Kwanini tunapeleka wanajeshi wetu badala ya Mwenge?

Kwanini tunapeleka wanajeshi wetu badala ya Mwenge?

Mwenge ni kuwapumbaza watanzania tu, hakuna cha amani wala utulivu ukaletwa na mwenge
Labda ni ushirikina tu huo.
Kuamini kuwa moto wa mafuta unaweza kuleta amani ni sawa na kuabudu sanamu.
 
Mwenge ni ibada ya sanamu na kafara ambayo nchi inatoa kila mwaka kwa ajili ya amani,kumbuka hakuna ufalme unaofitin ufalme mwenzake yaani ile ni Ibada ya SANAMU full na kamj wewe una dini usishiriki huo uchawi
 
Umenifanya nicheke peke yangu. Ahahahahahahahaha. Kama unaamini mwenge unalinda taifa nakushauri nyumba yako usiweke geti wala milango wewe weka mapazia tu ila usisahau ndani ukutani kubandika picha za mwenge.
 
Mwenge nadhani ni dhana mficho ya Taifa.! "sisi tunataka kuwasha Mwenge na kuuweka juu ya mlima kilimanjaro ili ulete tumaini........"..
Nukuzi kutoka katika Maneno ya Mwl Jk nyerere.

Natumai kila Taifa lina dhana yake mficho kwa ulinzi wa ama imani au Utaifa wao.! ukiaenda usie husika ukajaribu kufikiri waweza ona ni kama upuuzi tu.
mathalani kifimbo cha malkia kwenye olimpiki kina sabbu gani yakuzungushwa kwenye Nchi za madola?
au kile kinachoitwa mwenge wa olimpiki
ni dhana yake?

Ukienda China kuna jambo wanaliamini katika dragon toka kizazi kimoja kwenda kingine ukienda mgeni je dragon lao lina jambo lolote muhimu kwako?

Ukiangalia kwa mtazamo wa pesa utaona ni hasara lakini ukiangalia kwa Dhani ya Uhai wa Imani ya Kizalendo kwa Taifa ni kubwa sana.! Kwa kizazi kijacho labda tu ukiwa sio Mtanzania wa kweli jambo hilo linaweza kukusumbua.

Amani katika mataifa yenye machafuko. Huenda ni jambo la kisiasa zaidi ya kimani. Mathalani kulikuwa na haja gani ya Libya kuingia kwenye machafuko ?
Je UN hawakujua madhara ya Libya kwa siku za Mbele?
au Machafuko ya Syria UN hawajui sabbu za machafuko hayo?
the same DRC congo je UN hawajui..?

La hasha ni miradi yao wanayoitengeneza kwa manufaa yao wenyewe so sio uimara wa jeshi unaohitimisha migogoro katika Nchi zenye machafuko ila ni dhana. Iliyopandwa ndani ya fikra zao.!
ambayo yaweza kupandwa kwa kuaminishwa kuwa hawa wanapendelewa kuliko hawa na wale wananyanyaswa kuliko wale.
Wakishaanza kushambuliana walio wachonganisha wanapata wanachokitaka.!

Hivyo dhana ya Mwenge wa uhuru ni kuwakumbusha watanzania umoja wao na usawa wao ambao waweza kuondolewa na baadhi ya watu kwa kisingizio cha kisiasa.! Ambacho ukichunguza chanzo chake halisi sio ndani Ya Taifa letu..

"Kuwasha Mwenge na kuuweka Juu ya mlima kilimanjaro"

RIP.. Jk Nyerere..
RIP ... Nyirenda..

Kizazi kijacho kinachotafuta ukweli kitagundua siri hii.
Acha porojo mwenge hauna faida yoyote.
Mwenge hauko audited. Mahesabu ya mwenge hayakaguliwi.
Bajeti ya Mwenge haipitishwi Na bunge.
Mwenge ni kitega uchumi cha CCM Na mabosi wake.
Mwenge ni laana Na chukizo mbele za Mungu.
Isaya 50:11
 
Panapo tokea machafuko nchi mbalimbali Duniani, Tanzania imekuwa mstari wa mbele kupeleka wanajeshi wake wakalinde Na kuboresha amani.
Mazingira hayo Siyo rafiki. Ni nusu Vita kama sio Vita kamili.
Kwenye mission mbalimbali tumepoteza askari wetu ambao ni tegemeo kwa Taifa Na familia zao.
Tunao Mwenge wa Uhuru. Na Tunaambiwa amani Na utulivu vilivyopo nchini ni matokeo ya kuukimbiza mwenge nchi nzima.
Kwanini tusiukimbize mwenge kwenye nchi zenye machafuko kama Sudan Kusini, Congo etc ili wawe Na amani Na hivyo kuwaokoa askari wetu Na hata wenyeji wa hizo nchi?
Maoni Na majibu yenu ni muhimu.
swissme, BAK, mshana jr, Pascal Mayalla, Nyani Ngabu, Mzee Mwanakijiji, GuDume, CCM, CHADEMA
Bujibuji unataka bifu na mimi et...kwanini hujanitaja na mimi au kwasababu sijafika chuo?
 
Panapo tokea machafuko nchi mbalimbali Duniani, Tanzania imekuwa mstari wa mbele kupeleka wanajeshi wake wakalinde Na kuboresha amani.
Mazingira hayo Siyo rafiki. Ni nusu Vita kama sio Vita kamili.
Kwenye mission mbalimbali tumepoteza askari wetu ambao ni tegemeo kwa Taifa Na familia zao.
Tunao Mwenge wa Uhuru. Na Tunaambiwa amani Na utulivu vilivyopo nchini ni matokeo ya kuukimbiza mwenge nchi nzima.
Kwanini tusiukimbize mwenge kwenye nchi zenye machafuko kama Sudan Kusini, Congo etc ili wawe Na amani Na hivyo kuwaokoa askari wetu Na hata wenyeji wa hizo nchi?
Maoni Na majibu yenu ni muhimu.
swissme, BAK, mshana jr, Pascal Mayalla, Nyani Ngabu, Mzee Mwanakijiji, GuDume, CCM, CHADEMA
Mkuu Buji, umenikumbusha Mwenge: Ni Mwanga Tu Au Kuna Uvumba Fulani Unafukizwa Ili Kupumbaza Watanzania? Is it Justified?.
Mambo ya uvumba na mavumba ni territorial na directional, yaani yana mipaka na kulengeshwa, walengwa huwa ni Watanzania walio ndani ya mipaka ya nchi yetu, ukiishatoka nje ya mipaka yetu, uvumba ule haufanyi tena kazi, ndio maana wengi wa Watanzania waliopo nje, wanajitambua, na ndia sababu tunaogopa kutoa uraia pacha kwa diaspora wetu!, mimi nilishauri tuwape tuu uraia pacha ila tuwakataze wasishiriki siasa!, kumbe haina haja kuogopa kutoa uraia pacha, tuwape uraia pacha na kuwaruhusu kushiriki siasa ili siku wakirudi Tanzania, lazima kwanza wafanyiwe initiations za kutakaswa na moshi wa Mwenge, hivyo wafanane na sisi tuliofukizwa tukafukazika na ndio maana tumetulia tuli.

P.
 
Hivi mwenge una uhusiano gani na kondomu??
 
Mkuu Buji, umenikumbusha Mwenge: Ni Mwanga Tu Au Kuna Uvumba Fulani Unafukizwa Ili Kupumbaza Watanzania? Is it Justified?.
Mambo ya uvumba na mavumba ni territorial na directional, yaani yana mipaka na kulengeshwa, walengwa huwa ni Watanzania walio ndani ya mipaka ya nchi yetu, ukiishatoka nje ya mipaka yetu, uvumba ule haufanyi tena kazi, ndio maana wengi wa Watanzania waliopo nje, wanajitambua, na ndia sababu tunaogopa kutoa uraia pacha kwa diaspora wetu!, mimi nilishauri tuwape tuu uraia pacha ila tuwakataze wasishiriki siasa!, kumbe haina haja kuogopa kutoa uraia pacha, tuwape uraia pacha na kuwaruhusu kushiriki siasa ili siku wakirudi Tanzania, lazima kwanza wafanyiwe initiations za kutakaswa na moshi wa Mwenge, hivyo wafanane na sisi tuliofukizwa tukafukazika na ndio maana tumetulia tuli.

P.
Hayo mavumba Na mafusho hayana kinga? Je yana faida gani kwa ustawi wa Taifa lililo imara kiulinzi, kiusalama, kiuchumi Na kiutamduni?
Mavumba na mafusho Haya ni faida kwa wahindi, wachina Na wageni wengine. Watanzania tumegeuka watumwa ndani ya nchi yetu, rasilimali zetu zinaliwa Na wageni kwasababu ya UPUMBAVU wa mafusho ya mwwnge
 
Muache mzee wa watu,usimsumbue.
Mchawi mwenzio.

Huyu Forojo Ganze,alikuwa ni mmoja kati ya wazee waliotumwa kufanya zindiko la nchi baada ya uhuru kule bagamoyo, walipewa kazi ya kuhakikisha rais aliye madarakani hapingwi na mtu yeyote(Mwl.Nyerere), zindiko hilo lilifanyika bagamoyo ktk moja ya mashimo yanayopatikana wilayani hapo,zoezi hilo lilienda sambamba na kumuuliza shetani na malaika zake ni jambo gani lifanyike ili Tanzania iendelee.
Forojo Ganze ndiye mtu pekee aliyeingia ktk hilo shimo kwaajili ya kuuliza, alikaa huko kwa muda wa siku 10 huku akiwa amewaacha wenzake nje wakimgoja atakuja na jibu gani ili wakampatie rais na wazee wa Dar es salaam,kilichoshangaza siku ya kumi na moja alitoka akiwa hoi hajiwezi akiwa kama mtu aliyepigwa na alikuwa anaongea lugha isiyofahamika,wenzake wakiwa wanaongozwa na Yahaya Hussien walimbeba hadi ikulu Dar es salaam na walipomfikisha mbele ya mwalimu Nyerere alitamka maneno hayo yanayohusu mwenge kwa kiswahili kisha akanyoosha juu mkono wake wa kulia ambao tayari ulikuwa umeandikwa namba hii 115,kisha akakata roho.
Baada ya mazishi mwalimu aliyafanyia kazi maneno ya Forojo Ganze akaanzisha mwenge wa uhuru bila kujua ulikuwa na maana gani, baada ya hapo aliwagiza yahya Hussein atafasiri maana ya ile namba 115, kama kawaida ya shehe Yahaya alitafasiri akamwambia kuwa namba hiyo inamaanisha "utakufa ukiwa na umri wa miaka 77 na taifa la Tanzania kwa kipindi hicho litakuwa na umri wa miaka 38.
Hii inamanisha ukichukua 77 umri wa mwalimu jumlisha 38 umri wa taifa utapata 115, na hii ndivyo ilivyokuwa, mwaka 1999 mwalimu alikufa akiwa na miaka 77 na taifa lilikuwa na miaka 38 ya uhuru (77+38=115) pia utamaduni wa rais kuongea na wazee wa Dar es salaam unaendelea hadi sasa na wamekuwa na maamuzi ya kitaifa na husikilizwa sana wanachokisema,mbona haijawahi kutokea rais akaongea na wazee wa bukoba jambo la kitaifa?,zindiko la bagamoyo linafanya kazi.
Safu hii ilikuwa ya watu 5 ambao ni.
1. Mzee Ramadhan, alizaliwa mwaka 1920,
2. Ally Tarazo(1929),
3. Komwe wa Komwe(1918),
4. Sheihe Yahya Hussein(1925),na
5. Forojo Ganze (1902)
 
Panapo tokea machafuko nchi mbalimbali Duniani, Tanzania imekuwa mstari wa mbele kupeleka wanajeshi wake wakalinde Na kuboresha amani.
Mazingira hayo Siyo rafiki. Ni nusu Vita kama sio Vita kamili.
Kwenye mission mbalimbali tumepoteza askari wetu ambao ni tegemeo kwa Taifa Na familia zao.
Tunao Mwenge wa Uhuru. Na Tunaambiwa amani Na utulivu vilivyopo nchini ni matokeo ya kuukimbiza mwenge nchi nzima.
Kwanini tusiukimbize mwenge kwenye nchi zenye machafuko kama Sudan Kusini, Congo etc ili wawe Na amani Na hivyo kuwaokoa askari wetu Na hata wenyeji wa hizo nchi?
Maoni Na majibu yenu ni muhimu.
swissme, BAK, mshana jr, Pascal Mayalla, Nyani Ngabu, Mzee Mwanakijiji, GuDume, CCM, CHADEMA
Mambo ya ulinzi hayahojiwi.....hya wee shairi yako...anko....
Kama hujaoa au huna watoto wengi
Sema...upesi nikupe Dada zangu 3 uwajaze mimba upesi ...ili jin lako tubaki nalo
 
Back
Top Bottom