Kwanini Tanzania Walimu wenye Masters hawatambuliwi kimasilahi?

Kikwava

JF-Expert Member
Sep 6, 2015
1,121
527
Habari.

Kwasasa dunia inafanya mapitio ya mitaala ya kufundshia/kujifunza huko mashuleni, huku swala la elimu za walimu ambao ndio wadau wa mitaala hiyo likiwa gizani. Kwa mfano, kwa Tanzania muundo wa kiutumishi wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaanzia elimu ya cheti hadi shahada ya kwanza tu, ambapo mwalimu akiwa na shahada ya pili (masters/PhD), mfumo haumtambui kimasilahi na kimuundo, tofauti na nchi zingine kama Kenya, South Africa, Nigeria, Zimbabwe na kwingineko.

Serikali ingelitazama hili swala kwa jicho la utatu kwa kuwaandalia muundo wa kiutumishi na kimasilahi walimu wenye shahada ya pili (masters/PhD) waliopo huko mashuleni. Ifikie kipindi sasa iwe ni kawaida kumwona mwalimu mwenye PhD anafundsha shule za msingi huko. Hii ishu italeta mapinduzi makubwa sana kwenye idara ya elimu na ualimu hasa huko mashuleni, tofauti na sasa ambapo mwalimu akishapata shahada ya pili tu huanza kuomba kuhamia idara zingine ambapo anaona atapata maslahi kulingana na elimu aliyonayo. Wakati huo elimu yake (masters/PhD) ingetambulika kimuundo na kimasilahi, angepata utulivu kituoni pale alipokuwa anafundisha bila kutafuta fursa mahali pengine.

Napenda kuwasilisha.
 
Habari.

Kwasasa dunia inafanya mapitio ya mitaala ya kufundshia/kujifunza huko mashuleni, huku swala la elimu za walimu ambao ndio wadau wa mitaala hiyo likiwa gizani. Kwa mfano, kwa Tanzania muundo wa kiutumishi wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaanzia elimu ya cheti hadi shahada ya kwanza tu, ambapo mwalimu akiwa na shahada ya pili (masters/PhD), mfumo haumtambui kimasilahi na kimuundo, tofauti na nchi zingine kama Kenya, South Africa, Nigeria, Zimbabwe na kwingineko.

Serikali ingelitazama hili swala kwa jicho la utatu kwa kuwaandalia muundo wa kiutumishi na kimasilahi walimu wenye shahada ya pili (masters/PhD) waliopo huko mashuleni. Ifikie kipindi sasa iwe ni kawaida kumwona mwalimu mwenye PhD anafundsha shule za msingi huko. Hii ishu italeta mapinduzi makubwa sana kwenye idara ya elimu na ualimu hasa huko mashuleni, tofauti na sasa ambapo mwalimu akishapata shahada ya pili tu huanza kuomba kuhamia idara zingine ambapo anaona atapata maslahi kulingana na elimu aliyonayo. Wakati huo elimu yake (masters/PhD) ingetambulika kimuundo na kimasilahi, angepata utulivu kituoni pale alipokuwa anafundisha bila kutafuta fursa mahali pengine.

Napenda kuwasilisha.
Hao wanapaswa kua asstant lecturer vyuo vikuu sio sekondari tena, hiyo ndio misallocation of human resource
 
Hao wanapaswa kua asstant lecturer vyuo vikuu sio sekondari tena, hiyo ndo mis allocation of human resource
Ila Hawa Walimu wangetambuliwa kimasilahi na kimuundo wangebaki mashuleni pale pale wanapofundisha na kuondoa dhana ya jamii kuwa Walimu ni Watumishi wenye Elimu ndogo. Wanaondoka mashuleni kwa kukosa masilahi yanayoendana na Elimu zao.
 
Wanawatambua pale wanapotaka kuwapa vyeo tu!

Tena wanawachukia kiaina hasa maafisa elimu wa WILAYA kuhisi wanataka vyeo vyao!
Hii yote yakuwekeana chuki itaondoka endapo Serikali itaanza kuwatambua Walimu wenye Masters kimasilahi bila kujali yupo nafasi gani.. vinginevyo watapigwa fitna mpaka kuathri utendaji kazi wao.
 
Ni mambo muhimu ya kutazama katika taifa letu. Akina "unanijua mimi ni nani" hawatafurahi wakiona mtu mwenye elimu zaidi yao. Afisa elimu wa wilaya ana degree, hata penda kuona waalimu waliomzidi elimu wilayani kwake. Naona kielimi tuishi kijeshi, tumechoka sasa. Ni marufuku katika shule ya sekondari mkuu wa idara awe na elimu ndogo kuliko anaowaongoza.
 
Habari.

Kwasasa dunia inafanya mapitio ya mitaala ya kufundshia/kujifunza huko mashuleni, huku swala la elimu za walimu ambao ndio wadau wa mitaala hiyo likiwa gizani. Kwa mfano, kwa Tanzania muundo wa kiutumishi wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaanzia elimu ya cheti hadi shahada ya kwanza tu, ambapo mwalimu akiwa na shahada ya pili (masters/PhD), mfumo haumtambui kimasilahi na kimuundo, tofauti na nchi zingine kama Kenya, South Africa, Nigeria, Zimbabwe na kwingineko.

Serikali ingelitazama hili swala kwa jicho la utatu kwa kuwaandalia muundo wa kiutumishi na kimasilahi walimu wenye shahada ya pili (masters/PhD) waliopo huko mashuleni. Ifikie kipindi sasa iwe ni kawaida kumwona mwalimu mwenye PhD anafundsha shule za msingi huko. Hii ishu italeta mapinduzi makubwa sana kwenye idara ya elimu na ualimu hasa huko mashuleni, tofauti na sasa ambapo mwalimu akishapata shahada ya pili tu huanza kuomba kuhamia idara zingine ambapo anaona atapata maslahi kulingana na elimu aliyonayo. Wakati huo elimu yake (masters/PhD) ingetambulika kimuundo na kimasilahi, angepata utulivu kituoni pale alipokuwa anafundisha bila kutafuta fursa mahali pengine.

Napenda kuwasilisha.
Suala la mwenye PhD kufundisha sekondari au primary ni wazimu wa hali ya juu sana.
 
Ni mambo muhimu ya kutazama katika taifa letu. Akina "unanijua mimi ni nani" hawatafurahi wakiona mtu mwenye elimu zaidi yao. Afisa elimu wa wilaya ana degree, hata penda kuona waalimu waliomzidi elimu wilayani kwake. Naona kielimi tuishi kijeshi, tumechoka sasa. Ni marufuku katika shule ya sekondari mkuu wa idara awe na elimu ndogo kuliko anaowaongoza.
Ndo hapo Sasa unakuta afsa elimu / mratibu ana elimu ndogo kuliko Walimu wake..anakosa kujiamini anaanza Vita Sasa😄
 
Kwa kuzingatia Aina ya Walengwa/Wateja/Wanafunzi, Ukubwa wa kazi yenyewe na Mazingira tuliyopo KAZI YA UALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI elimu ya DIGRII MOJA INATOSHA. zaidi zaidi hao walimu walipaswa kujikita kwenye kwenda kujipatia mafunzo mafupi ya Mbinu za ufundishaji. Elimu ya Masters nk nk hazina nafasi kwa Kiwango hicho cha kazi. Workload ya Ualimu haiiitaji hizo Masters zenu. Msilazimishe kuuua sisimizi kwa AK 47
 
Suala la mwenye PhD kufundisha sekondari au primary ni wazimu wa hali ya juu sana.
Ndo hapo Sasa watafanyaje unakuta mtu ana masters na anasifa ya kwenda kufundsha vyuo likini akiandika barua kuomba kuhamishwa wakuu wake wa idara wanamwambia hawamruhusu kwasabu Walimu wachache..kuondoa hili Bora serikali iwape masilahi ya kimuundo na kiutumishi hukohuko mashuleni wanakofundsha.
 
Back
Top Bottom