SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,151
- 7,921
Watanzania tuna hulka ya kupuuzia mambo ya msingi na kuna katabia kalijengwa na kameota mizizi ambapo ukihoji ukagusa maslahi ya watu fulani wanajaribu kukunyamazisha unaambiwa "acha ujuaji". Matokeo yake watu wanaogopa kuuliza maswali ya msingi na makosa yanajirudia kama siyo matatizo kuwa makubwa zaidi.
Siku chache tu kabla ya ufunguzi wa AFL, zilitoka taarifa kuwa Rwanda ni moja ya wadhamini wakuu wa AFL na kwamba wachezaji wa timu zote shiriki watavaa nembo ya "Visit Rwanda" katika bega.
Hii ilileta minong'ono na nakumbuka kuwakumbusha wale walioona kuwa hili ni jambo dogo msije kushangaa miaka 20 ijayo baadhi ya vitu vya Tanzania ikiwemo Dar es Salaam au hata Simba SC vikadhaniwa vipo Rwanda na itakuja kuhitajika nguvu kubwa kurekebisha huo mtazamo. Wengi hatujui Kenya walitumia mbinu gani mpaka kuiaminisha dunia kuwa Mt. Kilimanjaro uko Kenya ila inawezekana zilikuwa ni mbinu zinazofanana na hizi.
Anyway, ingekuwa vizuri tukajua nini kilipelekea Simba katika game ya marudiano kule Misri kusitisha uvaaji wa nembo hiyo na ilileta athari gani katika makubaliano yaliyokuwa yameshafikiwa kati ya Simba, TFF na waandaaji wa AFL. Unaweza kuta kwa kukiuka mkataba wa ushiriki, Simba ilipoteza haki za maokoto waliyoahidiwa kutoka AFL na yamepelekea mvurugano tunaouona sasa hivi Msimbazi. Kama hili lilitokana na shinikizo la Serikali, hili linaweza kuathiri ushiriki wa Simba na timu zingine za Tanzania katika mashindano yajayo ya AFL.
Jana Simba imekabidhiwa tuzo ya kuwa na mashabiki bora wa AFL na tuzo waliyopewa ina maandishi makubwa ya VISIT RWANDA. Popote ambapo Simba inapost picha ya tuzo hii, tunaitangaza Rwanda tena kwa ukubwa kuliko hata nembo katika jezi.
Hatuwezi kujifunza kwa kufukia makosa au maamuzi kama haya chini ya kapeti. Yawekeni wazi tuyajadili kwa pamoja, hii ni nchi yetu sote. Wengine hatujabahatika tu kupata teuzi huko serikalini ila tuna mawazo yanayoweza kuisaidia nchi.
Nasubiri kuambiwa nipunguze ujuaji.
Siku chache tu kabla ya ufunguzi wa AFL, zilitoka taarifa kuwa Rwanda ni moja ya wadhamini wakuu wa AFL na kwamba wachezaji wa timu zote shiriki watavaa nembo ya "Visit Rwanda" katika bega.
Hii ilileta minong'ono na nakumbuka kuwakumbusha wale walioona kuwa hili ni jambo dogo msije kushangaa miaka 20 ijayo baadhi ya vitu vya Tanzania ikiwemo Dar es Salaam au hata Simba SC vikadhaniwa vipo Rwanda na itakuja kuhitajika nguvu kubwa kurekebisha huo mtazamo. Wengi hatujui Kenya walitumia mbinu gani mpaka kuiaminisha dunia kuwa Mt. Kilimanjaro uko Kenya ila inawezekana zilikuwa ni mbinu zinazofanana na hizi.
Anyway, ingekuwa vizuri tukajua nini kilipelekea Simba katika game ya marudiano kule Misri kusitisha uvaaji wa nembo hiyo na ilileta athari gani katika makubaliano yaliyokuwa yameshafikiwa kati ya Simba, TFF na waandaaji wa AFL. Unaweza kuta kwa kukiuka mkataba wa ushiriki, Simba ilipoteza haki za maokoto waliyoahidiwa kutoka AFL na yamepelekea mvurugano tunaouona sasa hivi Msimbazi. Kama hili lilitokana na shinikizo la Serikali, hili linaweza kuathiri ushiriki wa Simba na timu zingine za Tanzania katika mashindano yajayo ya AFL.
Jana Simba imekabidhiwa tuzo ya kuwa na mashabiki bora wa AFL na tuzo waliyopewa ina maandishi makubwa ya VISIT RWANDA. Popote ambapo Simba inapost picha ya tuzo hii, tunaitangaza Rwanda tena kwa ukubwa kuliko hata nembo katika jezi.
Hatuwezi kujifunza kwa kufukia makosa au maamuzi kama haya chini ya kapeti. Yawekeni wazi tuyajadili kwa pamoja, hii ni nchi yetu sote. Wengine hatujabahatika tu kupata teuzi huko serikalini ila tuna mawazo yanayoweza kuisaidia nchi.
Nasubiri kuambiwa nipunguze ujuaji.