu ya vijana wenzetu, hatuko tayari kusupport jambo analofanya kijana mwenzio, sawa kakosea kwasababu yeye sio mungu. lakini tuwe postive kidogo
 
Hivi kumbe Mbowe, Wema, Masogange na T. I. D. Ndio watu wenye nguvu Tanzania kiasi kwamba walikuwa na uwezo wa kuipangia ccm mgombea wa kumsimamisha kugombea urais? Inamaana hao ndo walimweka Mwinyi, Mkapa na Kikwete?
 
Kwani umeambiwa issue ya madawa imeisha mbona inaendelea!? Hukusikia Ridhwani kikwete kahojiwa!? Issue haiko Mikononi mwa Daudi anymore Huyo mtu alitaka kuitumia kwa manufaa yake binafsi hakuwa na nia njema hata kidogo!!
 
Wauza unga ndo wanaomzushia makonda wanataka sisi tudili na vyeti vya makonda huku wao wakipitisha unga airport
 
Watanzania tuamke tumuunge mkono makonda kudili na madawa ya kulevya sio jambo dogo
 
Kwa akiri za kutengeneza video ya uongo na kulazimisha irushwe Clouds TV kwa lengo la kumchafua Mtu. Akiri hizo zitashindwa kusema [HASHTAG]#Forgo[/HASHTAG] anauza madawa ya kulevya? Kwa chuki tu, au visasi?

Kama jinga hili lilikuwa na nia thabiti ya kuzui na kupambana na wauza madawa ya kulevya basi lisingekuwa linataja watuhumiwa jumanne na kuwataka walipoti polisi ijumaa.... Hata kama babaako ni muuzaji wa madawa, kwa hivo utamkamata?

Anachokifanya sasa kamishina kipo kisheria na ilipaswa kuwa hivyo tangu awali. Daudi alikuwa anatafuta umaarufu na vile ndo muamuzi wa Rais Ikulu basi kwa akiri mgando kama zake mtamuona alikuwa sahihi.


Vita haiwezi kuisha, na wauzaji inabidi wakamatwe ikiwezekana wanyongwe iwe fundisho, sio unatukamatia Chid Benz, Ray C, TID af unajitikisa matako et "Mbabe wa Vita", unakuja kuwataja akina Gwajima then inabainika hawauzi wala hawatumii, What the hell? Unamsafishaje huyo? Na uliwezaje kujiridhisha kumtaja bila kuwa na kidhibiti chochote? tunahitaji sheria ifuatwe na kuwe na kweli,haki na usawa pasipo kupakaziana kisa tulipigana vikumbo uchochoroni.
 
Nimeipenda hiyo dat's true kwnn vyeti not madawa wht th rsn bhnd?
 
Watu wanataka kutusahaulisha issue ya madawa na tung'ang'anie vyeti ili tu wauza unga wapate kujinasua. Tukumbuke, ni familia nyingi sana chovu zilinufaika na hii biashara na sasa wanahaha ndiyo maana wanashikilia bango story ya vyeti.
 
Mimi ninachoamini ni kwamba, MTANDAO wa madawa ya kulevya ndio unaofanya kazi ya kueneza propaganda za vyeti ili kujaribu kuficha maovu yao.
Hoja yangu ya msingi ni kwamba, Paul Makonda ameteuliwa muda mrefu sasa kuwa mkuu wa mkoa, hivyo basi;
(1)Kwa nini issue hii ya vyeti isingeibuliwa tangu alipokuwa ametoka tu kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa?
(2)Kwa nini issue za vyeti ziibuliwe mara tu baada ya kutajwa kwa watuhumiwa wa madawa ya kulevya?
 
Bashite acha porojo weka vyeti mezani yaishe!
 
Kwani mdaiwa wa vyeti ana uhusiano gani na vita ya madawa???

Vita inapiganwa na wenye jukumu lao, huyu yeye halimuhusu.
 
Mkuu randez haijalishi nilikuwa suala la muda tu halijafika na bado halihalalishi yeye kutochukuliwa hatua ndio maana tunasema za mwizi arobaini.kukingiwa kifua ni refa kuharibu game mzima kwasabu dhaifu iweje refa kawatoa nje kwa kadi nyekundu timu moja huku akimwacha mchezaji wa timu pinzani afanye faulo za ajabu uwanjani refa anapigiwa kelele kuwa anapendelea yeye anajibu asipangiwe cha kufanya na kumwambia huyo mcheza hovyo aendelee kucheza anavyotaka hiyo sio fair.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…