Kwanini siku hizi Bar hazina watu?

Kwanini siku hizi Bar hazina watu?

lendila

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2012
Posts
5,805
Reaction score
4,374
Wanajamii mimi ni mnywaji mzuri sana wa bar tofauti tofauti, lakini cha kushangaza siku za hivi karibuni nikienda bar watu wamepungua sana kwa kiasi kikubwa.

Anzia bar kubwa kama Rozlsi Garden,Corner bar, Break point, Igo bar watu , Uhuru Peak bar,Masai club, Jakalanda pub,.MK bar kote huko watu hamna na bar nyingine nyingi Dar.

Swali, je ni uchumi umeyumba au ni bar zimekuwa nyingi?

Swali la pili, ni watu wameamua kuokoka na kumrudia Mungu?

Wanajamii naombeni tusaidiane maoni.
 
Tatizo pesa zote zimeibiwa na kina pinda na kundi lake
Na afadhali zile za Epa walipiga zikaingia kwenye mzunguko lakini hizi za Pinda na Werema wameenda kuzichimbia nje
Ndio maana unaona hata serekali haina pesa za kununua dawa,sasa kama dawa hamna nchi nzima hizo bia zinanyweka vipi?
Tusubiri subiri uchaguzi ukaribie waende kwenye machimbo yao walipoziifadhi hizo pesa walete mtaani kuhonga watu hapo utaona bar zote tanzania zinajaa na watu wanaongea siasa!!
 
Tatizo pesa zote zimeibiwa na kina pinda na kundi lake
Na afadhali zile za Epa walipiga zikaingia kwenye mzunguko lakini hizi za Pinda na Werema wameenda kuzichimbia nje
Ndio maana unaona hata serekali haina pesa za kununua dawa,sasa kama dawa hamna nchi nzima hizo bia zinanyweka vipi?
Tusubiri subiri uchaguzi ukaribie waende kwenye machimbo yao walipoziifadhi hizo pesa walete mtaani kuhonga watu hapo utaona bar zote tanzania zinajaa na watu wanaongea siasa!!

Inawekana wakati wa epa nyumba zilipanda bei na wananchi walifaidika sana, mkuu umesama kweli, pesa ziko ulaya zimeficha
 
Wana jamii mm ni mnywaji mzuri sana wa bar tofauti tofauti, lkn cha kushangaza siku za hivi karibuni nikienda bar watu wamepungua sana kwa kiasi kikubwa, anzia bar kubwa kama rozi gaden, kona bar brek point, igo bar watu , uhuru peak bar masai clabu jakalanda pub, mk bar, kote huko watu hamna,na bar nyingine nyingi dar, swali je ni uchumi umeyumba au ni bar zimekuwa nyingi? Swali la pili ni watu wameamua kuokoka na kumedia mungu? Wana jamii naombeni tusaidiane maoni

Wewe kweli cha pombe, bar zote za Dar unazifahamu?
 
Mmmh! watu wengi ni wagonjwa wa maradhi mbalimbali kuanzia malaria, pressure, figo, uhanithi, kisukari, HIV na ugumba. Hivyo, baadhi ya masharti wanayopewa na madaktari wao kutibu maradhi yao ni kuacha kunywa pombe, hence low attendance. Acha mwenyewe leo kunywa pombe kabla hujaambiwa na dk. wako uache kunywa pombe. Watu wamegeukia kunywa Tanga fresh na mlonge, na kula matunda tu.
 
pesa zote kwenye kampeni za ccm. hili swali ungemwuliza kinana na nape.
 
Siku hizi wengi wanacheza viwanja vya nyumbani. Bia 2,3 utaenda kulala zako.
Haya ndiyo madhara ya kuwepo kwa shule za kata. Kila familia ina mtoto anayesoma sekondari, hivyo lazima alipe ada, michango, nauli kila siku na hela za matumizi. Hii inapunguza idadi ya beer kwenye familia. Hata kama huna mtoto wako, utapigiwa cm na dada yako kijijini kuwa mpwa wako kafaulu anatakiwa ada, michango, dawati, unifomu, n.k. Balaa gani hili walahi!
 
Ila kuna ukweli coz kiwanja changu "masai ya kino karbia na uhuru peak" watu wamepungua. But kuna mademu wakareeee ndo maana huwa cpakoci
 
Back
Top Bottom