Kwanini tunavaa pete ya ndoa mkono wa kushoto?

agudev

Member
Apr 5, 2016
76
122
Habari zenu wanaJF na hongereni na majukumu ya kuendeleza taifa hili.

Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, nimekuwa nikitatizwa na hili swali kichwani na nimejaribu kuuliza watu mbalimbali hasa Wakristo waliooa, majibu niliyopata mpaka sasa kusema kweli hayajaniridhisha kwani inaonekana watu huvaa pete mkono wa kushoto kwa vile kila mtu anafanya hivyo. Je uvaaji wa pete hii hauna maana yoyote?

Naangalia namna mkono wa kushoto unavyochukuliwa katika jamii zetu kama mkono usiofaa, mkono mchafu na mkono wa chooni, basi kama hili ni kweli iweje tuwe tunautumia mkono kuweka ishara ya uaminifu na upendo. Ndoa ni kiapo na kifungo chetu cha upendo na uaminifu na upendo mbele ya Mungu na mwenza wetu, ni ishara ya kukubali kujifunga maisha yetu na kuishi maisha ya nidhamu ya kujizua tamaa zetu za mwili, kujitoa kwa kushirikiana na mwenza wetu kuweza kujenga jambo lililo kubwa kuliko sisi ambalo ni familia. Ikiwa hivi vyote ni kweli, kwa nini basi tunaweka ishara inayowakilisha uzito wa maamuzi ya maisha yetu mkono ambao tunauchukulia kama mkono najisi?

Kawaida ni mwiko kabisa kutumia mkono wa kushoto kufanyia vitu muhimu; huruhusiwi kula kwa mkono wa kushoto, huruhusiwi kusali kwa mkono wa kushoto, huruhusiwi kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto, kusalimia kwa mkono wa kushoto, kutoa sadaka kwa mkono wa kushoto n.k, ina maanisha ndoa ina thamani ndogo sana kuliko namna ya kula chakula, kutoa salamu n.k?
 
You my friend upo zama za mawe, so old fashioned and outdated.

Kwa taarifa yako, 10% ya watu wote duniani wanatumia mkono wa kushoto kufanya mambo yote unayoyaita "muhim"

Hakuna kiungo cha binadam kisichofaa.

Kuhusu Pete ni Dhana ya matumizi ya mkono wa kulia kwa vitu kama kula nk... na ndio maana mkono wa kushoto unavishwa Pete, saa na urembo.

Mengine hayana umuhimu sana, kuvaa Pete ni alama ya upendo na uamunifu, wengine kisiasa, wengine ulozi tu, na wapo wanaoichukulia kiimani, wapo wanaovaa tu kuepuka bla bla za jamii.
 
Habari zenu wanaJF na hongereni na majukumu ya kuendeleza taifa hili.

Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, nimekuwa nikitatizwa na hili swali kichwani na nimejaribu kuuliza watu mbalimbali hasa Wakristo waliooa, majibu niliyopata mpaka...
Mkuu,
1. Anatomia ya binadamu inaonesha, kwa kawaida, sehemu kubwa ya moyo ipo upande wa kushoto.

2.Moyo wa binadamu unatumika kuonesha upendo.

3. Hapo zamani (kabla anatomia ya binadamu haijafahamika vizuri), waliamini kuwa kuna mshipa mmoja wa damu unatoka moja kwa moja kutoka kwenye moyo mpaka kwenye kidole cha nne cha mkono(kutoka kidole gumba) wa kushoto, na kurudi kwenye moyo moja kwa moja bila kutoa matawi.

Kwa sababu hizo wakaona njia bora ya kuonesha upendo ni kumvisha kito cha thamani yule umpendaye kwenye kidole chenye uhusiano wa moja kwa moja na moyo(kiungo kiashiriacho upendo).
 
Habari zenu wanaJF na hongereni na majukumu ya kuendeleza taifa hili.

Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, nimekuwa nikitatizwa na hili swali kichwani na nimejaribu kuuliza watu mbalimbali hasa Wakristo waliooa, majibu niliyopata mpaka sasa kusema kweli hayajaniridhisha kwani inaonekana watu huvaa pete mkono wa kushoto kwa vile kila mtu anafanya hivyo. Je uvaaji wa pete hii hauna maana yoyote?

Naangalia namna mkono wa kushoto unavyochukuliwa katika jamii zetu kama mkono usiofaa, mkono mchafu na mkono wa chooni, basi kama hili ni kweli iweje tuwe tunautumia mkono kuweka ishara ya uaminifu na upendo. Ndoa ni kiapo na kifungo chetu cha upendo na uaminifu na upendo mbele ya Mungu na mwenza wetu, ni ishara ya kukubali kujifunga maisha yetu na kuishi maisha ya nidhamu ya kujizua tamaa zetu za mwili, kujitoa kwa kushirikiana na mwenza wetu kuweza kujenga jambo lililo kubwa kuliko sisi ambalo ni familia. Ikiwa hivi vyote ni kweli, kwa nini basi tunaweka ishara inayowakilisha uzito wa maamuzi ya maisha yetu mkono ambao tunauchukulia kama mkono najisi?

Kawaida ni mwiko kabisa kutumia mkono wa kushoto kufanyia vitu muhimu; huruhusiwi kula kwa mkono wa kushoto, huruhusiwi kusali kwa mkono wa kushoto, huruhusiwi kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto, kusalimia kwa mkono wa kushoto, kutoa sadaka kwa mkono wa kushoto n.k, ina maanisha ndoa ina thamani ndogo sana kuliko namna ya kula chakula, kutoa salamu n.k?
The ancient Romans believed that the fourth finger of the left hand had a vein that ran directly to the heart and so chose to wear the ring as a symbol of love on this finger.

Warumi wa kale waliamini kwamba kidole cha nne cha mkono wa kushoto kilikuwa na mshipa unaoenda moja kwa moja kwenye moyo na hivyo kuchagua kuvaa pete kama ishara ya upendo kwenye kidole hiki.
 
You my friend upo zama za mawe, so old fashioned and outdated.

Kwa taarifa yako, 10% ya watu wote duniani wanatumia mkono wa kushoto kufanya mambo yote unayoyaita "muhim"

Hakuna kiungo cha binadam kisichofaa.

Kuhusu Pete ni Dhana ya matumizi ya mkono wa kulia kwa vitu kama kula nk... na ndio maana mkono wa kushoto unavishwa Pete, saa na urembo.

Mengine hayana umuhimu sana, kuvaa Pete ni alama ya upendo na uamunifu, wengine kisiasa, wengine ulozi tu, na wapo wanaoichukulia kiimani, wapo wanaovaa tu kuepuka bla bla za jamii.
Kwa taarifa yako, 10% ya watu wote duniani wanatumia mkono wa kushoto kufanya mambo yote unayoyaita "muhim""
Kitu gani nilichosema hapo kinatokea zama za mawe au kipo outdated? Sijaongelea hiki kitu kwa watu wote duniani (halafu hata hii 10% unayoisema sijui umeitolea wapi?). Kila jamii duniani ina namna ya vitu inavyoamini kuwa miiko na visivyo ruhusiwa katika jamii hiyo, miiko na makatazo yaliyopo katika jamii moja sio lazima kuwa mwiko katika jamii nyingine wala miiko ya jamii moja haiwezi kutumika kama standard ya kupima jamii zingine na kuziita "Old fashioned and outdated".
Mfano jamii nyingi kutemea mtu mate ni alama ya dharau lakini jamii kama za Wachaga kutemea mtu mate ni alama ya baraka, huwezi kuita hii "Old fashioned" kwa vile eti ipo tofauti na namna watu wengine wanavyofanya.
Hakuna kiungo cha binadam kisichofaa.
Ukiongelea kiungo kama sehemu ya mwili kweli hakuna kiungo kisichofaa kwa sababu kila kimoja kipo kufanya kazi yake lakini tukirudi tena, mkono wa kulia unapewa uzito kuliko mkono wa kushoto katika jamii ya yetu (hapa Tanzania). Kama huamini hili jaribu kutoa kumpa mtu/kupokea kwa mkono wa kushoto, kusalimia kwa mkono wa kushoto, kusali kwa mkono wa kushoto halafu utoe hii sababu ya "Hakuna kiungo cha binadam kisichofaa". Wengi tumekuzwa hivi kuuona mkono wa kushoto kama mkono usiofaa, ndio miiko katika jamii zetu. Unaweza kusema hivi vitu sio "scientific" lakini hutupimi tamaduni na imani za watu kwa "science", jamii husika inaamua yenyewe vitu gani vinafaa na vipi havifai.
Kuhusu Pete ni Dhana ya matumizi ya mkono wa kulia kwa vitu kama kula nk... na ndio maana mkono wa kushoto unavishwa Pete, saa na urembo.
Unarudi pale pale tena, "Dhana ya matumizi ya mkono wa kulia kwa vitu kama kula n.k", unafikiri ni kwa nini ni mkono wa kulia unatumika kula na sio kushoto ikiwa "Hakuna kiungo cha binadam kisichofaa"? pia unaongelea upande mmoja tu wa mkono wa kulia...upande wa pili, mkono wa kushoto hutumika kujisafishia chooni, je uchafu upi ni afadhali? uchafu wa chakula au uchafu wa chooni?

Mengine hayana umuhimu sana, kuvaa Pete ni alama ya upendo na uamunifu, wengine kisiasa, wengine ulozi tu, na wapo wanaoichukulia kiimani, wapo wanaovaa tu kuepuka bla bla za jamii.
Mada ya uzi huu haijaongelea uvaaji wa pete za kisiasa au ulozi, ninaongelea uvaaji wa pete kama ishara ya kifungo cha ndoa. Sijajua unaamini nini kuhusu pete lakini kama huamini kuna umuhimu wowote wa pete ya ndoa basi sidhani kama ni mtu sahihi wa kujibu namna gani inabidi kuvaliwa, lengo langu katika uzi huu ni kujua kutoka kwa watu wengine kama mimi wanaoamini katika alama na uzito uliopo kwenye pete ya ndoa.
 
Mkuu,
1. Anatomia ya binadamu inaonesha, kwa kawaida, sehemu kubwa ya moyo ipo upande wa kushoto.

2.Moyo wa binadamu unatumika kuonesha upendo.

3. Hapo zamani (kabla anatomia ya binadamu haijafahamika vizuri), waliamini kuwa kuna mshipa mmoja wa damu unatoka moja kwa moja kutoka kwenye moyo mpaka kwenye kidole cha nne cha mkono(kutoka kidole gumba) wa kushoto, na kurudi kwenye moyo moja kwa moja bila kutoa matawi.

Kwa sababu hizo wakaona njia bora ya kuonesha upendo ni kumvisha kito cha thamani yule umpendaye kwenye kidole chenye uhusiano wa moja kwa moja na moyo(kiungo kiashiriacho upendo).
Nakubaliana na point yako ya kwanza na ya pili lakini hii ya tatu inaonesha wengi wetu tunavaa pete mkono wa kushoto kwa mkumbo tu na hakuna maana yoyote nyuma yake
 
Sijaona hata mmoja aliesema kuwa huo ni utumwa wa kuwaabudu na kuwatukuza waleta dini kama tu ulivyoutumwa mwingine.
 
Mkuu suala la kuvaa pete mkono wa kushoto ni la karibu dunia nzima ila hilo suala la mkono wa kushoto kuwa najisi sijui mchafu ni la jamii ya nchi fulani tu

Sasa huwezi kujadili suala linalohusu utaratibu wa karibu dunia nzima kwa kutumia imani za jamii ya watu fulani tu

Kama ulivyosema si watu wote wana hizo imani kuhusu mkono wa kushoto, ila ni watu karibu wote duniani huvaa pete mkono wa kushoto wanapofunga ndoa, hasa ukizingatia hizo imani zinazohusu mkono wa kushoto ni dhana potofu tu zilizotungwa na zisizo na uhalisia wowote
 
Back
Top Bottom